UPENDO WA KIMAPENZI MAHABA.
Kumbuka kwamba kuna aina tano za upendo.Lakini katika kitabu hiki tutatafakari kuhusu upendo wa kimapenzi mahaba.
1.Upendo wa Ki-Mungu.
2.Upendo wa Kirafiki.
3.Upendo wa Kindugu.
4.Upendo wa Kimapenzi Mahaba
5.Upendo wa Kujipenda Mwanyewe.
Maana Ya Upendo Wa Kimapenzi Mahaba.
Upendo wa kimapenzi au kimahaba unaokuwa kati ya watu fulani kusababisha watu hao kuwa na uhusiano wa kimapenzi(mahaba)kati yao.yaani watu wawili mtu mme na mtu mke.Tunaona neno la Mungu katika kitabu chake maalumu kinachohusu mahaba ya wapenzi wa wili.kitabu cho wimbo ulio bora.Mapenzi na neno la Kiswahili linalojumlisha idadi kadhaa ya hisia,kuanzia mahaba,pendo hata upendo wa ki-Mungu.Ni kwamba kitenzi kupenda kinaweza kurejerea aina,za hisia hali za mitazamo tofautitofauti,kuanzia ridhaa ya jumla ya kitu(Napenda kula hiki)maamuzi kati ya watu wawili na kumbatio,kubalifu,zingatio,atamio la moyo na nafsi na akili.Kwa utaratibu wa Mungu na jamii zilizo sawa sawa”Eros ni aina ya upendo unaotakiwa kuwa kati ya watu wenye uhusiano wa ki-ndoa,yaani mtu mme na mtu mke. Aina zote za upendo zinahusisha moyo nafsi na akili,lakini Eros huwa na sifa ya kuwa na hisia zenye nguvu zaidi kutoka moyoni kuliko aina zingine zote za upendo.Eros ni aina ya upendo wenye nguvu kali sana ya hisia za binadamu.Tunaona neno la Mungu katika kitabu maalumu kinachohusu mahaba ya wapenzi wawili.Kitabu kiitwacho Wimbo Ulio Bora. 8:6,Neno la Mungu linasema kwamba upendo Eros una nguvu sana kama mauti.Nguvu hiyo ya upendo huunganisha nafsi,fikra,hisia na maamuzi yao kwa sababu ni upendo uliolenga kujenga nendoa Nzuri na familia Bora kabisa.
Mifano Ya Upendo Wa Kimapezi.
1:UpendowaYakoboKwaRaeli.Mw29:10-30.
Yakobo
alipomkimbia kaka yake Esau,alikimbilia nchi ya mbali,nchi ya mama yake kwa
mjomba wake Labani.Labani alikuwa na binti wawili,mkubwa aliitwa Lea na mdogo
aliitwa Raheli.Neno la Mungu Biblia inasema Lea alikuwa na macho mazito,yaani
ukimwangalia,utadhani amelala,kumbe ndio anakuona.Na Raheli alikuwa na umbo
zuri la mwili na sura nzuri ya usoni.Biblia inasema Kwamba,Yakobo alimpenda
Raheli. Mw 29:16-20. Labani
alimwambia Yakobo akachunge wanyama wake kwa mnda tena wa miaka saba nyingine
kama mahari,ndipo atampa Raheli kuwa mke wake.Yakobo alipendezwa na hilo,na
alikubali kutumika na kuchapa kazi kama kawaida yake ya uchapaji kazi.Kwa jinsi
Yakobo alivyompenda Rahali kwa upendo wa Eros,Yakobo alikamatwa kimapenzi kuwa
mke wake alichapa kazi Sana Na kwa bidii kiasi kwamba,ile miaka saba ilionekana
michache sana.Hiyo ni nguvu ya upendo Eros.Yakobo alimtwaa katika upendo Eros
kwa Raheli na ilikuwa kali sana.Upendo Eros ina uwezo wa kufanya mtu asione
ugumu wa kazi,asione machungu,asione umbali wa mwendo,asione ukali wa
jua,asione aibu wala woga mbele za watu wengine.Eros ina nguvu sana juu ya mtu
mwenyewe hata kutawala utu wake wote.Eros ina nguvu ya fikra,hata kutawala
mawazo ya mtu,Eros ina nguvu ya hisia,hata kutawala kuhisi kujisikia kwa
mtu,Eros ina nguvu ya Maamuzi,hata kutawala matendo ya mtu kabisa.Unaweza
ukamkuta kijana siku hizi ni msafi sana kuliko unavyomfahamu,kumbe amekwisha
kamatwa na binti mwanamwali kama Yakobo alivyokamatwa na Raheli.Yakobo alijaa
Raheli katika mawazo yake,kila saa alikwa akimuwaza Raheli kwa mnda
mrefu.Yakobo alijaa Raheli katika hisia zake kiasi cha kutosikia machungu ya
ile kazi na hata kuona miaka saba kuwa si kitu kikubwa,Yakobo alijaa Raheli
kataka Maamuzi yake,hata kumfanya afanye kazi kwa nguvu kama roboti ili tu
kumpata Raheli.Raheli ndiyekuwa nguvu na hamasa ya Yakobo kudamka alfajiri na
mapema kwenda kulisha mifugo ya mjomba wake Labani.Upendo Eros una nguvu kama
mauti.Upendo wa kimapenzi huwa kati ya watu wawili wanaoelekea katika uhusiano
wa kudumu wa kuwa mme na mke.Hahukuw mpango wa Mungu kwamba upendo huo wa
kimapenzi kuwa wa kujiribu na kuacha,kwa sababu eros ni upendo wenye nguvu sana
ya hisia,hivyo huathiri sana moyo, ufahamu, hisia za mtu pengine hata afya ya
mwili wa mtu kabisa kama hatajua kuutawala ipasavyo.Hivyo eros si upendo wa
kuingia na kutoka utakavyo,kama mtu abadilishaye nguo.
2: Upendo wa Isaka kwa mkewe Rebeka.Mw 26:1-12.
Isaka
alikuwa akiishi kataka nchi ya Wafilisti.Watu wale wakamwona Rebeka,wakavutiwa
na uzuri wake,hata wakamtamani.Wakamuuliza Isaka,ee bwana huyu msichana
tunayemwona katika boma lako na wakati mwingine unaambatana naye,ni nani
kwako?.Isaka aliogopa kusema ni mke wake,kwa maana wange muua Isaka ili
wamchukue Rebeka,kwa ajili alivyokuwa mzuri
wa kuvutia.Isaka aliwaambia kwamba ni dada yake nao waka mwacha.Lakini
kumbe wale watu walitumwa na mfalme wa Wafilisti,ili kumpeleleza na kujua
uhusiano wao, kwasababu mfalme alivutiwa sana na uzuri wa Rebeka,akataka
kumuoa.Na hata siku moja mfalme Abimeleki alipokuwa akipita mtaani,akakatiza
mtaa ambao nyumba ya Isaka ilikuwepo.Mfalme Abimeleki akachungulia
dirishani,akamwona Isaka akichezacbeza na Rebeka mkewe”kimahaba,mfalme
Abimeleki akamwita Isaka,akamwambia,kwa jinsi nilivyowaona mkichezeana vile
lazima huyu ni mkeo,huwezi kucheza-cheza vile na dada yako,mbona uliniambia
kwamba huyu ni ndugu yako?.Isaka akajibu niliogopa nisije nikauwawa kwa ajili
yake.Basi Abimeleki akamlaumu Isaka,kwa kusema,mtu mmoja wetu angelala na
Rebeka bila kufiliri ni mkeo kwasababu ulisema mwenyewe ni dada yako.Ndipo
mfalme akaamuru watu wote wasimguse Isaka wala mkewe,akasema amgusaye mtu huyu
au mkewe lazima atauawa.
Ifahamike
kwamba tuingipo katika mahusiano ya kimapenzi ndoa tuwe tume fanya maagano na
Mioyo na nafsi na akili zetu.
Dalili Na Sifa Za Upendowa Kimapenzi.
RomanticLove
1.Mvuto kwa haiba yake na kuchukuliana nayo(Mwonekano na Tabia)
2.Kukaa
mawazoni kwa mtu anayependa kujaa moyoni.
3.Shauku
kubwa ya kuishi pamoja kila wakati.(Kuambatana)
4.Heshima
kubwa kwa mtu anayependwa.(Kipaumbele.
5.Kumjali
na kumtanguliza mtu 'apendwaye.
6.Zawadi
na gharama kwa mtu apendwaye.Kujitoa.
7.Furaha
na Amani kutawala moyoni.
Kumpata Mwenzi Wako Wa Ndoa.
Mith 19:14-21.
a.Mweleze Mungu Haja Zako.
b.Mwombe Mungu Akukutanishe Na Mwenzi Wako.
c.Tengeneza Marafiki.
d.Thibitishia Moyo Wako Kwamba Umependa Kweli Kweli.
e.Ishasha Za Kutambua Penzi La Kweli.
f.Omba Ushauri Kwa Watu.
g.Mwendee Na Useme Naye Kwa Hekina.
h.Thibitisha Uhusiano Wako.
a:Mweleze Mungu Vizuri Zile Haja Za Moyo Wako.
Mungu
ameahidi kuwa atakupa mtu w kufanana na wewe. Mw 2:18. Kwa hiyo
ni muhimu sana ujijue wewe ukoje,kisha ndipo utaweza kumweleza Mungu na
kumwomba akupe mtu wa haja ya moyo
wako.Hivyo ni muhimu sana kujijua kujitambua na kujielewa kwa jinsi uluvyo na ni
aina gani ya watu ambao wewe unaendana nao.Hii ni kwa sababu watu tuko
tofauti.Unaweza kuishi na mtu yo yote duniani,lakini hutaweza kuishi vizuri na
kila mtu.Maisha mazuri yanakuja kwa kukutana na mtu ambaye mnaelewana na
mnaendana.Ndio maana Mungu alisema kuhusu Adamu kwamba,mwenzi wake wa maisha
atafanana naye.Usimfiche Mungu haja za moyo wako.Kumbuka yeye ni baba yetu na
sisi tu watoto wakewapenzi.Fahamu kwamba Mungu anaheshimu sana,haja za moyo
wako ambazo zitakupa wewe furaha ya Maisha. Math 7:7-11,Zab
145:17-18,Isaya 45:11,1Kor 7:39.Maombi yako ya bidii yatampa Mungu
kumchonga,kumwanda.Kila kitu uubwa na kuandaliwa mapema na Mungu.Maombi ya
mwenye haki yafaha sana mtu akiomba kwa
bidii . Yak 4:16,Kol 4:2.
b:Mwombe Mungu Akuonyeshe
Na Akukutanishe
Na akukutanishe na mwenzi wako.
Kila
mmoja wetu ambaye Mungu amempangia kuwa na mwenzi,ana mwenzi huyo mahali fulani
hapa duniani.Lamsingi ni kufanya Maombi kuomba Mungu kumfinyanga na kumchonga
huyo mwenzi wako popote alipo.La pili inahusu kumwomba Mungu kusababisha
mazingira ambayo yatawakutanisha na kutambuana baada ya kupata ufahamu wa Mungu
ya kwamba ndiye.Hiyo ndiyo maana halisi ya kufunuliwa au kuonyeshwa.Zab
32:8,Isaya 43:26,45:11,Efe 1:15-19.
c:Tengeneza Marafiki Wa Kweli.
Watu
wengi humwomba Mungu kwa uaminifu sana ili wapate wenzi wa maisha.La kini
wanafanya makosa makubwa ya kujifungia katika kisiwa cha upekee.Ni ngumu sana
kuonekana na kujulikana tabia na utu wako wa ndani kama hutachangamana na
jumuiya za fahumu kwamba Mungu ndiye chanzo cha urafiki.Hata Yesu Kristo
alikuwa na marafiki wa kiume na wa like pia. Yoh 11:5.Jitaidi
kufanya marafiki mbalimbali ila mwombe Mungu akupe marafiki wazuri.kwa kuelewa
vizuri kuhusu marafiki soma mada na kipengele,kinachozungumzia aina ya upendo
wa kirafika katika sura hii ya kwanza katika kitabu hiki.
d.Thibitasha Moyo Wako Kwamba Unampenda
kweli.
Kadri
unavyoendelea na maisha ya uaminifu katika wokovu,maombi na kujifunza neno la Mungu na kumtumikia
Mungu kwa namna mbalimbali,Mungu atasababisha ukutane na mtu anayefanana sana
na haja za moyo wako kuhusu mwenzi wa maisha.Utahitaji usikivu mkubwa wa rohoni
kutambua aina gani ya upendo unaingia moyoni mwako kuelekea kwake kwa sababu
kuana aina tano za upendo.Upendo wa ki-Mungu,upendo wa kindugu,upendo wa kirafiki,upendo
wa kimapenzi, upendo wa kijipenda mwenyewe. Muh 9:8-9. Kati ya
watu unaofahamiana nao,yupo mmoja ambaye atakuwa watofauti sana ndani
yako.Mungu atampa kuonekana watofauti sana kuliko wengine wote
wanaokuzunguka.Hivyo kabla ya kwenda kusema naye na kumshirikisha uonavyo wewe
moyoni mwako,thibitisha kimaombi tena na tena kwamba ndimi yako Kuna
upendo wa kweli kwa ajili yake.Marko 5:25:34(30). Inasema wangi
walimgusa Yesu lakini mmoja tu ambaye atakuwa na mguso qa tofauti katika moyo
wako.
1.Mtu huyo atakamata umakini wako na atakuvutia.
2.Mtu huyo atajaa katika mawazo yako kuliko kawaida
na wengine.
3.Utatamani sana uwepo wake mtu huyo katika wote
kuwa naye.
4.Utapenda kuwasiliana na mtu huyo mara kwa mara
kuliko wote.
5.Utakuwa na moyo wa kujali,wema zaidi na kujitoa
sana kwake.
6.Utakuwa na heshima ya hali ya juu sana adabu utii
uaminifu kwake.
7.Tatakuwa na maneno mazuri maneno laini,maneno ya
upendo kwake.
8.Utakuwa na moyo uwezo wa kumvumilia au kumchukuliana
naye vile alivyo.
9.Utakuwa na hamu ya kumgusa kumshika kwa upendo
wala sio tamaa.
10.Utakuwa na moyo na utayari wa kumlinda na
kumhifadhi.
11.Upendo wenu utapendeza mbele ya watu wengi si
lazima wote.
12.Utakuwa na amani na furaha ya hali ya juu moyoni
mwako.1Kor 13:4-8.
f.Omba Ushauri Kwa Watu.
2Kor 13:1,Zab 73:24, Mith 15:22.
Ushauri
kutoka kwa watu werivu walionahufu ya Mungu ndani yao,na wanao wajua na
kuwafahamu vyema ninyi wawili utakuthibitishia kwamba ulichosikia moyoni juu ya mtu huyo Ni sahihi.Wakati
mwinginse si wakati wote watu wa pembeni huwa na uwezo wa kuona mbali
zaidi.Wanaweza kuona vitu ambavyo ninyi mlio ndani ya urafiki hamuoni
bado.Washauri wanaweza kutumiwa na Mungu kuthibitisha mawazo uliyo nayo na
mipango uliyonayo.Ushauri wa watu unaweza kusaidia kufanya maamuzi magumu
muhimu.Math 18:16,1Tim 5:19,Ebr 10:28. Mwombe Mungu akuongoze kwa
watu wazuri wenyehofu ya Mungu ndani yao wenye hekima watakao washauri.Lakini
la muhimu liko kwako wewe kuliko watu wote.Washauri watabaki kuwa washauri wala
wasiwe waamuzi,wewe ndiwe uwe mwamuzi wa mwisho.Ni vizuri kupima ushauri wote
unaopewa kwa maombi na kwa uongozi wa Mungu.Wakati mwingine Mungu anaweza
kukuongoza kitu ambacho hakuna mtu mwingine anachokiona ukionavyo wewe.Neno la
Mungu linasema kwamba amani ya Kristo itakusaidia kufanya maamuzi.Kol
3:15,Isaya 55:12.
g.Mwendee Na Usemenaye Kwa Hekima.
Wimbo
ulio Bora 3:1-4.
Baada ya maombi ya subira,Mungu akuongoze kusema naye kwa wakati utakaoongozwa na Mungu.Uwe jasiri na muazi.Useni wako uwe wa kawaida usichague maneno magumu wala misamiati wala mafumbo.Uwe wazi na wa kawaida sana.Usiyatumie maneno ya kiroho saaaaaana,ili kumtisha usitumie maneno kama Mungu ameniambia au Mungu amesema Bwana wa majeshi,maneno kama haya yanamfunga mtu kusema ndiyo”kwa maana atashituswa nayo na kuogopa lakini kama ni mtu jasiri na hajakupenda hajakukubali,mtapambana.Huo sasa si mwelekeo mzuri.Kijana mmoja alipomfikia mt u ambaye moyo wake wa tamaa ulimwishi na alimwendea akaanza kuporomsha maneno makali mfano anazungushia mlima wa moto,hutaolewa na mtu mwingine ila mimi,na ukinikataa,Bwana atakutapika.Hii si hekima ya Mungu.Mungu harumii nguvu,ikiwa kwenda mbinguni Mungu halazimishi watu je itakuwa ndoa?Wewe ukishasema maneno rahisi, mfano nimeomba kwa muda,na hivi ndivyo ninavyosikia moyoni mwangu kwamba,nakupenda sana,na ikiwa itampendeza Mungu na wewe pia,basi na uwe mwenzi wangu wa maisha.Ukisha mwambia maneno hayo rahisi au yanayofanana na hayo,amini kwamba kama ni mpango wa Mungu muwe wote pamoja maishani,maombi yako na neema ya Mungu vitamsaidia kufanya uamuzi mzuri kwa ajili yenu wawili.Unaweza kupata jibu la ndiyo au hapana au subiri.Mtu wa Mungu huongozwa na Mungu, halazimishi ovyo kwa kitu kama hiki.Maana yangu ni kwamba,hauhitaji kutumia nguvu za mwili wala akili kuwaza sana.Baada ya kuongea na kutua mzigo wako kwake,pumzika na umwachie Mungu kumalizia kazi.
h.Thibitisha Uhusiano Wako,Wenu.
Wimbo ulio Bora 3:4.
Baada
ya kuliongea na kulitafakari pamoja kwa muda mtakaoona unatosha au unafaa,ni
muhimu.Sasa mpelekane mbele katika mamlaka zenu za kifamilia na
kikanisa.Uhusiano mzuri usiwe wa mafichoni.Tunaona huyu mpenzi katika kitabu
cha Wimbo anasema,anataka kumtafuta mpenzi wake,amshike mkono,wapelekane kwa
wazazi.Huo ndio utaratibu mzuri kibiblia.Familia na kanisa watawasaidia kufuata
taratibu za kiutamaduni na kiroho ili mhalalishwe kuwa mume na mke.Ndipo ndugu
na marafiki mtawashirikisha mipango yote ili kuandaa arusi yenu
Bishop:Rhobinson
S.Baiye
rhobinsons.blogspot.com
Whatsapp.0764127531
Mwanza Tanzania
No comments:
Post a Comment