CHUO CHA KUTAFAKARI NA KUTAFSIRI MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA TAKATIFU) Zab 1:1-3).2Timotheo 3:14-17.2Petro 1:21: Rhobinson S.Baiye/rhobinsons.blogspot.com/ rhobinsonsaleh1@gmail.com / Whatsapp 0764127531/ 0683476510/ Mwanza Tanzania Andiko Kuu La Huduma Ezekieli 3:1-3
Thursday, June 4, 2020
KANISA NA UWAJIBIKAJI WAKE
A.Kanisa
Na Uwajibikaji
Mwanzilishi
Wa Kanisa.
Kwa kufahamu
mwanzilishi wa kanisa,Biblia ina majibu
sahii.Math 16:18, inasema kwamba Nami nakuambia Wewe ndiwe Petro,na juu
ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu;wala milango ya kuzimu
haitalishinda,Andiko hili linamaanisha kwamba mwanzilishi wa kanisa ni Yesu Kristo.
Na
katika hili Yesu aliwajibika katika mambo ya roho na katika mambo ya mwili au
ya kijamii na kulirithisha kanisa kuwajibika,katika mambo ya roho na katika
mambo ya kijamii pia.Fahamu kwamba tunajifunza mbinu za kuimarisha na
kustawisha kanisa la mahali.Na kanisa lolote lile la mahali haliwezi kuimarika
na kustawi bila kuwajibika kwa kutafuta mbinu na kuimarika na kustawi
kwake.kuwajibika katika mambo yake kama kanisa, na kuwajibika katika mambo ya
kijamii au uma.
Mungu
anaupenda ulimwengu na hakomi kuhusika nao:Dhamira hii ya ndani inamaanisha
makanisa kushiriki katika sehemu za umma.Mungu aliumba dunia kwa njia ya Neno
na akalipa uhai kwa njia ya Roho.Kanisa linaitaji kuwa na mafanikio maendeleo
ili kumiliki kutawala fedha pesa na mali yaani kanisa kuwa na uchumi wa hali ya
juu sana.Kwamaana kanisa litakapo miliki na kutawala pesa na mali na watu wengi
nilazima kanisa litaimarika na kustawi sana. Na kanisa ili limiliki pesa na
mali nilazima kanisa yaani watu wa wajibike katika kujitoa au kutoa pesa zao
mali zao nguvu zao,michango mbalimbali katika kanisa,kwa kufikia mafanikio ya
kuimarisha na kustawisha kanisa la mahali.Kama tulivyoona katika kanisa na maono thabiti.Kwa maana kanisa lisilokuwa na maono haliwezi
kuwajibika kwa kuwa halina dira ramani na mwelekeo.Kanisa laweza kuwajibika kwa
kutimiza mambo kama haya na yanayofanana na haya.Mfano kanisa laweza kuimarika
kama mambo haya yakifikiwa.
A.Maendeleo
Ya Kiroho
Kuhubiri
injili ya Kristo Yesu popote ili kufungua makanisa kwa kupanua kazi ya Mungu.
Kufundisha
waamini na kukulia neno.
Kukuza
na kuendeleza huduma na karama zilizomo ndani ya watumishi na viongozi na
waamini.
Kuwatuma
watumishi na viongozi katika makanisa ili kufanya kazi ya Mungu.
Kubariki
watoto.
Kubatiza.
Kumega
mkate (Meza ya Bwana)
Kubariki
watumishi na viongozi.
Kudumu
katika upendo.
Kudumu
katika umoja
Kudumu
katika mshikamano
Kudumu
katika maombi
Kudumu
katika imani thabiti.
B.Maendeleo
Ya Kijamii (Kimwili)
Kanisa
ni vema kuwajibika katika maswala ya kijamii yaani katika mambo ya kimwili
pia.Kwa maana biblia inasema kwamba mwili pasipo roho umekufa na roho pasipo
mwili imekufa.Katika mambo yanayoleta afya ya kanisa ni kama haya. Kutengeneza
miradi mikubwa ya kanisa.
Kujenga
majengo (mahekalu)
Kujenga
shule za chekechea,shule za msingi,shule za sekondari,na vyuo.
Kujenga
zahanati
Kujenga
vituo vya kulelea watoto yatima.
Kusaidia
wasio jiweza’
Kusaidia
wafungwa.
Kusaidia
wajane
Kumiliki
vyombo vya mziki.
Vyombo
vya usafiri.Magari,Ndege,nk
Kuwawezesha
watumishi na viongozi katika kanisa.
Internent
Café
Stationeries
Computer
training Centers
Yumba
za kupangisha
Nyumba
za kulala wageni
Vyobo
vya habari kama Radio,Tv,Stations
Mifugo
mbalimbali.
Mashamba
Zana
za uvuvi.
Maduka
nk.
Hiyo
ndiyo dira yaana mwelekeo wa kuliimarisha na kulistawisha kanisa ya mahali.
Ni
neno la kuaminiwa mtu akitaka kazi ya askofu atamani kazi njema.1Tim 3:1.Je!
Umejitafutia mambo makuu? Usiyapate;kwa maana tazama,nitaleta mabaya juu ya
wote wenye mwili,asema Bwana;lakini roho yako nitakupa iwe nyara,katika mahali
pote utakapokwenda. Yer 45:5.Wakristo wengi husita katika habari ya
kutazamia au kutaka kazi ya kuwa kiongozi.Hawana uhakika kama ni vizuri kwa mtu
kutafuta huduma ya kuwa kiongizi.Hufikiri ni afadhali kazi ya uongozi imtafute
mtu kuliko mtu kuitafuta kazi.Je,siyo hatari kumpa mtu aliye na tabia ya kunai
makuu? Je, hakuna ukweli fulani katika usemi usemao kwamba,kunai makuu ni
udhaifu unaowaaribu watu wenye akili nyingi?. Ni kweli si vema mtu mkristo
kunai makuu kwa faida yake mwenyewe.Lakini fahamu kwamba Biblia inaturuhusu
kuzitaka karama zilizo kuu yaani karama zile tuzipendazo kila mmoja wetu.Hata
hivyo hakuna karama ambayo ni nzuri au kuu kuliko nyingine,bali karama na
huduma itakuwa kuu kwa Yule aitakayo zaidi.Yoh 4:10,Md 8:20,11:17,Rum
1:11,5:15,6:23,11:29,12:6,1Ko
1:7,12:1,4,9,28,31,14:1,12,2Kor
1:15,8:20,9:5.
Tunaposema
kwamba kiongozi na kuwajibika kwake tunamaanisha kuzingatia na kutekeleza
yanayomuhusu yeye kama yeye.Fahamu kwamba kuna uongozi na kiongozi wa
uongozi.Kiongozi ndiye anayeitwa mtumishi kiongozi,ikimaanisha mtumishi
kiongozi wa uongozi,katika shirika na katika kanisa pia.Uwajibikaji wamwanzoni
kabisa wa kiongozi ni .
Kusikia
kabla anaowaongoza hawajasikia.
Kufika
kabla ya anaowaongoza hawajafika.
Kufanya
kutenda kabla ya anaowaongoza hawajatenda.
Kushiriki
kabla ya anaowaongoza hawajashiriki.
Kushika
na kukusa kabla ya anaowaongoza hawajashika na kukusa.
Kusema
na kunena kwabla ya anaowaongoza hawajasema na kunena.
Kuyabeba
maono kuliko ye yeto kati ya anaowaongoza.
Ongoza
Kwa Tabia Na Sifa Za Kiongozi Wa Kiroho.
Anayetamani
kuongoza na anayeongoza wengine kama Mkristo, lazima ajifunze kwa Kristo.Kristo
hakuongoza kwa matakwa yake mwenyewe wala kwa vitisho bali kwa maadili.Hata
hivyo Yesu Kristo alifundisha wanafunzi wake jinsi ya kuongoza kwa kufuata wema
wa Mungu na maadili ya Neno la Mungu.Yesu alitumia Neno la Mungu kuwa mwongozo
katika kufundisha jinsi ya kuishi kwa maadili milele. Jitieni nira
yangu,mjifunze kwangu;kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo;nanyi
mtapata raha nafsini mwenu.Mathayo 11:29.
Ni
wajibu wetu kujifunze kwa Yesu Kristo kwa maana yeye ndiye kichwa cha kanisa na
mwenye maono makubwa juu ya kanisa lake.Na pia lazima tujifunze kwake yeye aliye mwalimu mkuu
wa kanisa tena Ustadi wake kama kiongzi wa watu na kanisa ni kiongozi
mtumishi.Kwa maana Kristo hakuja kutumikiwa bali kutumika.Mathayo 20:26-28
(28) Yesu Kristo aliongoza kwa kutumikia wengine.Upole wake na upendo wake
na moyo wa kutumika uliwavutia wote aliowaongoza.Yesu hakupima ukuu wa mtu kwa
watumishi aliokuwa nao,bali kwa wingi wa watu aliotumikia.Bilashaka Yesu
alitimiza wajibu wake na kuutimiza unabii wa Isaya.Isaya 53:1-12.
Alitabiriwa
atakuwa mfalme, lakini ni mfalme mtumishi.Lakini katika wakati wetu watumishi hawataki kuwa
watumishi bali Wafalme wanao
tumikiwa.Yesu alikuja kwa sababu ya utumishi utumwa.Wafilipi 2:6-7.Yesu
Kristo alifanya jambo ambalo lilionyesha wazi kwamba yeye ni kiongozi mtumishi
mwenye kujishusha,wakati alipowatawaza wanafunzi wake miguu yao.Yohana
13:4-5.aliwafundisha kwa mfano wake mwenyewe.Na funzo hili haliwezi
kusahulika kamwe katika maisha ya mtumishi ambaye ni kiongozi mtumishi.Yesu
alipiga magoti na kutawadha miguu ya wapendwa wake kwa unyenyekevu mkubwa.Ni
vema kujifunza kanuni za kuishi katika utumishi utumwa kutokana na Yesu Kristo
Bwaana wetu,alipotawadha miguu michafu ya wapendwa wake.
Mtumishi
Kiongozi Na Maisha Ya Unyenyekevu.
Ni vema kuzama kwa kina katika maisha ya mtumishi kiongozi.Fahamu
kwamba kiongozi Ni Kiongozi wa viongozi na uongozi
na watu.Kwanza tuliweke sawa na kulifafanua jina au neno Kiongozi na maana yake
na matumizi kake.Hapa kila herufi ina maana yake tujaribu kuona maana ya kila
herufi kwa maana neno kiongozi ni kifupi cha maneno ambayo yamebeba wajibu wa
kiongozi.
KIONGOZI.( K ) Ina maanisha Kielelezo.Kielelezo ni mtu au kitu
halisi mfano wake kitumiwacho kuonyeshea au kuelekeza kitu halisi; ni mchoro au
picha na ni tendo la kuelekeza au kuonyesha
kitu au jambo fulani.Hapo maana hiyo inatuonyesha kwamba kiongoza hana
budi kuwa kielelezo kwa wale anao waongoza inampasa kuwa kelelezo ili kutimiza
wajibu wake na kuwa mwajibikaji.Kila anayetaka na kutamani kazi ya mtumishi
kiongozi yampasa kujifunza kwa Yesu aliye mtumishi na kiongozi na mwalimu mkuu
aliye kielelezo chetu.Yohana 13:4-5,15,1The 1:7,2The 3:7-10,1Timotheo
1:16,2Timotheo 1:13,Tito 2:7,1Petro 2:21,1Timotheo 4:12.
KIONGOZI.Katika kufafanua na
kutafsiri kirefu cha neno na jina Kiongonzi herufi ( I _) Ina beba au kuwakilisha
neno Imani ikimaanisha kwamba kiongozi
lazima awe na imani thabiti isioyumba na kuyumbisha bali ni mtu kiongozi aliye
na imani yenye viwango kuzidi wale anao waongoza.Kwanza kumbuka,Basi imani
ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana.Maana
kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.Kwa imani twafahamu yakuwa ulimwengu uliumbwa
kwa neno la Mungu,hata vitu visivyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo
dhahiri.Waebrania 11:1-3.Katika hili mtumishi kiongozi,anatakiwa kuwa na
hakika na mambo yaliyomo katika maono anayoyabeba.Haijalishi kwamba hayaonekani
kwa macho ya wale anaowaongoza.Yampasa kuwaaminisha na kuwafikisha katika
kiwango cha imani aliyonayo,na kuakikisha
kwamba wame kuwa na hakika na
kile kinacho aminiwa na kiongoza.Hapo kiongozi atapata njia ya kuwajibika
katika kuliimarisha na kulistawisha kanisa.Kumbuka mfano ambao Yesu Kristo
aliowambia wanafunzi wake akisema.Akawaambia,mfano mwingine,akisema,Ufalme
wambinguni umefanana na punje ya haradali,aliyoitwaa mtu akaipanda katika
shamba lake;nayo ni ndogo kuliko mbengu zote;lakini ikiisha kumea,huwa kubwa
kuliko mboga zote,ikiwa mti,hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi
yake Mathayo 13:31-32.Kiongozi inampasa awe na imani ya kuhamisha milima yaani
mambo yanayoshindikana kutekelezeka.Mathayo 17:20.
KIONGOZI:Katika neno au sifa hii
kiongozi,twende tukatafari herufi hii kama imebeba hapo. ( O ) Katika neno hii kiongozi
limebeba (o) mbili na kila moja ina maana yake,hebu tuone maana ya (o) ya mwanzoni.O.Ina
maana ya Onyesha njia likitokana na kitenzi kuonyeshi.Kwa hiyo kila kiongozi ni
mtu nayewajibu wa kuonyesha wale anaowaongoza njia ya kupita au ya
kuenenda.Tujifunze kutoka kwa mwalimu mkuu ambaye ni Yesu Kristo ambaye ndiye
kiongozi aliyeonyesha wanafunzi wake pamoja na ulimwengu wote.Basi mimi
nikienda na kuwaandalia mahali,nitakuja tena niwakaribishe kwangu;ili nilipo
mimi,nanyi mwepo.Nami niendako mwaijua njia.Tomaso akamwambia,Bwana,sisi
hatujui uendako;nasi twaijuaje njia?Yesu akawaambia,Mimi ndimi njia,na kweli,na
uzima mtu haji kwa baba,ila kwa njia ya mimi.Yohana 14:3-6.Kwa sababu Yesu
alifahamu kwamba niwajibu wake kuwaonyesha njia wanafunzi wake na ulimwengu kwa
ujumla alifanya hivyo kama kiongozi.Inatufaa zaidi kujifunza kwake na kutimiza
wajibu wetu kama viongozi watumishi wa Mungu.Yesu aliweka wazi mambo matatu
Kwamba yeye ndie Njia yeye ndie Kweli yeye ndie Uzima. Akiwa na maana yakwamba
kila apendaye njia iliyo sahihi ya kwenda kwa Baba yampasa kumfuata yeye aliye
njia.Na yeye apendaye kufahamu kweli katika jambo lolote amwamini yeye aliye
kweli.Na Yule apendaye kuona na kuishi katika uzima,hana budi kumwamini na
kuishi kama alivyo Kristo kwetu yeye ndiye uzima,mtu asie kufa milele.Viongozi
watumishi wa Mungu hawana budi kuonyesha wale wanaongozwa njia iwapasayo.
KIONGOZI. Katika hili herufi inayofuata ni ( N ) Herufi hii katika zile
zinazokamilisha neno kiongozi linamaana ya kuwa kiongozi ni mtu ambaye aliyejaa
Neno la Mungu lenye kutamanika na watu na
Mungu pia.Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi,maarifa,tena yawapasa
watu kuitafuta sheria kinywani mwake;kwa kuwa yeye ni mjumbe wa BWANA wa
majeshi.Hayo ni maneno ya Mungu kutoka kwa mtumishi wake Malaki.Malaki
2:7.Jifunze kutoka kwa mwalimu na wenye kujaa maneno yenye kujenga kufariji
na kutia moyo.Basi kila asikiaye hayo maneno yangu,na kuyafanya,atafananishwa
na mtu mwenye akili,aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;mvua
ikanyesha,mafuriko yakaja,pepo zikavuma,zikaipiga nyumba ile,isianguke;kwa
maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.Na kila asikiaye hayo maneno yangu
asiyafanye,atafananishwa na mtu mpumbavu,aliyejenga nyumba yake juu ya
mchanga;mvua ikanyesha,mafuriko ya kaja,pepo zikavuma ,zikaipiga nyumba ile,ikaanguka;nalo
anguko lake likawa kubwa.Mathayo 7:24-27.
KIONGOZI: Tunaendelea na ufafanuzi
wetu wa neno kiongozi kwa kila herufi jinsi inavyowakilisha na kubeba utumishi
wa mtumishi kiongozi katika kuongoza kwake.Na herufi ( G ) ina maana ya Geuza Neno geuza ni neno
litokanalo na kitenzi kugeuza kikimaanisha kubadili kitu kiwe katika hali au
sura na mwonekano na Umbo jingine.Ni Kufanya umpande uliokuwa chini uwe juu au
uliokuwa mbele uelekee nyuma.Hapa ina beba dhamana ya mtumishi kiongozi
kubadili mambo kwa kuyaboresha zaidi.Yesu anasemaje kwa hili na anahusikaje
katika hili? Mungu alimtuma mwanaye kwa makusudi ya kugeuza mambo kwa
kuyaboresha na kuyaandaa ili yawe kama Mungu alivyokusudia yawe.Maana Mungu
hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu,bali ulimwengu uokolewe
katika yeye.Yohana 3:17.
Ukitafakari sana torati kama ilivyoandikwa na Musa Kumb
31:9,Musa akaiandika torati hii,akawapa makuhani,wana wa lawi,waliolichukua
sanduku la agano la Bwana,na wazee wote wa Israeli.Utangundua kwamba imejaa
hukumu.Kutoka 21:1-36.22:1-31,23:1-9
Bilashaka utaamini kwamba pia torati ilikuwa imeruhusu kulaaniwa
kwa mtu.Kumb 27:15-26.
Ni vema kujifunza kwa mwalimu mkuu Yesu Kristo hijapokuwa kuna watumishi wengi katika Biblia wafahao
sisi kujifunza kwao.Kwa nini Yesu ni muhimu sana? Kwa kuwa Yesu ndiye mwisho wa
sheria na wanashia.Rumi 10:4,Gal 3:24.Yesu Kristo kiongozi wa kufuatwa
na kujifunza kwake ni mfano wa kuwa kiongozi mwema aliye Geuza mambo na
kuyaboresha kabisa.Yesu aligeuza mambo mengi na kuyaboresha,lakini tutaona
machache ya kutuimiza zaidi.
Kuhusu hukumu,kama tulivyoona hapojuu katika Yohana 3:17.Maana
Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili aukumu ulimwengu,bali ulimwengu,uokolewe
katika yeye.Yesu alisemaje kuhusu hukumu? Mathayo 7:1-5. Yesu aligeuza ikimaanisha alileta badiliko hukumu
ikabadilika ikageuka kuwa upendo na msamaha kwa aliyekosa na kustahiki
hukumu.Mathayo 6:14.
Kuhusu kulaani Yesu alileta badiliko la kubariki kuliko
kulaani,Yesu ni kiongozi wa mfano wa pekee.Luka 6:24-36.
Ni kweli kiongozi ambaye ametokana na Mungu nilazima awe mtu wa
kugeuza na kuleta mabadiliko chanya katika uongozi wake.Viongozi ambao hawawezi
kugeuza mambo, Biblia inasema na kuwaita Mbwa bubu.Walinzi wakeni
vipofu,wote pia hawana maarifa;wote ni mbwa walio bubu,hawawezi kulia huota
ndoto,hulala hupenda usingizi.Naam,mbwa hao wana choyo sana,hawashibi kamwe;na
hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno;wote pia wamageuka upande,wazifuate
njia zao wenyewe,kila mmoja kwa faida yake,toka pande zote.Husema, Njoni,nitaleta
divai,Na tunywe sana leo,Sikukuu kupita kiasi.Isaya 56:10-12.Kiongozi
hugeuza mambo kwa kuandaa viongozi wapya,na kugawa madaraka inapobidi
kufanyahivyo. Luka 3:5.Kila bondo litajazwa,Na kila mlima na kilima
kitashushwa;Palipopotoka patakuwa pamenyoka,Na palipoparuzwa patalainishwa.Nilazima
kiongozi atendee haki herufi .O.
KIONGOZI. Herufi
( O ) ina wakilisha au inabeba wajibu
kiongozi kuongoza kwa kutangulia mbele wale anao waongoza .O,Ikimaanisha kwamba
kiongozi ni lazima kuwa mbele ya kundi au kikundi cha watu anaowaongoza kwa ili
kuwaelekeza pakwenda.Na neno ongoza na tendo kuongoza linamaanisha kuwa mkuu na
msimamizi wakila shughuli.Tujifunze kwa mwalimu mkuu Yesu Kristo anasemaje
katika hii.
Yohana
10:2-5,Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.Bawabu humfungulia huyo,na
kondoo humsikia sauti yake;naye huwaita kwa kondoo wake kwa majina yao,na
kuwapeleka nje.Naye awatoapo nje kondoo wake wote,huwatangulia;na walekondoo
humfuhata,kwa maana waijua sauti yake.wengine hawatamfuata kabisa,bali
watamkimbia;kwa maana hawajui sauti za wageni.Naamini
umepata jambo la msingi na la muhimu sana katika herufi O.viongozi hawana budi
kutangulia katika kila jambo. Rumi 2:17-24.
KIONGOZI.Katika herufi ( Z ) inawakilisha wajibu wakiongonzi katika
kuzingatia mambo.zingatia lina maana ya kutia moyoni yote ambayo ni maagizo ya
Mungu kwako na maazimio ya baraza kuu na kanisa.Wewe kiongozi unapozingatia kwa
kutuyumbisha.Kumbuka wakati kiongozi anaposimamia kundi la kiroho,ni mtu mwenye
kusimama mbele za Mungu kwa ajili ya watu na anasimama mbele za watu kwa ajili
ya Mungu.Luka 15:17.Jifunze kwa watumishi wa Mungu kama vile Musa,na Nehemia,Manabii,Mitum
E,walivyo
zingatia yawapasayo.
KIONGOZI. Herufi ( I )
Ina wakilisha na kubeba wajibu wa kiongozi wa kuimarisha na kustawisha kundi.Ni
wajibu wa kiongozi kuimarisha ikiwa na maana ya kutafutakundi liwe na nguvu ya
kiuchumi,nguvu ya umoja,nguvu ya kielimu,nguvu ya neno la Mungu liwe kwa wingi
ndani ya anao waongoza.Kiongozi ana wajibu wa kufanya kundi liwe madhubuti.1Fal
2:12,Zab 30:7,40:2.AYubu 4:4.Ezekieli 20:32.
Hicho
ndicho kirefu cha neno kiongozi.Na ili kanisa liimarike na kustawi nilazima
kanisa liwajibike na kiongozi awajibike na uwongozi uwajibike,hapo ndipo kanisa
la mahali litaimarika na kustawi sana.
rhobinsons.blogspot.com
rhobinsonsaleh1@gmail.com
Whatsapp.0764127531
Mwanza
Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UONGOZI BORA WA KIROHO
Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...
-
Sauti Ya Gombo International Ministries Network KUANDAA MAHUBIRI NA MAFUNDISHO YA NENO LA MUNGU ...
-
Sauti Ya Gombo International Ministries Network KUTAFAKARI NA KUTAFSIRI MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) NENO LA MU...
-
Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...
No comments:
Post a Comment