Tuesday, June 2, 2020

KANISA LENYE MAONO THABITI

 

KANISA NA MAONO THABITI

Yoeli 2:28  Ufunuo 1:9-20

Twasoma katika unabii wa Yoeli kwamba Hata itakuwa,baada ya hayo kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili;na wana wenu,wakike na wakiume,watatabiri,wazee wataota ndoto,na vijana wenu wataona maono.Na katika ufunuo wa Yesu kwa Yohana,Yohana anasema alikuwa katika roho na aliona maono.Je?maono au ono inamaana gani?

Maana ya maono

Maono au Ono ni picha ya mambo au vitu inayomjia mtu ubongoni mwake;ni taswira ambayo ya weza kuonekana au kujitokeza kwa njia ya dhamira safi au katika hali ya kuwa katika roho kama Yohana alivyoyaona maono akiwa katika roho.Kwa  maana nyingine yasema kwamba maono ni hali ya kuona mbele,ukilinganisha naya nyuma.mtu moja alisema kwamba maono ni daraja inayounganisha yaliyopo na yajayo.Kuna tofauti wa maona na ndoto,Ndoto ni matukio ya kale,Ni kumbukumbu  ya mambo ya kale.Lakini maono yanahusika na mambo yajayo.Ndoto inahusu  mambo yalivyokuwa,hali maono yanahusika na mambo yanavyoweza kuwa.Uzee na ujana ni maneno mawili yanayohusiana.Fahamu kwamba kuna vijana ambao huona tu vizuizi,na mawazo yao yako katika shida wanayoiona .Na ni wanaume wenye ndoto wanafikiri kizee,wakizingatia yaliyopita.Mwenye maono hufikiri mambo yanavyoweza kuwa Kiongozi  na kanisa lenye maono huona nyota,na kuamini kwamba ni yenye kuwa na Mungu,na ina nguvu za kusababisha mabadiliko.

Maono yatokayo kwa Mungu huleta mabadiliko,na maono hayo huona mafanikio katika siku za baadaye.

Nguvu Iliyomo Katika Maono Yatokayo Kwa Mungu.

Kanisa la mahali halipaswi kupuuza  nguvu zilizomo katika maono.Washirika wanaume na wanawake na vijana wenye maono hubadilisha ,mwonekano wa kanisa.Ni vema kanisa na watumishi pamoja na viongozi katika kanisa kujiuliza  maono tuliopewa na Mungu na kuyapokea ni yapi? Je tumeyaishi ya maono? Na kama kanisa la mahali halijui ono lao basi kanisa hilo na watumishi wake bado wanaishi bila kutambua wito wao.Basi kanisa hilo linaishi wasivyostahili kuishi.Katika maono mnanguvu za ajabu.Kile ambacho mtu alichokiona katika ono ndicho humpa moyo na mvuto wa kufanya au kuwajibika katika kutimiza majukumu yake ya kila siku,ili kufikia kile alicho kiona.Na kama kanisa la mahali halina maono inamaanisha kwamba kanisa hilo halina dira/ mwelekeo.Tunaweza kusema kwamba hutia nguvu katika ono lako,ikiwa utadumu katika ono hilo.Mungu hawezi kuweka ngvu katika ono lako kama haudumu katika ono lenyewe.Huduma na karama na wito wako ni kazi yake.Vivyo hivyo nguvu za kutekeleza ono zinatokana naye.

Kusudi La Ono/ Maono Katika Kanisa La Mahali. watumishi na viongozi katika kanisa la mahali,huendeleza shughuli zao za kila siku wakiwa na azimio la matarajio ya kufanikiwa.maono ya kanisa humpa kiongozi mwelekeo na majukumu katika siku zake,Kusudi la kuwa na maono ni kuweka mwelekeo dira ya Mungu katika mzunguko wa maisha ya kanisa,ili kuimarisha na kulistawisha kanisa la mahali.Fahamu kanisa ilinahitaji maono ono thabiti,na yatokayo kwa Mungu.

·      Maono yatokayo kwa Mungu hutoa mwelekeo kwa mtu.

·      Maono yatokayo kwa Mungu hutoa mwelekeo kwa jamii.

·      Maono yatokayo kwa Mungu hutoa mwelekeo kwa nchi.

·      Maono yatokayo kwa Mungu hutoa mwelekeo kwa ulimwengu.

·      Maono yatokayo kwa Mungu hutiisha kanisa.

Kumbuka kwamba watu wengi na makanisa mengi hayana mawazo ya hatima yao.Wengi wanaona tu wakati uliopo na vikwazo vyake.Fahamu kwamba katika shirika lolote,lazima pawepo na viongozi na wasimamizi.Na hufananishwa na kundi la wavumbuzi waliokuwa wakijaribu kutengeneza njia vichakani.Msimamizi alikusanya kundi lake akawapa visu,misumeno,na shoka kama vitendea kazi ya kutengeneza njia kwenye msitu mzito sana,Msimamizi alipoona mambo hayawezekani aliwambia kwamba basi yatosha na akapaza sauti na kuwa kataza kwamba wasiendelee na kazi hiyo eti kwamba wamepotea njia na kuelekea upande usiofaa.Huyo ndiye kiongozi ambaye anajali na kufahamu hatima ya sika za baadaye.Mungu ametupa wanaume kwa wanawake kuongoza kututoa katika msitu.Mfano wa Musa na Nehemia, Esta na Paulo walikuwa viongozi wenye maono.Walitoa  mwelekeo na kuakikisha kwamba wanafuata maono waliopewa na Mungu.Ni vema kuishi katika maono au ono ulilopewa na Mungu.

Kanisa Na  Umiliki Wa Ono Au Maono Yake.

Ni vema kila kanisa la mahali liweze kumiliki ono lake.Kufuatana na mazingira uzoefu,maono ya kanisa ya  yaweza kuwatofauti kulinga na mambo matatu muhimo.Mazingira ya kanisa,Uzohefu na Kiwango cha fikira na ujuzi wa mtumishi kiongozi.Lakini kumbuka haijalishi uko katika mazingira gani,wajibu wako ni kutimiza kile ambacho Mungu amekuitia kukifata.Kazi ya Mungu ndani ya kanisa na ndani ya watumishi na viongozi ni ono maono ambayo Mungu anayo juu ya kanisa na watumishi wake.Soma Malaki 2:Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa,tena yapasa watu kuitafuta sheria ya Bwana kinywani mwake,kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi.

Ni lazima kanisa lione  na kuamini na kumiliki ono lake.Kanisa likumbatie  ono lake kama kipawa na dira muhimu kutoka kwa Mungu.Mungu yuko tayari kushiriki na wewe katika ono la kanisa la mahali.Kanisa limiliki maono katika pande mbili muhimu.Maono katika hali ya kiroho (ibada) na maono katika hali ya kijamii ( kimwili ) Mambo haya utayaona kwa kina katika sura ya (10).

1.Kanisa La Mahali Kutimiza Ono Lake

Kanisa la mahali kwa kutimiza maono yake halina budi kuimiza viongozi na watumishi pamoja na waumini kulipenda kanisa na kulithani kanisa,katika kudumu katika upendo.1Kor 13:1-8,Upendo husababisha na kutoa msukumo wa kujitoa na kutoa malizake na nguvu zake kwa moyo bila kusukumwa.Kwa  kutimiza maono kanisa lazima lidumu katika umoja kwamaana umoja unanguvu na unapendeza sana Zaburi 133:1-4.Kanisa la mahali likiwa pamoja kwa umoja haliwezi kushindwa kutimiza maono yake.Soma katika sura ya pili ili ufahamu kwa kina kuhusu umoja.Hatuwezi kusahau mshikano katika kanisa ni jambo muhimu na lenyenguvu sana katika kutimiza maono ya kanisa la mahali mshikamano  hudhihirishwa na lugha na matendo na mwenendo.kwa kutimiza maono lazima kanisa lidumu katika maombi,na katika imani thabiti na   kumiliki uchumi ambao hulipa kanisa uwezo wa kifedha.Imani thabiti inahitajika katika kutimiza maono pamoja na mfumo unaofaa hufanya mambo kuwa mepesi na rahisi kufanyika.Kutambua na kuwa na mtazamo mzuri katika nyakati.Kwa kutimizwa kwa maono ni lazima maono yenyewe yaeleweke kwa maana kuna maono mengine hayaeleweki.Na kutoeleweka kwa maono huleta uzito wa kutotekelezeka kwa maono ambayo hayana mpangilio na hayaonyeshi mwelekeo.Kanisa lenyewe halina budi kuwajibika katika kutimiza maono yake.Watumishi na viongozi hawana budi kuwajibika kila mmoja katika nafasi yake ili kutimiza yale ambayo Mungu anahitaji kutimizia kanisa kupitia kwa kiongozi na mtumishi huyo.

2.Ono Maono Lazima Yaatamiwe.

Ni vyema kufahamu kwamba nilazima maono yaatamiwe.Mtu anapopokea maono kutoka kwa Bwana,huwa kuna msukumo wa kuanza kufanya kitu kwa haraka.Lakini  maono lazima yaatamiwe kama kuku anavyoatamia mayai yake siku (21).Tujifunze kwa Mungu aliyetuumba alikuwa na maono na mpango mzuri juu ya mtu na ulimwengu. Yohana 3:16-17.Lakini lakuzingatia ni kwamba Mungu aliatamia maono yake kuhusu ulimwengu na waulimwengu.Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.Nayo nchi ilikuwa ukiwa tena utupu,na giza ilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji;Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.Mungu ni Roho na roho ya Mungu ilitulia juu ya maono yake.Lakini makanisa mengi ya mahali pamoja na watumishi wake hawana utulivu katika maono,na ndio maana makanisa hayo hayaimariki na hayastawi.Ona jinsi maono ya Mungu yalivyokuwa makubwa na yenye uzito mkubwa sana.Tafakari jinsi ufalme wa mbinguni ulivyo,pamoja na ufalme wa anga ulivyo na ufalme wa dunia (ulimwengu) ulivyo.Hayo yote ndiyo maono ya Mungu.Ilibidi Mungu kuatamia maono yake ili yakomae na kuwiva.Nilazima watumishi na viongozi pamoja na washirika kuacha papara,wawe watulivu katika maono.Hata kama maono hayajadhihirika bado yaatamie moyoni mwako,na usiwe mwongeaji na mwenye kusema au kuyatangaza kabla ya wakati wake.Husi yakinahi maono yako yasiwe mzingo mzito kwako na uyapende maono yako.Yajue,yafahamu maono uliyonayo.

3.Maono Lazima Yashirikishwe

Ni vema watu washirikishwe maono ya kanisa ili yawe wazi na yafahamike na yaandikwe.Yatakapoandikwa na Watu kushirikishwa,kutakuwa na watu ambao wapotayari kujiunga na kuhudumu pamoja nanyi.kwa sababu ya kuwashirikisha watu.Kutakuwa na kundi kubwa ambalo litazaa makundi ambayo yatafanya kazi kubwa na kwa wepesi kuliko ambavyo ungefanya peke yako au peke yenu.Ukiwa mtu wa kufanya kila kitu peke yako hautaweza kufanya kitu cha maana katika dunia hii.Bali mtu anayeweza kuwaandaa wengine kutekeleza maono ya pamoja na mtu awezaye kuunda kikundi/vikundi anaweza kufanya kazi yenye maana kwa ufalme wa Bwana wetu Yesu Kristo.Biblia inasema kwamba,Na watu watano wa kwenu watawafukuza watu mia,na watu mia wa kwenu watawafukuza watu elfu kumi;na adui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.Mambo ya walawi 26:8.Hayo ni kwa sababu ya kushirikisha wengine maono tulionayo.Mmoja angefukuzaje watu elfu,Wawili wangefukuzaje elfu kumi,kama mwamba wao asingaliwauza,kama Bwana asingaliwatoa? Shirikisha vijana,wanaume,wanawake,maskini,matajiri,

 Wenye elimu mbalimbali,wasionaelimu,wazee,watu warika zote.Rasilimali zitatokana na watu hao kama watashirikishwa  kikamilifu.Chukua mda wa kuwaandaa na kuwaelimisha  ulichokiona unachokiona na kitakacho tokea.Wape nafasi na kuhudumu kwa uhuru.

2Kor 9:13,1Yohana 4:13.

 4. Maono Hujaribiwa.

Fahamu kwamba maono hujaribiwa kwa matatizo mengi,misiba ,uasi,yatakuweka katika migigiro na wengine kusema kwamba sio Mungu aliyekupa maono hayo bali ni miemuko yako tu.Kila aina ya hatua itachuliwa kinyume nawe unapoingia katika kutekeleza maono uliyopewa na Mungu.Mkeo/mmeo watoto wako wanaweza kuinuka kinyume na maono yako.Jaribu la kukosa watu muhimu katika maono uchumi kutokuwa sawa,jaribu la mapinduzi katika nafasi yako kama mbeba maono.La kukumbuka ni kwamba maono hujaribiwa kulingana na ukubwa na uzito wa maono ulivyo.Maono makubwa kujaribiwa kwa majaribu makubwa zaidi.Twaweza kuyaona na kujifunza kupitia maono ya Nuhu katika kutengeneza  Safina ono lilikuwa  Mwisho Wa kila mwenye mwili kuangamizwa  kwa Garika. Mwanzo 6:13.Abrahamu Kumbuka Abrahamu alikuwa na maono makubwa sana, mataifa yote kubarikiwa kutokana na uzao wake.Je wakumbuka majaribu aliyokumbana nayo? Mwanzo 12:1-.Tafakari kuhusu Musa Kutoka 3:1-Tafakari kuhusu Nehemia ,1:1- Tafakari kuhusu Paulo Md 9:1- Kujaribiwa kwa maono yetu katika kila hatua kusitukatishe tamaa wala kuogopa ya kwamba hatuwazi kuyafikia yale tuliyoyaona.

5.Maono Lazima Ya Dumishwe.

Kudumisha ni kuendeleza jambo.Inamaana kwamba Mungu anapokupa maono nilizima kuyadumisha maono ambayo umepewa na Mungu,Maono ni kitu muhumu sana

Na ni lazima kushikilia au kudumisha.Tazama  ono aliliopewa Yona kwaenda kuhudumia nchi ya Ninawi,lakini yeye alikwenda katika njia zake zingine.Matokeo yake adhabu ya Mungu ilimfikia Yona.Mungu akiamua kukupa maono huwa hajutii kwa nini nimempa mtu huyu maono haya kwa maana Mungu wetu ni Mungu ajuae,na anatujua sana,ndiyo maana hawezi kujutia.Hesabu 23:19.Tunapodumisha maono tunamfuraisha Mungu.Tuwe na mikakati ya kuwaandaa wengine ili maono yetu yapatekudumu.Na haijalishi tunapita kwenye shida na katika mafanikio lazima tudumishe maono.Ezekieli 29:18,Ayubu 24:22,Zaburi 89:29,85:5.( Luka 1:50)

6.Maono Lazima Yaanzishwe Na Mungu.

Maono sahihi  ni maono ambayo huanzishwa na Mungu mwenyewe.Katika wakati wetu huu,baadhi ya wajiitao watumishi wenye maono kutoka kwa Miungu lakini sio.Maono kamili kutoka kwa Mungu yanaweza kutoka au kukujia kwa njia tofauti na yalivyo watokea wengine.Ona Nuhu Mungu alimwambia,Abrahamu Mungu alisema naye  moja kwa moja,ona Musa aliona na kusema na Mungu moja kwa moja.Ona Yusufu yalimtokea katika ndoto.Je! maono uliyonayo yametokana na nani? Isaya  6:8-13,61:1-11, 41:10-18,

7.Maono Lazima Yawe Na Mipaka.

Kama tulivyoona maono ni kitu kizuri sana katika maisha yetu.Mungu anapokupa maono nitabia yake kukuwekea mipaka ya hayo maono.Twaweza kwenda kinyume na maono yenyewe hii ndiyo maana halisi ya mwanadamu.Jifunze kwa Yoshua mtumishi wa Musa,alivyoambiwa na Mungu baada ya Musa mtumishi wa Mungu kufa.Mungu alimwambia Yushua kwamba,Yoshua 1:1-9 (7-8)2 Wafalme 9:1-13.

8.Maono Ufunguo Wa Mafanikio.

Ni kweli maono ni ufunguo wa kufaulu.Kufaulu ni kupata,yaliyokusudiwa; ni kufanikiwa ni kushinda mtihani na nikufikia malengo.Na maono ni ufunguo wa kupata yanayokusudiwa na maono ni ufunguo wa kushinda mtihani na mitihani katika maisha.Maono ni ufunguo wa kufikia malengo.Biblia yasemaje kuhusu maono? Biblia inasema kwamba,Pasipo maono watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu Yule aishikaye sheria.Mith 29:18.Twaweza kujifunza kupitia Taifa la Israeli na manabii wa Mungu kwa ajili ya Taifa hilo.Na kupitia maono na kutoa unabii hizo zililifaa Taifa la Israeli.Maono ni dira na mwelekeo wa kanisa familia taifa.Mfano  ugonjwa wa CORONA,ulitangazwa kutoka katika taifa la watu wa China mnano Mwezi wa 12 ( ) Mwaka 2019. Ugonjwa huo ulisambaa Duniani kote,yaani katika kila Taifa duniani.Manabii katika mataifa mbalimbali walitoa unabii kupitia maono ambayo waliyaona kuhusu ugonjwa huo.Watawala yaani maraisi wa mataifa mbalimbali walitoa mwelekeo dira kwa ajili ya kushinda ugonjwa wa CORONA, COVID 19,Natamani ufahamu maono ya mtawala yaani Raisi wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania aliyeingia madarakani mnamo mwaka wa 2015.

Wakati,wa kisa cha kwanza cha Corona kutangazwa mnamo tarehe 16 mwenzi wa 3 mwaka 2020, Raisi JOHN JOSEPH POMBE MAGUFURI,aliutubia taifa kwamba wamlilie Mungu yaani Taifa la Tanzania kufunga na kuomba kwa muda wa siku tatu.Ijuma,Juma mosi na Juma Pili.Na matokeo chanya alipotokea Raisi huyo alitangaza tena na kuwaomba Watanzania kuomba maombi ya Shukrani kwa muda wa siku tatu.Ijuma ya tarehe 22-23-24/5/2020.Juma mosi na Juma Pili. Mataifa yalifaulu kupita maono.Fahamu maono ni mafunuo muhimu.

Kufa Kwa Maono

Tunayo  maono lakini fahamu kwamba maono uliyonayo yaweza kufa.Haijalishi usipokuwa makini maono yako yatakufa.Miaka kadha iliyopita mtumishi wa Mungu aitwaye BILL GOTHARD.alisema juu ya kufa kwa ono maono.Alieleza jinsi wanaume na wanawake walioteuliwa na Mungu walivyopitia vipindi vigumu vya giza,walipoona ugumu katika kutimiza ono la Mungu,kama vile Eliya alivyojificha ili asionekane na malkia Yule mkatili,Yezebeli.Eliya alikuwa na woga mwingi ingawa Mungu alimwonyesha uwezo wake akiwa katika mlima uitwao Karmeli.Eliya alikuwa amepoteza imani Mungu hasingefanya yale aliyosema naye.Fahamu kwamba kila kiongozi wakati mwingine hufikia hali ya kukata tamaa.Na katika kipindi hicho mtu mwenye maono hupoteza mwelekeo na maono na asipokuwa makini maono ni marehemu.Jua kwamba jambo hii ni muhimu sana katika maono.Ulicho nacho ni hakikisho la ono hilo.Unaweza kujiuliza tu,je?limetoka kwa Mungu? Au nimekosea njia?Anachotakiwa mtu wa maono anapaswa kufanya ni kumwamini Mungu na kuamini dhamira zake.Wakati fulani mtu mwenye maono anapoona giza,na kuzingatia imani yake kwa Mungu,basi Mungu humpa nguvu katika ono lake.Na nyakati nyingine  Mungu hutujaribu ili kudhihirisha uwazi wako,na utayari wako katika maono.Mtume Paulo alipita katika mambo kama hayo katika Wakorintho wa pili aliposema kuwa na hukumu ya kifo.hapo alikuwa amevujika moyo kiasi cha kutamani kufa,lakini alipata neema na utulivu ndani ya Kristo,na kumwezesha kuendelea.Na hata wengi wetu labda itakulazimu kuruhusa maono ulionayo kufa.Hebu mpe aliyekupa maono kipaumbele,kwa maana yalikuwa yake  kabla ya kuwa ya kwako.Ukifanya hivyo basi atatia nguvu tena katika ono lako na litakuwa

 

Bishop.Rhobinson S.Baiye

rhobinsons.blogspot.com

rhobinsonsaleh1@gmail.com

Whatsapp.0764127531

Mwanza Tanzania.

 

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

UONGOZI BORA WA KIROHO

Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...