Tuesday, June 2, 2020

KANISA LENYE MALENGO

KANISA LENYE MALENGO

Kanisa lenye malengo ni kanisa lililo na umoja ndani yake.Kwa maana umoja ni nguvu na mtengano ni udhahifu.Na maandiko matakatifu yanatuonyesha kwamba,ni vema na tena yanapendeza kukaa pamoja kwa umoja.Zab 133:1-4,Md 4:32-35.Na kanisa likiwa na umoja lazima litashugulika na lengo au malengo yake wala si vinginevyo.Lakini fahamu kwamba umoja unanguvu zake.

Nguvu Ya Umoja.

Umoja una nguvu zake,na nguvu hizo ni za ushindi maana palipo na umoja ushindi haupingiki wala hauzuiliki. kwa nini ushindi wa umoja ni lazima? Mwanzo 11:1-9) Mst 3-4 Mst 6 Mst 7-9,Ukisoma mistari hiyo katika kitabu hicho katika sura hiyo hapo,utaona na kufahamu kwa nini ushindi wa umoja ni lazima.Watu wa Mwanzoni walithamini umoja na ndiyo sababu yao kufaulu katika mipango na mikakati waliyoipanga kwa kufikia malengo waliyojiwekea.Hadi Mungu  alithibitisha kwamba kitu au jambo linalofanyika katika umoja haliweza kuzuilika.Mwanzo 11:6,Bwana akasema,Taza,

Watu hawa ni taifa moja,na kugha yao ni moja;na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya,wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya.

Maana Na Matumizi Ya Nguvu.

Kama mwandamu naamini unahitaji kujuwa na kufahamu maana ya neno nguvu na jinsi inavyofanya,au matumizi ya nguvu.Kwa kawaida sana nguvu ni uwezo wa kufanya jambo,ni madaraka uvumilivu wa kuweza kuendeleza jambo.ngvu ni msukumo mkali unaotokana na nishati.Kwa kuelewa nguvu ni nini hasa,ni vema tujifuze kwa Yesu Kristo kama yasemavyo maandiko yeye, ndiye nguvu za Mungu.Wanafunzi wa Yesu Kristo waliogopa sana.Dhoruba ilipozuka ghafla walipokuwa wakivuka bahari ya Galilaya kwa mashua.Hapana shaka kwamba walizoea kuona dhuruba katika bahari hiyo,kwa sababu bahadhi yao walikuwa wavuvi hodari.Math 4:18-19,Lakini ilikuwa dhoruba kubwa ya upepo wenye nguvu nyingi.Bahari ilichafuka kwa sababu ya dhoruba  hiyo.Wanaume hao walijikakamua sana kuongoza mashua,lakini dhoruba  ilikuwa kali sana.Yesu alikuwa amelala usingizi  katika tezi,akiwa amechoka baada ya kuwafundisha watu siku nzima,Huku wakiogopa kufa.Wanafunzi walimwamsha na kumsihi.Bwana tuokoe,tuna karibia kuangamia.Marko 4:35-38,Math 8:23-25.Yesu hakuogopa.Kwa ujasiri aliukemea upepo.Mara moja upepo na bahari ikatii dhoruba ikakoma,mawimbi yakatulia,kukawa shwali.Kwa hiyo fahamu nguvu za Mungu zimo katika Yesu Kristo.Yohana 1:1-4.

1.Umoja Ushugulisha N a Lengo.

Tumeona jinsi watu wabiblia walivyo thamini umoja.Walithamini umoja kwa sababu waligundua mbambo makubwa ambayo yamo na yatokanayo na umoja.Jambo kubwa la umoja ni nguvu za umoja,na nguvu za umajo kushugulika na lengo au malengo ambayo watu jamii imejiwekea.Kama kanisa la mahali linahiji kuimarika na kusitawi nilazima lishugulike Na lengo au malengo wala si vinginevyo.Kanisa ambalo lisilo kuwa na migogoro ni kanisa ambalo linaloshugulika na lengo malengo yao wala si migogoro.Lengo ni nini,lengo au malengo ni wazo au mawazo makuu ya ubinadamu

F.Schiller alizungumzia juu ya umuhimu wa kuweka malengo makubwa ni rahisi kuingia na kamanda mkuu Alexander wa Macedon alisema juu ya malengo:Kama haiwezekani,nilazima ifanyike.Fahamu lengo,katika maisha ya mtu linaweza kuelezewa na maneno yafuhatayo:Picha halisi au halisiya nini suala la mtu binafsi ni kwa kuifadhiwa katika akili ya matokeo ya mwisho yaliyotarajiwa.Lengo lina muundo wake na huanza na ufahamu wa mtu juu ya kufikiri kupitia njia zinazowezesha utendaji weke.Bila lengo hakuna ukuaji,badala ya kutambua moja ya asili ya mtu.Uwezo wa mtu wakawaida ni kama bahari kubwa,ni kama bara jipya lisilohifadhiwa.Ulimwengu wa uwezekano unaotarijiwa kutolewa na kuelezwa uzuri.Fahamu kufanikiwa ni malengo,na mengine ni maoni.Watu wote na makanisa yote yaliyofanikiwa walikuwa na lengo kubwa.Walijua walichokitaka na walihitaji mkazo mmoja katika kufanikisha hilo,kila siku.Uwezo wako wa kanisa kuweka malengo ni ustadi wa mafanikio.Malengo ya kufungua akili yako chanya na mawazo chanya ya kufikiri malengo.Ukiwa na malengo wewe ni wakuteleza tu,na utapita kwenye mikondo ya maisha.Na ukiwa na malengo wewe ni wakuruka kama mshale moja kwa moja kwa kuwa msababishaji ni wewe.Ukweli ni kwamba unao uwezo mkubwa zaidi na kama kanisa la mahali linaweza kudumu hadi kuja kwa Kristo,Fahamu kwamba chochote ambacho umekamilisha hadi sasa ni sehemu ndogo tu ya kile kinacho wezekana kwaka na kwa kanisa pia.Moja ya sheria za kanisa kufaulu ni hili hapa,Haijalishi limeanza kwa mazingira gani au linaongozwa na nani,limwetokao wapi,ni maamuzim ya mtu peke yake na kanisa lenyewe pasipo kutengemea maamuzi ya mtu au watu aharufu.Fahamu malengo yako nyenu yawe wazi.Malengo yaliyo wazi,yanaongeza ujasiri wako na wakanisa pia.Na unakuza uwezo wako na kuongeza viwango vyako vya motisha.

Malengo  Uhunda Ulimwengu Wako Mwenyewe.

Lengo malengo katika ugunduzi mkubwa zaidi katika historia ya mwanadamu na nguvu ya akili yako kuunda mambo ya maisha yako.Kila mtu anachokiona  katika ulimwengu  huu ni wazo la mtu na liliweka malengo yake hadi hapo yalipofikia.Kwa maana  lilianza wazo,hamu,tumaini na ndoto,iwe katika akili ya mtu mmoja au katika akili ya watu wengi.Wazo mawazo yako ya kanisa ni ubunifu.Mawzo malengo yako aidha ya kanisa  yanaunda ulumwengu wako ulimwengu wa kanisa na kila kitu kinachotokea kwako na kwa kanisa pia.Kauli kuu ya muhtasari wa dini zote,falsafa Metaphysiki,saikolojia hii.Inasema kwamba uko hivyo ulivyo ni kwa sababu ndivyo unavyofikiri wewe kuwa.Maranyi kanisa linaishi katika mazingira na tabia ya kiwango cha fikira za mtumishi kiongozi mkuu.Ulimwengu wako wan je mwishowe unakuwa  onyesho lako la ulimwengu wako wa ndani na vioo hukurudia kwa unavyofikiria.Chochote unacho fikiria juu ya hilo huibuka katika ulimwengu wa ukweli wako.Fahamu kwamba maelfu ya watu waliofanikiwa wameulizwa,mnda wao mwingi wanafikiria ni nini? Jibu la kawaida linalotolewa na watu waliofanikiwa ni kwamba wanafikiria juu ya kile wanachotaka,na jinsi ya kukifanikisha.

Faida Ya Kanisa Kuwa Na Malengo

Kunafaida katika kanisa kuwa na malengo na hata mtu binafsi kuwa na malengo kuna  hizi ambazo nitazihainisha hapa na faida za jumla.yaana ni faida atakazozipata mtu dinafsi na kanisa lenyekwa na malengo.Kwa kuwa kanisa yenye umoja ujishugulisha na lengo au malengo waliojiwekea wala si vinginevyo.Sasa kabla hujakamilisha chochote maishani,na lazima ufahamu unahitaji nini.Ni lazima ukae chini utafakari kama kile unachokifanya kama kina samani kwako;ikiwa hakina thamani kwako,basi tenga muda ujiwekee malengo yenye maana kwako.Kwa maana maisha ya kanisa au mtu bila malengo ni sawa na kuanza safari bili kufahamu unakotaka kwaenda au kufika.Kanisa kujiwekea malengo kuna umuhimu mkubwa sana kwa  maana hufanya kanisa kujikita kwenye malengo kuliko kujikita kwenye migogoro isiyonatija.Mtu Kanisa lifahamu kwamba kujiwekea malengo ni hatua ya kwanza ya kufanya visivyoonekana vionekane dhahiri.

1: Faida Ya Kwanza Yakuwa Na Lengo.

Mwanzo kabisa lengo au malengo yanakupa mwongozo  yaani mwelekeo maishani.Malengo hulisababisha kanisa kubaini kitu kinacholengwa,na kulifanya kanisa kuelekeza nguvu zake kwenye kitu husika.Badala ya kushika hiki na kile au kuwa huyu na Yule malengo au lengo litaliwezesha kanisa kufahamu kipi kifanyeke na nani afanye na kwa mnda wa kufanya.Ifahamike kwamba kanisa kuwa na mwongozo nijambo muhimu sana kuliko kuishi maisha ya kudandia mambo ni vizuri kanisa kama kanisa kuwa na mwelekeo.Na mwelekeo huletwa na Malengo ya kanisa.Na kanisa ambalo halina malengo ni kanisa ambale linafananishwa na chombo ambacho kina endeshwa na mawimbi ya bahari likipelekwa huku na kuele likidandia mambo kwa kukosa mwongozo.Yakobo 1:5-8

 

2: Faida Ya Pili Yakuwa Na Lengo.

Lengo Huleta Uwezo Na Ngvu Za Maamuzi.

Baada ya kanisa kupata mwongozo utokanao na malengo sasa basi litaweza kubaini ni maamuzi gani yanafaa na ni yapi ambayo hayafai kulingana na malengo  ambayo yapo.Pia kanisa litaweza kufahamu mambo ya msingi katimaisha ya kanisa hilo.Kanisa lenye malengo huwa makini sana kwenye maamuzi yake kwa kuwa linalinda,lisije likafanya maamuzi yatakayoathiri lengo au malengo huka.Kwa hiyo kanisa lenye kudumu katika umoja lina kuwa makini sana kulinda umoja huo katika maamuzi kulingana na maelengo yatokanayo na umoja wao.Maamuzi sahihi na kwa wakati sahihi,na kwa watu sahihi. Kum 16:18-19,17:7-9,25:1.

3:Faida Ya Tatu Yakuwa Na Lengo.

Lengo huwezesha Kutawa Baadaye.

Kanisa limapokuwa na malengo na mipango sastahiki na kuyatimiza ni wazi moja kwa moja limekwisha tawala baadaye pasipo watu kufahamu kwamba tayari kanisa limekwisha tawala.Kuweka malengo ni jambo zuri ambalo litaliwezesha kanisa kutahamu aina ya mfumo wa maisha yake ya baadaye.Lambo la muhimu ni kuhakkikisha kuwa unaweka mpango sahihi na wakati sahihi na kwa watu sahihi.Kwa sababu unaweza kwafanya vitu sahihi na kwa mnda sahihi lakini usiyafanye kwa watu sahihi utakuwa umepoteza mnda.Ni muhimu kanisa kuhakikisha kila siku kuna kitu kinachofanyika ili kukamilisha sehemu fulani ya malengo iliyojiwekea maishani.Fahaumu kwamba malengo na ramani katika mzunguko wa kanisa hata maisha ya mtu.Bila shaka lengo malengo hutawala katika mnda uliyopo na mnda wa baadaye bila watu kujua na kufahamu.Mwanzo 1:26,Mathayo 20:25,Marko 10:42

 

 

Lengo Huwezesha Kujikita Kwenye Mambo Muhimu.

Yapo mambo mengi katika maisha ya kanisa la mahali ya kila siku.Lakini yawezekana siyo yete ya muhimukatka kutimiza malengo ya kanisa.Kanisa likiwa na malengo ni rshisi kubaini mipango au mambo ya msingi na ya muhimu kwa kutazama yale yote yanayokinzana na malengo.Haijalishi Kanisa linalikodolea macho jamnba fulani,kwa kiasi gani,kama linakinzana na yake halina budi kuliacha au kuachana nalo.Ni kweli yapo mambo mengi ambayo kanisa kama kanisa linayag`ag`ania lakini hayana umuhimu kabisa katika afya ya kanisa.Hata wapo watumishi,viongozi,na watenda kazi wengine katika kanisa ambao si wamuhimu lakini wanag`ag`ganiwa kuwepo katika huduma au nafasi walizonazo ao walipo.Watu kama hao wasio wa umuhimu wana lichelewesha kanisa kufika pale ambapo wanahitaji kufika,kulingana na malengo yaliyopo.Kumbukumb la Torati 10:11

5: Faida Ya Tano Yakuwa Na Lngo.

Kanisa linapokuwa na malengo thabiti  washirika pamoja na watumishi na viongozi huwa na matumaini na huhamasika pakubwa.Na hamasa huzidi pale ambapo tunaanza kuona pale tunapokamilisha malengo yetu ya mnd mfupi,ili kutuhamasisha kufanya bidii zaidi kuyafikia yale ya mnda mrefu.Ni kweli na wazi kwamba chanzo kizuri cha hamasa ni kujiwekea  malengo na kuanza kuyatimiza.Kumbuka kwamba utekelezaji wa malengo ni njia mojawapo muhimu ya kuhamasisha na kushawishi washirika kuamini na kudumu kwa kile kilicho pangwa.Na zaidi sana hata wale ambao wako nje na kanisa,watakapoona maendeleo watafahaumu na kusema hayo ndiyo malengo,na hivyo ni vyepesi sisi kuwafikia na kuvuta kutukaribia.Mathayo 27:20,Luka 24:29,Md 6:11,

6: Faida Ya Sita Yakuwa Na Lengo.

Fahamu kwamba mtu au kanisa lenye malengo Hulinda muda haliwezi kamwe  kupoteza muda.Kanisa likiwa na malengo ni wazi kwamba mnda wake wote utakuwa umegawanywa kwenye kuyafanyia kanzi na kuyatimiza malengo wala sivinginevyo.Kwa njia ya kujiwekea malengo kanisa halitoweza kwa kufanya mambo ambayo hayaliwezeshi kanisa kifikia ndoto malengo yake.Haitarajiwi kanisa lenye malengo kulewa na au kuleweshwa na na matokea ya mipango ya malemalengo.Haitarajiwa kanisa kutokuwajibika kwa kuwa lina malengo.samahani mengi ambayo ungetarajia kuyavuna katika sura hii na kipengele hiki,yanazungumzwa kwa kina katika sura ya 8,isemayo kanisa na nyakati.Mathatayo 2:7,16,9:15,20.

7:Faida Ya Saba Yakuwa Na Lengo.

Kanisa lenye malengo hufanya uwekezaji.Uwekezaji ni hali au tendo na njia ya fedha au mali zako kuzaa zaidi.Kanisa likiwa na malengo  yaliyo wazi,litafahamu nini,wapi,na lini liwekeze.Kwa kuwa malengo  yataliwezesha kanisa kubaini ni uwekezaji gani unaoendana na malengo ya kanisa.Lakini kama kanisa halina malengo kama tulivyoona tangu mwanzoni mwa mada hii,laweza kuwekeza kwa kila kitu ambacho kinacho jitokeza mbele yake,na matokeo  yake huwa na kinyume na matarajoyo.Kwa hiyo wewe mcha Mungu katika Kristo  fahamu kila unachokifanya katika kanisa una wekeza na siku mja vita rudi kwako ma kukusaidia na hapo utakuwa umepata faida kwa kile ulicho wekeza madhabahuni.Wekeza katika Ibada ya Utoaji,Wekeza katika Ibada ya Maombi,Wekeza katika Muda,Wekeza katika kusifu na kuabudu Mungu,na hayo yote utapata faida nzuri ya uwekezaji wako.Mathayo 2:11,19-21,Fahamu kwamba wakati utakapopata au kupokea msaada kutoka kanisa lako,hapo fahamu umepata faida ya uwekezaji wako katika kanisa.akumbuka kwamba Mungu hutubariki kulingana na uwekezaji wetu kwake.Kanisa linapotoa misaada kwa mayatima,walemavu, wajane na wagane,wafungwa,nk,ha

Po kanisa litakuwa limewekeza kwa Mungu,na litapata faida katika uwekezaji huu.

8:Faida Ya Nane Yakuwa Na Lengo,

.Kainsa au mtu binafsi aliye na malengo hujitathmini.Kanisa linapimaje kufanikiwa au mafanikio yake kama  halina kipimo cha kupimia kufanikiwa huko,malengo ni kipimo muhimu kitakachowezesha kanisa kutathimini kama limefanikiwa au la.Kanisa likiwa na malengo ni rahisi kutazama kama yale yaliyofanywa au yanayofanywa yameliwezesha kufikia lengo au malengo yake.Kama yameliwezesha basi ni vizura na yanatia moyo sana.Lakini ikiwa hayajaliwezesha kufikia lengo malengo,kuna mambo ya kutazama upya.

Umuhimu Wa Kanisa Kutathimini Mambo Yake.

Katika mfumo wa kanisa na maendeleo yake,tathmini au kutathmini ni utaratibu maalumu wa kupima mafanikio ya matokeo na malengo yaliyokusudiwa,unafanywa kulingana na utaratibu wa kanisa husika mara ngapi kwa mwaka au kwa miaka mingapi.kanisa litatathmini likijitahidi  kuchambua hatua zilizofikiwa kufanikisha lengo kuu la mfumo wa kanisa ambao ni mfumo wa ukaguzi unaofanya kazi kwa ufanisa ili kutoa huduma bora kwa washirika.Kwa kufikia malengo au lengo hili maeneo ya matokeo yafuatayo yaliwekwa ili yafanyiwe ufatiliaji na tathmini.

Miradi  Inayofadhiliwa  Inafanya Kazi Kwa Ufanisi?

Tathimini inataka kuona namna ambayo maeneo ya kutolea huduma yanayofadhiliwa katika kanisa yanakamilika na yanafanya kazi ya kutoa huduma zinazo hitajika.Kwa kufahamu kama miaradi hiyo inafanya kazi kwa ufanisi nimuhimu kanisa kujifanyi tathmini kupitia kamati ya ukaguzi wa fedha na mali za kanisa,na ifanywe kwa upole na hofu ya Mungu.2Nyakati 32:28,Wagalatia 6:1,Efe 4:2,Mathayo 9:8,2Kor 7:11.

Vipaumbele Vya Kanisa Vinazingatiwa?

Tathmini itapima kiwango ambacho vipaumbele vya kazi au miradi ya kanisa ilivyozingatiwa,kutekelezwa na inavyotoa huduma zilizokusudiwa.Kanisa lenyekudumu katika umoja lazima liwe na nguvu.Na vema kutimiza maono mikakati na kuyatathmini kama mambo yako sawa.Luka 15:17

Jidihada  Za Washirika Zinatambulika Na Kuwezesh

            Wa Na Kupewa Usaidizi?

Tathmini itapima namna ambavyo jitihada za washirika zinavyotambuliwa na kuungwa mkono kifedha kitaaluma.

Kanisa ambalo linadumu katika nguvu za umoja nilazima litathamini jitihada za washirika.

Fedha Zinazotolewa Kwa Usawa ndani Ya Kanisa?

Tathmini itapima namna ambavyo miradi inavyotekelezwa imeleta mabadiliko chanya katika kanisa zetu zenye hali duni kutokana na kigezo cha mgao wa fedha kwa usawa .Msisitizo unatolewa kwenye kupunguza utofauti wa upatikanaji wa huduma kati ya makanisa ambayo yana hali bora nay ale yenye hali duni.1Sam 15:22,Zaburi 62:12,

Usimamiza Wa Fedha Za Kanisa Unaboreshwe.

Tathmini itapima  namna idara za makanisa zinavyozingatia taratibu za usimamizi wa fedha kama vile maandalizi sahihi ya malipo,maandalizi na mawasilisho ya taarifa za fedha,kujibu hoja za ukaguzi kwa wakati.mpngo mzuri wa vyanzo vya watumishi wa idara ya fedha na vitengo au matawi yake na mikakati ya kuboresha ukusanyaji wa vyanzo vya ya ndani ya kanisa.Zaburi 109:8,Hesabu 3:36,1Nya 9:23,24:3,19,26:

1,2:9:4,23 2,Md 1:20./

Je,Maeneo Yenye Mazingira Mangumu Yanafaidika?

Malengo ni kutengeneza utaratibu wa kutekeleza miradi yenye ubora kwenye makanisa yenye mazingira magumu katika maeneo yao,licha ya changamoto zilizopo.Tathmi

Mini itapima kuona kama zinaandaa ya kuwavutia waamini wapya.Tufahamu kwamba mazingira ya kanisa yanahubiri  kwamba Mungu yupo na nimtendaji mzuri sana,katika watu wake.Ezra 3:6-7,14,4:1,5:15,6:5,12,8:23;

Washika Wanaendelezwa Na Kusimamiwa Ipasavyo?

Tathmini itapima kuona kama washirika wanaendelezwa kimafunzo yenye ufanisi katika ngazi ya juu na ya msingi za katika ngazi zote kutokana na utaratibu wa kanisa husika,pamoja na matokeo ya mafunzo hayo katika usimamizi wa miradi ya kanisa.Tathmini itapima pia mbinu za bora na jitihada za kanisa kuwawezesha watumishi kuendele kubaki hazinzina ya hekima katika kanisa.Mathayo 28:16-20,11:1,Marko 4:1,6:2,Luka 3:23,20:21,Md 1:1,4:18,Zaburi 32:8,45:4,Mithali 4:11.

Je,Kanisa Na Miradi Inasimamiwa  Kwa Uwazi..?

Uwazi na uwajibikaji ni jambo jingine muhimu kwenye tathmini katika mfumu wa kanisa.Ni muhimiu kuthmini ili kuona kama mfumo huu umesimamiwa kwa uwazi na kuwajibika kwa washirika na watumishi na viongozi katika kanisa.Pia tathmini itaainisha kuona namna kanisa lilivyochangia kukuza umoja na utawala bora.

Je Fedha Za Kanisa Zinagawika Kwa Usawa?

Tathmini itapima matokeo ya kanuni ya ugawaji wa rasilimali iwapo imezingatia usawa na haki katika upatikanaji wa huduma za kanisa.Ukisoma kwa makini katika kitabu cha matendo ya mitume,inasema kwamba wakati kanisa lilipoongezeka palikuwa na manunguniko,Md 6:1-7,Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao,palikuwa na manung`uniko ya Wayaudi wa Kiyunani juu Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku.Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi,wakasema,Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani.Basi ndugu chegueni watu saba miongoni  mwenu walioshuhudiwa kuwa wema,wenye kujawa na Roho na Hekima,ili tuwaweke juu ya jambo hii;na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.Neno hii likapendeza machoni pa mkutano wote;wakachagua,Stefano,mtu aliejaa imani na Roho mtakatifu,na Filipo,na Prokoro,na Nikanori,na Timoni,na Parmena,naNikolao mwongovu wa Antiokia.

Ambao wakawaweka mbele ya mitume,na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao.Neno la Mungu likaenea;na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu;jamii kubwa ya makuhani wakatii ile imani.

Bajeti Ya Kanisa Kwa Jumla.

Ifahamike kwamba fedha za kanisa haziwezi kutosha kukizi vipaumbele vyote vya kanisa kwa wakati mmoja.Hata hivyo ni muhimu kuboresha hali iliopo kwa 1% ya jumla ya vipaumbele vyote vya kanisa vinatekelezwa kwa mwaka. Inafaa tathmini angalau mradi mmoja kwa kila kanisa la kijii wakati wa zoezi la tathmini.Hivyo tathmini itapima namna ambavyo fedha  za kanisa zinavyoongezeka kufikia lengo.Tunapotathmini mipamgo ya maendeleo ya kijamii ni vema pia kujitathmini katika mambo ya roho.

 

Kimeandaliwa na kuandikwa na

Bishop.Rhobinson S.Baiye.

rhobinsons.blogspot.com

rhobinsonssaleh1@gmail.com

Whatsapp.0764127531

Mwanza Tanzania.

 

 

 

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

UONGOZI BORA WA KIROHO

Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...