Sunday, June 21, 2020

DUMISHA UMOJA WAKO KATIKA KUSAMEHE NA KUTUBU TOLEO N0 1.

DUMISHA UMOJA WAKO KATIKA KUTUBU

NA KUSAMEHE. Math 6:14-15


Tabia Ya Kutubu Na Kusamehe.

Kukiri kosa na kuomba msamaha kunawashinda wengi.au kusamehe baada ya kuombwa msamaha ni kazi ngumu kwa wengi.Tabia ya kutubu na kusamehe hujenga mahusiano kwa upya.Ukijizoeza kutubu na kusamehe kutakufanya urekebishe makosa uliyoyafanya.Kutubu na kusamehe kunahitaji unyenyekevu wa hali ya juu sana.Lakini katika kitabu hiki tutajikita hasa katika kusamehe na kusamehewa au kuombwa samahani na kuomba samahani.

Dumisha Umoja Wako Na Mungu Katika Kutubu

                           Na Kusamehe.

Kutubu hurejesha uhusiano wako na Mungu  kwa upya.kuwasamehe wengine na kuomba msamaha  huimarisha umoja wako na Mungu na kuondoa kila kunyanzi moyoni.Mungu yuko tayari na anasubiri kumsamehe mtu anaye omba msamaha. Imeandikwa katika Zab 86:5Kama wewe Bwana u mwema,umekuwa tayari kusamehe,na mwingi wa fadhili kwa watu wote wakuitao.

Daudi Aliweka Wapi Tumaini Lake La Kusamehewa?

Daudi alihitaji kuweka sawa umoja ukaribu wake na Mungu ilibidi Daudi aweke tumaini lake la kusamehewa kwa Mungu.Imeandikwa katika Zab 51:1,Ee Mungu unirehemu sawasawa na rehema zako kiasi cha wingi wa rehema zako uyafute makosa yangu.Fanya hivyo kati yako na Mungu na watu pia.

Rehema Ya Mungu I Kiasi Gani?

Kwa kufahamu kuasi cha rehema ya Mungu,imeandikwa katika Zab 103:11-12,Maana mbingu zilivyo inuka juu ya nchi kadiri ili ile rehema  zake ni kuu kwa wamchao kama mashariki ilivyo mbali na magaribi,ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.

Kuna Ahadi Kwa Wanao Omba Kusamehewa

Kumbuka kwamba kuna ahadi kwa ye yote anayeomba kusamehewa na Mungu.Imeandikwa katika 1Yoh 1:9Tukiziungama dhambi zetu,yeye nimwaminifu na wahaki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimuwote.

Mungu Atakusamehe Kama Unawasamehe Wengine.

Biblia inadhibitisha kuwa Mungu atakusamehe ikiwa wewe unawasamehe watu wengingine.Imeandikwa katika Math 6:14-15,Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi bali msipowasamehe  watu makosa yao wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.

Wale Waliyosamehewa Husamehe.

Nakuomba msomaji wa kitabu hiki ufahamu kwamba wale wanaosamehewa husamehe wengine.Pia imeandikwa katika Efe 4:31,Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi kasamehane kama Mungu katika Kristo aliwasamehe ninyi,.

Kusamehe kwa kweli hakuhesabu makosa

Fahamu ndugu yangu kusamehe kwa kweli hakuhesabu wingi wa makosa.Imeandikwa katika  Math 18:21-22.Kisha Petro akamwendea akamwambia Bwana ndugu yangu anikose mara ngapi name ni msamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia sikwambii mara saba bali hata saba mara sabini.Yesu alimaanisha kusamehe hakuna ukomo au kikomo.Wewe inakubidi kusamehe ili kutimiza sababu za kusamehe tutakazoziona hapo chini.Endelea kusoma  sababu za kusamehe.

Je Tunapo Samehewa Ni lazima Tuwe Na Hofu?

Hakuna haja ya kuwa na hofu wakati tunapo samehewa.Imeandikwa katika . Nilikujulisha dhambi yangu wala sikukuficha upotovu wangu Nalisema nitakiri maasi yangu kwa Bwana nawe utanisamehe upotovu wa dhambi yangu.Katika kusamehe Yesu ametukomboa  katika sheria ya dhambi na mauti kama mshahara  wa dhambi.Rum 8:1-11.Wakolasai 2:13-14

Tunapo Hitaji Msamaha Tunahitaji Nini?

Fahamu kwamba wakati unapo hitaji kusamehewa na Mungu unahitaji kuoshwa kutakaswa kuwa mweupe pe.Imeandika katika Zab 51:2-4,Unioshe kabisa na uovu wangu maana nimejaa makosa yangu na dhambi yangu I mbele yangu daima Nimekutenda dhambi wewe peke yako na kufanya maovu mbele za macho yako wewe ujulikanaye kuwa unahaki unenapo,na kuwa safi utoapo hukumu.

Omba Msamaha

Jambo hili ni muhimu sana.Omba msamaha usisubiri kuombwa msamaha.Imeandikwa katika Zab 51:7-12,Unisamehe kwa hisopo nami nitakuwa safi,unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko dheluji,unifanye kusikia furaha na shangwe,mifupa ilio ponda ifurahi. Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu uzuj ifute hatia zangu zote Ee Mungu uniumbie moyo safi uifanye upya roho ilio tulia ndani yangu usinitenge na uso wako wala roho wako mtakatifu usiniondolee unirudishie furaha yawokovu wako unatengeneze kwa roho ya wepesi.

 Amini Mungu Amekusamehe

Kuwa na imani kwamba Mungu amekusamehe.Imeandikwa katika Zab 32:1-6,Heri aliyesamehewa dhambi na kusitiriwa makosa yake heri Bwana asiyemhesabia upotovu,ambaye rohoni mwake hamna hila.niliponyamaza mifupa yangu ilichakaa kwa kuugua kwangu mchana kutwa na kwa maana mchana na usiku mkono wako ulinilemea jasho langu linakauka hatanikawa kama nchi kavu wakati wa kaskazi nalikujulisha dhambi yangu wala sikuuficha upotovu wangunalisema nitayakiri naasi yangu kwa Bwana naweukanisamehe upotovu wa dhambi yangu kwa hiyo kila mtu mtauwa akuombe wakati unapopatikana hakika maji makuu yafurikapo hayatamfikia yeye.

Usiombe msamaha kwa sababu wengine wanaomba msamaha,bali omba usamehewe na Mungu kwa kujutia dhambi na makosa yoko.

Dumisha Umoja Wako Na Mke,Mme Katika

                 Kutubu Na Kusamehe.

Kosa linapotendeka,msamaha huhitajika kutoka pande zote mbili.kutokukiri makosa sio njia ya kutukuwa mkosaji, na tabia hiyo huharibu uhusiano kati ya mke na mume.Hata kama huoni kosa,fahamu mwezako analiona.Ni vyema kuomba msamaha ili kurejesha uhusiano mzuri uliokuwepo.Unaweza kugundua baadaye kuwa ulikuwa ukikosea.Makosa yasiwe sababu ya kufarakana na kuharibu uhusiano wenu.

Maana  Ya Msamaha Au Kusamehe

Katika Biblia neno la kigriki linalotafsriwa kusamehe linamaanisha kihalisi kuhachilia.Ni kama wakati ambapo mtu anaamua kutodai malipo ya teni.Yesu alitumia ulinganisho huu alipowafundisha wanafunzi wake ambao aliwaita mitume  wake alipowaambia salini hivi.Utusamehe makosa na dhambi zetu kama vile tunavyo wasamehe wanao tukosea.Luka 11:4.

Vivyo hivyo alipotoa mfano kuhusu yule mtumwa asiye na rehema Yesu alilinganisha msamaha na mfano wa kufuta deni.Math 18:23-35.Tunawasamehe wengine  tunapoepuka kinyongo na kutodai malipo kwa sababuu ya uchungu au hasara tuliyopata.Biblia maandiko matakatifu yanatufundisha kwamba upendo usio na ubinafsi ndio msingi wa msamaha wa kweli kwa kuwa upendo,hauhesabu mabaya.1Kor 13:1-8

Kusamehe Hakumaanishi Yafuatayo

Kupuuza Kosa:Andiko la Isaya 5:20.linawashutumu wale wanaosema kuwa matendo mabaya au yasiyofaa hayana madhara au yanakubalika.Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema,na kwamba wema ni uovu.watiao giza badala ya nuru,na nuru badala ya giza.Watiao uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu!Katika undugu na urafiki na utu na ndoa nivema kutopuuza mambo yanayofaa kati yenu.Kwa sababu kusamehe na kusamehewa sio kupuuza mambo bali ni kufuta mambo.Usiweke kweli badala ya uongo na usiweke uongo badala ya kweli.Kut 23:1,Usifumishe habari za uongo,usitie mkono wako pamoja na waovu,kuwa shahidi wa uongo.

 Kuishi Kana Kwamba Kosa Halijatendwa.

Kuishi au kujifanya kana kwamba haujatenda kosa au haujatendewa kosa si kwamba ina maana  kwamba dhambi imesamehea la hasha.Mungu alimsamehe Daudi Mfalme wa Israeli dhambi zito aliyoitenda,lakini Mungu hakumlinda Daudi kutokana na madhara ya matendo yake.Mungu alimwongoza Daudi aandike kuhusu dhambi zake na hadi leo zinakumbukwa kwa kusomwa kwa kile Daudi alicho kiandika.2 Sam 12:9-13.

Kuruhusu Wengine Wakutumie Vibaya

Kwa mfano,tuseme kwamba umemkopesha mtu pesa,naye anazitumia vibaya halafu anashindwa kukulipa kama alivyoahidi.Sasa anasikitika sana na kuomba msamaha.Je,unaweza kumsamehe kwa kuweka kinyongo moyoni,na kutomkunbusha-kumbusha jambo hilo? Na labda hata kufuta deni hilo.Na hata hivyo unaweza kuamua kutokumkopesha pesa tena.Zab 37:21,Mith 14:15,22:3,Gal 6:7

Kusamehe Bila Misingi Halali.

Mungu hawasamehi watu wanaotenda dhambi kimakusu

Di na kwa ukatili hukataa kukubali makosa yao na kubadilika na kuomba msamaha wale ambao wameumizwa.Mith 28:13 Md 26:20,Ebr 10:26.Watu hao wasiotubu yaani watu wasio mgeukia Mungu huwa ni maadui wa Mungu naye Mungu hatazamii kuwasamehe watu ambao yeye hawasamehi.Zab 139:21-22,

Kusamehe Makosa Ya Kudhaniwa

Nyakati nyingine,huenda tukahitaji kukubali kuwa hatukuwa na sababu ya kukasirika. Biblia inasema tusiwe na hasira kwa maana hasiri hukaa katika kifua cha wapumbavu.Mith 7:9.Unapodhani kwamba umekosewa na mtu halafu ukamsamehe bila kuwa na hakika kwamba umekosewa na ukasamehe,unafananishwa na kicha mwendawazimu,ambaye husema mambo mengi lakini kesho ukimuuliza anakuambia yaliyotofauti na yajana.

 SABABU ZA WEWE KUSAMEHE ALIYEKU

                               KOSEA

Sababu ni kitu ambacho kinachofanya kitu kingine kitokee.kisa chanzo.Sababu ni maelezo yanayoonyesha kwa nini hoja zilizotolewa hazikubaliki au kwa nini zinakubalika.Sababu ni lengo au malengo au madhumuni yanayompeleka mtu kufanya jambu fulani.Usifanye jambo lolote pasipokuwa na sababu.Ata kicha anafanya mambo kinyume na kawaida sababu na akili zake zimechanganikiwa hazina kumbukumbu na hazina aibu.Hapa chini nimekuorodheshea baazi za sababu za wewe kumsamehe aliyekukosea.

Kukuweka Huru

Kutokusamehe kunakufanya uwekama mtumwa na kujisikia vibaya kabisa kukosa amani na zaidi ni pale utakapokutana au kumwona yule aliyekukosea anafuraha na anaendelea na maisha yake bila tatizo lolote.Fahamu mtenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.Yesu akawajibu,amin amin,nawaambia,kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.Math 8:34.Isaya 61:1.Roho ya Bwana Mungu ijuu yangu;kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekeve habari njema;amenitu

Ma ili kuwaganga waliovujika moyokuwatangazia mateka uhuru wao,na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.Yohana 8:38.

Kukupanguvu Za Kuendelea Mbele Zaidi

Kuna mambo mengi mazuri na muhimu zaidi katika maisha kuliko chuki na hasara.Kwa nini ufikirie tu kuhusu mtu aliyekuumiza au kukukwaza? Usipo msamehe utabaki kuumia tu na kushindwa kufanya mambo muhimu ya kusonga mbele na kupata mafanikio yatakayomshawishi na kuona umuhimu wako wa kuzaliwa na Mungu kuruhusu wewe kuishi duniani.Math 5:16,Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema,wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni Sheria na manabii.

Kulinda Afya Yako

Uchungu na maumivu uliyoyapata baada ya kukosewa ni dhahiri kuwa yanaweza kusababisha matatizo ya afya kama vile msongo wa mawazo,kukonda,ugojwa wa moyo.Kumbuka msango wa mawazo ni chanzo cha maradhi mbalimbali kama vile shinigizo la damu,kiharusi,nak.Sasa kwa nini yakuandame kwa sababu ya kutosamehe! Ni muhimu na busara kusamehe aliye kukosea ili afya yako iwe vizuri.Math 9:12,Marko 2:17,16:18,2Fal 4:35.

Huondoa Hasira Na Chuki

Ni kweli chuki na hasira huingia nafsini na moyoni mwako mara tu unapokosewa.Ukiwa na chuki na hasira kali nafsini na moyoni mwako,na ni dhahiri utapunguza tija katika yale unayofanya katika mzuguko wako wa maisha.Unaposamehe unajiweka katika hali nzuri zaidi kiutendaji.Fahamu kwamba hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu.Na chuki husababisha mauaji.Efe 4:26,Iweni na hasira ila msitende dhambi;jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka.Efe 4:31,Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu,pamoja na kila namna ya ubaya.

 

Huondoa Utawala Wa Mtu Mwingine katika Akili

                                     Yako

Ni dhahiri kwamba unamkumbuka mtu aliyekukosea kila wakati akilini mwako.Ni wazi kwamba ukisikia jina lake likitajwa au hata sauti yake tu unapata maumivu kutokana na lile alilokufanyia.Fahamu huo ni utawala wa mtu mwingine ambao umetawala akili na fikra zako.Ni vema msamehe leo ili uendelee na maisha yako yeye uhuru.1Kor 15:24,Soma Wakolosai 2:23,Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima,katika namna ya ibada mliyoitunga wenyewe,na katika kunyenyekea,na katika kuutawala mwili kwa ukali;lakini hayafai kitu kwa kuzuia tama za mwili.

Hukuletea Utulivu Wa Akili.

Ni dhahiri shahiri kwamba watu wengi wakikosewa wanashindwa kupata utulivu wa akili.Jambo hili limefanya wengi hata kushindwa kutimiza  majukumu yao ya kila siku.Mara kichwa kinauma,mara sijisikii vizuri,mara sina nguvu mara sina mood.Hayo yote hudhihirisha ukosefu wa utulivu wa akili.Math 7:24,Bali kila asikiaye hayo maneno yangu,na kuyafanya,atafananishwa na mtu mwenye akili,aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.

Ni Aina Bora Ya Kisasi

Je unafikiri kamba kulipa kisasi ni kufanya baya au mabaya kama uliyofanyiwa? Kama jibu ni ndiyo,unakosea kwa kiasi kikubwa sana.Fahamu ni pale mtu anapokukosea lakini wewe unamfanyia jambo jema.Hapo umemmwagia makaa ya moto kichwani mwake.Math 5:37,Bali maneno yenu yawe Ndiyo,ndiyo,Siyo,siyo;kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu kuhusu kujilipiza kisasi.Linganisha na Md 7:24.

Huonyesha Upendo Mkuu

Kuna wakati mtu aliyekukosea anaumia kutokana na kosa alilofanya lakini anashindwa kuja kuomba msamaha.Kumbuka kumsamehe kuna dhihirisha  upendo wa hali ya juu hata kama hajaja kukuomba msamaha.1Kor 13:1-8.Kumbuka kwamba tumesoma kwa undani sana kuhusu neno upendo katika sur ya kwanza.Tume ona upendo wa ki-Mungu,upendo wa kirafiki,upendo wa kindugu,upendo wa kimapenzi mahaba ndoa,upendo wa kujipeda mwenyewe.

Kiashiria Cha Ukomavu Wa Imani

Ni kweli hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kusamehe kama hana au sio mkomavu wa imani kiakili na kihekima na busara za kutosha.Fahamu watu wachanga hupenda kubeba na kutunza chuki na hasira,wao ni heri kubaki na maumivu katika maisha yao yote kuliko kuyaachilia ili wawe huru.Math 17:20,

Dumisha Umoja Wako Na Jamii Katika Kutubu Na  

                  Kusamehe.

Tabia ya kusamehe  na kuomba msamaha kwa watu wote ni ya misingi katika kujenga mahusiano mazuri na watu.Kutubu na kusamehe kunasaidia kuliweka wazi kosa na kuanzisha jitihada za kutorudia makosa, badala ya kujenga ukuta wa kujilinda kwamba hujakosea ni bahati mbaya.Jamii ya watu hupenda na kuthamini mtu mwenye roho na moyo wa kuomba msamaha wakati anapokosea jamii.Baadhi ya watu katika jamii hujilkita kuchenga ukuta wa kujilinda  ili kupata nafasi ya kuwadhihirishia jamii kwamba hawajakosea na hata kama wamekosea ni bahadi mbaya kwa kutokea hayo yaliyo tokea.Lakini ni vema wewe mtumishi kiongozi ama mkristo ni vema kuomba msamaha unapokosea.

Hitimisho

Ni dhahiri kusamehe ni jambo gumu lakinki ni muhimu hasa kwako wewe uliyekosewa.Ikiwa ni mzazi,mpenzi,ra

Fiki,ndugu,jirani,mfanyakazi wako,mtumishi wako,mwa

Jiri wako,mme ama mke wako amekukosea ni vema kumsamehe kutakufungulia ukurasa mwingine mpya.Kwa njia hii utafanya maisha yako kuwa yenye tija amani na furaha zaidi. 1Timotheo 2:1-7,Wafilipi 4:4-7

Tutaendelea kutoa mengi katika neno hii Msamaha.

Kimeandikwa na

Bishop.Rhobinson S.baiye

Rhobinsons.blogspot.com

Rhobinsonsaleh1@gmail.com

Whatsapp. 0764127531

Mwanza Tanzania.Mkolani.

 

 

 

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

UONGOZI BORA WA KIROHO

Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...