JIPENDE
MWENYEWE KWANZA
![]() |
|
Naomba
ufahamu kwamba kitabu hiki kimehusika na aina Ya upendo wa kujipenda mwenyewe.
Kwa maana kuna aina Tano za upendo haijalishi wengi hufundisha na kuaminisha
watu kwamba kuna aina nne za upendo,huku wakiacha upendo wa kujipenda wewe
mwenyewe.Maandoko matakatifu yanasema mpende jirani yako kama nafsi yako.Ikimaanisha
kwamba mtu hujipenda au mtu upenda nafsi yake.Mathayo 22:39.
Tano
Za Upendo Aina
- Upendo wa ki-Mungu /Agape.God love
- Upendo wa kirafiki / Phileo. Friend love
- Upendo wa kindugu / Storge. Familiy love
- Upendo wa kimapenzi mahaba. Romantic love.
- Upendo wa kujipenda mwenyewa.Personal love.
upendo wakujipenda mwenyewe.
Aina
hii ya upendo wa kujipenda mwenyewe ni Upendo ambao binadamu anakua nao kwa
kujijali na kujipa thamani yeye
mwenyewe, pamoja na mapungufu yote yale aliyonayo.Huwezi kukuta hata siku moja
mtu anajijukia mwenyewe.Aina hii ya Upendo huzaa kitu kinachoitwa
ubinafsi.Pamoja na Biblia kusema Mpende jirani yako kama nafsi yako.Biblia
inaturuhu tupende nafsi zetu.Na ndio sababu mtu akijitoa uhai kwa kujinyonga au
kujimaliza kwa chuma cha mcha kali au kwa sumu na kwa njia ye yote ile ni
mtenda Dhambi.
Umuhimu Wa Kujipenda Mwanyewe.
Unapofanikiwa
kujipenda mwenyewe unakuwa umejipa nafasi kubwa sana ya kutambua thamani yako
na uwezo wako ambao umebarikiwa na Mungu kuwa nao.Na kwa maana hiyo basi hata
unaweza kufanya mambo yako kwa kujiamini kabisa,bila ya kutetereshwa na mtu
yeyote yule.Lakini pia utakuwa na uwezo wa kukaa peke yako na hakuna kitu
ambacho kitakacho kosekana. Hayo yote ni
kwa sababu tayari umeshajipenda mwenyewe unajithamini na kujijali pia.Watu
wengi huwa wanashindwa kujipenda wao wenyewe na wakati huo huo wanasema kwamba Kuna
watu ambao wanaowapenda.Ukweli ni kwamba huwezi kumpenda Mtu mwingine ikiwa
wewe mwenyewe umeshindwa kujipenda vile ambavyo unatakiwa kujipenda.Siku zote
ukijipenda mwenyewe basi kila kitu kwako kitaenda vile ambavyo kinatakiwa
kiende na lazima utafurahia maisha yako na nchi yako upewayo na Bwana Mungu
wako.
Ukijipena
wewe mwenyewe kuna baadhi ya vitu ambavyo vinaitajika kujifanyia mwenyewe
badala ya kusubiri mtu mweingine aje akufanyie.Ukikaa na kusubiri mtu unayempenda akufanyie, nina uhakika kabisa
kuwa inawekana,ukasubiri milele na vitu hivyo visitokee.Kwa hiyo basi
ukijipenda wewe mwenyewe utaweza kufanya
vitu kama unavyotaka.
Mambo Ya Kudhingatia Unapofanya Maamuzi.
Unapo
jipenda mwenyewe kuna mambo ambayo unatakiwa kuyadhingatia ili maisha yako
yaende sawa.
d.Jiamini
katika kufanya kazi kwa kile ambacho unakuwa unakihitaji.
g.Kuwa mtu wa kujifariji na kujitia moyo pale ambapo utakuwa umekosea na kufanya mambo yako yawe rahisi.
Bila
shaka hayo mambo yaliyotajwa hapo juu ya nakupa tunaini kubwa la kuweza
kujipenda mwenyewe,kwani kila kitu kitaenda katika mstari wako na hiyo ni
habari njema kwa kila mtu.
Kujipenda Mwenyewe Hakuna Gharama.
Kujipenda
mwenyewe hakuna gharama yoyote ile zaidi ya wewe mwenyewe kujitambua na kujua
ni nini ambacho unakitaka katika maisha yako.Unaweza ukajiuliza nitawezaje
kujipenda Mimi mwenyewe?.Tazama hapa chini imeandaliwa njia kadhaa ambazo
zitasaidia katika safari yako ya kuanza kujipenda wewe mwenyewe na utazifurahia
bila shaka kwani zitakusaidia sana katika kuyaendesha maisha yako na ya
wengine.Mtu asipojipenda yeye wenyewe hawazi kumpenda mtu mwingine,nikama mtu
hasipo jihurumia hawezi kumuhurumia mtu mwingine.
Mambo Ya Kufanya Unapo Jipenda Mwenyewe
1:Jiongeleshe
Mwenyewe Kama Vile Unaongea na Mtu Ambaye Unampenda na kumjali.
1.Ongea Wewe Mwenyewe Kama Unaongea Na Mtu.
Mara
nyingi tunapoongea na watu ambao tunawapenda na kuwajali huwa tunatunia sauti
tamu yenye upole ndani yake bila kusahau maneno ya busara na yaliyojaa
ustaarabu ya kutosha ili tu waweze kutuelewa na waweze kutambua kuwa tunawajali
na kuwapenda.Vivyo hivyo kwako mwenyewe unatakiwa uongee ndani ya kichwa chako
kwa sauti tamu yenye upole huku ukiwa na maneno ya busara hakika na kwambia
utajisikia vizuri sana na utaona ni jinsi gani una upendo wako mwenyewe na
ujitaidi mara njingi kuonea maneno yenye
kutia moyo na faraja moyo wako.Epuka kuongea maneno mabaya ya kukukatisha tamaa
na kukifanya kujiona mnyonge katika jamii.
2.Jione Mwenyewe Katika Macho Ya Yule.
Mfikirie
mtu yeyote anayekupenda anaweza kuwa mtoto wako,mchumba,mama,baba,dada,mtu
yeyote anayekupenda muone kama kasimama mbele yako
anakuangalia,jiulize(a)anaona nini kwako.(b)Akiambiwa akuelezee wewe ni mtu wa
namna gani atakuelezaje.(c)Kwa nini anakupenda?(d)Ni kitu gani anajivunia
kutoka kwako?.Ukifanya zoezi litakusaidia sana kutambua ni jinsi gani unapendwa
kwa kuwa maswali hayo ukijiuliza lazima majibu yake yata kuwa mazuri ambayo
moja kwa moja yatakushawishi wewe mwenyewe kujipenda badala ya kujichukia.penda
nafsi yako kwanza.
3:Kama Kuna Kitu Hukipendi Kutoka
Kwako.
Kama
kuna kitu ambacho hukipendi kutoka kwa mtu mwingine ambaye ni wakaribu yako
bila shaka,utajitahidi kadiri ya uwezo wako ili mtu yule Kibadilishe,vivyo
hivyo kama kuna kitu ambacho hukipendi kutoka kwako huna budi kukibadilisha
kwani kikiendelea kuwepo kinaweza kuyaharidu maisha yako.Mara nyingi vitu vingi
ambavyo huwa hatuvipendi kutoka kwetu wenyewe huwa vinatokana na malezi ambayo
tumekulia kwa mnda mrufu,kwa hiyo kuna vijitabia ambavyo unakuta sio vizuri na
huwa hatuvipendi.Basi ukishatambua kuwa kuna kitu ambacho hukipendi kutoka
kwako hanza kukibadili kitu hicho kwa maana hakuna kitu ambacho kinashindikana
chini ya jua hasa ukiwa umeamua kutoka moyoni kwamba kitu fulani lazima
nikiache kwani hakifai katika maisha yangu.
Jihudumie Vizuri Wewe
Mwenewe.
Watu
wengi huwa tunajua kuwapa zawadi watu tunaowajali na kuwapenda na katika
orodha ya kuwapatia zawadi huwa
tunasahau kujiweka na sisi wenyewe.Tunachohitaji ni wengine kuwa na furaha huku
Sisi tukiwa nyuma na wanyonge.
Yabadili
maisha yako sasa kwa kuweza kujipendelea wewe mwenyewe kwenye ile orodha ya
watu wanaostahili kupata zawadi kutoka kwako mwenyewe halafu ya wengine
yafuate.Unapojipa zawadi mwenyewe unajipa nafasi kubwa ya kujipenda na kuona
kabisa kuwa unastahili vitu vizuri katika maisha yako na usisite kujipongeza
kwa zawadi uliyojipatia.
5.Jisikilize Wewe Mwenyewe.
Mara
nyingi tunapenda kusikiliza mawazo ya watu wengine huku tukiwa hatujipi na fasi
nzuru ya kusikiliza mawazo yetu ambayo kwa kiasi kikubwa yanaweza kutusaidia
sana katika maisha yetu.Ukiwa na tabia ya kujisikiliza wewe
mwenyewe,nakuakikishia kwamba kila kitu lazima kitaenda sawa.Lakini wakati
ukiwa unajisikiliza wewe mwenyewe haimaanishi kuwa mawazo ya watu wengine
hayana nafasi,lakini pia mawazo ya watu wengine yawe na nafasi pia.kwa hiyo
jijengee mahusiano mazuri wewe mwenyewe kwa kujisikiliza wewe mwenyewe huku ukiendelea kujipenda wewe
mwenyewe.
6.Jiulize Ni Vitu Gani Unahitaji Wewe Mwenyewe.
Jiulize
ni vitu gani unahitaji kwa kujiuliza mwaswali haya.
a.Je
nahitaji nini kwa sasa?
b.Je
nahitaji muda wa kukaa peke yangu?
c.Je
nahitaji kurahisisha maisha?
d.Je
nahitaji muda wa kucheza na kufurahia maisha?
e.Je
nahitaji kwenda sehemu yoyote?
Hayo
ni baadhi ya maswali ambayo unaweza kujiuliza wewe mwenyewe katika harakati za
kujipenda zaidi na zaidi wewe mwenyewe.Bila shaka au mashaka akitokea mtu
akikutatulia maswali yako hayo hakuna utakachokifanya zaidi ya kumpenda sana
mtu huyo.Itakuwa vyema maswali ukiyatafutia ufumbuzi wewe mwenyewe ili ujipe
nafasi ya kujipenda.Kukifanikiwa kujipenda utaona maisha yako yanavyobadikika
na wala hautajuta katika maamuzi yako ya kujipenda wewe mwenyewe kwanza,halafu
wengine wafuate ni uamuzi mzuri utakuwa umejitendea haki.
Kuipenda Nafsi Yako Kuna Maanisha Nini?
Kumbuka
kwamba tumekwisha kufahamu maana ya kupenda,mwanzoni mwakitabu hiki.Kimetuambia
kwamba,watu wengi wametoa maana tofautitofauti za upendo.Sasa fahumu kwamba
wanatoa maana ya upendo kutokana na aina za upendo.Jambo ambalo sio
sahii.Kumbuka maana ya upendo halisi ni
kumbatio,maanuzi,aminio,adhimio,kukubali,kuridhia,atamio la moyo nafsi na
akili.Na ili kufahamu kuipenda nafsi yako kunamaanisha nini endelea kusoma hapo
chini.
Kuipenda Nafsi Yako Kwa Afya Ya Roho.
Ili
kufamu kuipenda nadsi yako,Kumbuka kwamba ni tamko la maandiko matakatifu yaani
Blblia takatifu.Kumbuka Mungu aliumba mtu akiwa
nafsi hai. Mwa 2:7. Zab 66:9. Bwana wetu Yesu Kristo alisema kwamba Luk 17:33,Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi
yake,ataiangamiza;na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.Math 16:25-26, kwa kuwa
mtu atakaye kuiokoa nafsi yake,ataipoteza,na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa
ajili yangu ataiona.Kwanza atafaidiwa nini mtu akiupata
ulimwengu wote,na kupata hasara ya nafsi yake?Au mtu atatoa nini badala ya
nafsi yake?. Katika maandiko hayo mawili kuna mambo muhimu ya
kutafakari sana.Moja kuangamiza nafsi.Mbili kuiponya natsi.Tatu kuipoteza
nafsi.Nne, kuiona nafsi.Kupoteza nafsi hapa linamaanisha kwamba,kukosekana na
kutojulikana na kutojali mambo ya ulimengu,kwa hiyo katika mambo ya mwili tumwe
wafu.Kut 20 :13-17.Usiuwe,Usizini,Usiibe,usishudie uongo,Usitamani.Gal
5:19-21.Basi matendo ya mwili nidhahiri,ndiyo
haya,uasherati,uchafu,ufisadi,ibada ya
sanamu,uchawi,uadui,ugomvi,wivu,hasira,fitina,faraka,uzushi,husuda,ulevi,ulafi,na
Mambo yanayofanana na hayo,katika hayo aawaambia,mapema,kama nilivyokwisha
kuwaambia,ya kwamba watu watendao Mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa
Mungu.1Yoh 2:15-17. Msipende dunia,wala mambo yaliyomo katika dunia.Mtu
akiipend dunia,kumpenda baba hakumo ndani yake.Maana kila kilichomo
duniani,yaani,tamaa ya mwili,na tamaa ya macho,na kiburi cha uzima,havitokani
na Baba,bali na vyatokana na dunia.Na dunia inapita,pamoja na tamaa zake,bali
yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.Gal 5:22-24.Lakini tunda la
Roho ni upendo,furaha,amani,uvumilifu,utu wema,fadhili,uaminifu,upole,kiasi,juu
ya Mambo kama hayo hakuna sheria.Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili
pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake
.Ukimpenda Mungu utaipenda nafsi yako ambaye ndiye chanzo cha nafsi yako.Ukimpenda Mungu utangamiza nafsi yako,na mambo ya dunia hayatakuwa tena na mvuto kwako.Imeandikwa katika 1Yoh 2:15-17,huwezi kufurahia anasa za ulimwengu na kuwa rafiki wa Mungu.Imeandikwa katika Yak 4:4. Je ni mambogani mabaya?Imeandikwa Gal 5:19-21.Usifuate mambo yanayopendwa na dunia yasiyo mema.Imeandikwa katika Rum 12:2. Kumjua Yesu Kristo kunakata tamaa za ulimwengu.Imeandikwa katika Gal 6:14.Epuka elimu za dunia.Imeandikwa katika Kol 2:8.Ishi kama makao yako yako mbinguni.Imeandikwa kataka 1Pet 2:11.
Ifungue Nafsi Yako Katika Kifungo Cha Nafsi.
Mwanadamu
ana sehemu kuu tatu ambazo ni,mwili,nafsi na roho.Kazi ya nafsi ni kuunganisha
mwili na roho.Biblia inaongelea kuhusu uumbaji uliofanywa na Mungu kama
ilivyoandikwa.Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi,akampulizia
puani pumzi ya uhai mtu akawa nafsi hai.Ndiyo maana kila mwanadamu
alifinyangwa kutoka kwenye mavumbi ya ardhi,na kitendo cha Mungu kumpulizia
pumzi huyu mwandamu,maana yake Mungu aliweka Roho.Mtu akawa nafsi hai na hivyo
Biblia haisemi kwamba mtu akawa roho hai bali nafsi hai.Maana yake kama nafsi
iliwekwa ndani ya mtu vivyo hivyo nafsi yaweza kuondolewa na mtu kufa.Kuna mtu
wa mbinguni na kuna mtu wa duniani.Ndivyo
ilivyoandikwa,Mtu wa kwanza,Adamu,akawa nafsi iliyo hai;Adamu wa mwisho ni Roho
yenye kuhuisha. 1Kor 15:45-47. Maana yake mbinguni hakutoki udongo,bali
roho.Mtu wa kwanza udongo mtu wa pili ni roho.Zab 14:7,Uitoe nafsi yangu
kifungoni.Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki wata nuzunguka.Kwa kuwa wewe
unanikirimu.Nafsi inaweza kuwekwa kifungoni.Fahamu kwamba ndani ya
nafsi ndiko kunakowekezwa aina zote za
elimu na imani na ujuzi.Daudi alijua kwamba nafsi yake ilikuwa salama,na kama
nafsi iko salama mambo yote yatakuwa salama.Na ukimwona mtu ye yote hajisikii
raha akiwa ndani ya Kristo,ujue tayari nafsi yake mtu huyo ipo kifungoni.Hesabu
30:10-13,Ayubu 33:18,22,28.Zab 35:7. Mith 3:4-5:( Zab 86:13)(Mith 23:13-14( Luk
9:23-24)Yoh 12:25,Gal 2:20,Rum 12:2(1Sam 2:30-35)Moyoni mwangu nimeliweka neno
lako. Zab 119:11,Kut 15:19,123:4
Bishpo
Rhobinson S.Baiye
rhobinsons.blogspot.com
Whatsapp:0764127531
Mwanza Tanzania
No comments:
Post a Comment