UBORA WA LUGHA N0 2
Kitabu hiki
kiitwacho ubora wa lugha namba mbili kinahusu hasa na lugha ya kushawishi mtu
au watu kumwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wao.Kitabu hiki kinakupa
mbinu muhimu ambazo zitatufanya tuweze kuwashawishi watu kujiunga na makanisa
yetu ili zipate kuimarika na kustawi.Ubora wa lugha namba moja kimo katika
Tuvuti hii kaisome utakifuraia
sana.Itapendeza kama utasoma kwanza namba moja ili upate kuelewa namba mbili
hii.Nimemnukuu Daktari Mark Goulston. Anasema mambo mengi katika lugha
inayoshawishi msome hapo chini
.Daktari Mark Goulston Anasemahivi:
1:Kila Mtu Ana Mahitaji Yake.
Kila
mtu ana mahitaji yake,matamanio yake na pia ajenda zake.Na tena kila mtu ana
siri yake ambayo anaificha,na hataki watu wengine waijue.Na pia kila mtu
anapilika zake na msongo wa mawazo,na hana muda wa kumtosha kufanya kila
anachotaka kufanya.Ili kuweza kwenda na hayo yote yanayoendelea kwenye maisha
yake,mtu anajitengenezea ukuta ambao bila ya kujua hayo huwezi kumshawishi kwa
jambo lolote.Fahamu kwamba ukitaka mtu afanye au akupe chochote unachotaka,anza
kwanza kuvunja ukuta huu ambao kila mtu amejijengea.Kanisa ni lazima kuvunja
ukuta ambao umejengeka na kila mshirika kama mahitaji binafsi,matamanio binafsi,siri
zake binafsi,imani,za kigeni,mategemeo,matumaini,mila,testuri,na lugha
utamaduni,ili Kuimarisha na kustawisha kanisa. Za 11:10,14,2:9,3:7,7:2,28:5,29:5,46:9,48:7.Mith
15:4, Mik 2:13,3:3,Ombolezo 2:9,3:4 Math 5:19,6:19,12 :1,20,26:61,27:40,
2:Ushawishi Na Mzuguko Wake.
Ushawishi
unaenda kwa mzunguko ambao ana hatua tano muhimu.Yaani kabla mtu hajashawishika
kufanya chochote unachomwambia,anapitia hatua hizi tano ambazo unatakiwa
kuzijua na kujua jinsi ya kumpitisha mtu kwenye kila hatua.
a:Hatua Ya Kwanza.
Hatua
ya kwanza ni kumtoa mtu kwenye kukataa mpaka kuwa tayari kusikiliza.Wakati
wowote mtu yupo kwenye hali ya kukataa, unahitaji kuwa na mbinu ya kufanya
akusikilize.Tumia lugha ambayo mtumishi kiongozi mshirika na asiyeamini
ashawishike kukusikiliza sio lugha ya kumweka mbali nawewe na kanisa.Kufanya
hivyo kutaimarisha na kustawisha kanisa.
b:Hatua Ya Pili.
Hatua
ya pili nikumtoa mtu kwenye kusikiliza mpaka kukufikiria.Hapa mtu anakuwa
amesikiliza kile ulichomwambia,na kuna mbinu bora za kumwambia na akaanza
kufikiria kwamba anaweza kufanya au anaweza kuwa tayari.Ni vema kutumia lugha
ambayo itamweka mtu unaye wasiliana naye kuwa tayari kulifikiria sana kanisa
lako.Kwa kufanya na kutumia lugha hiyo itaimarisha na kustawisha kanisa lako.
Hatua
ya tatu ni kumtoa mtu kwenye kukufikiria mpaka kuwa tayari kufanya.Baada ya mtu
kufikiria kwamba anaweza kufanya anashawishika zaidi na kuwa tayari
kufanya.Tumia lugha ambayo itamfanya mtu kuwa tayari kufanya kwa ajili ya
kanisa na mtu mmoja mmoja katika kanisa na katika jamii yako.Hiyo ndiyo lugha
bora sio bora lugha,kufanya hivyo kutaimarishana kustawisha kanisa la mahali ulipo.
d:Hatua Ya Nne.
Hatua
ya nne ni kumtoa mtu kwenye hali ya kuwa tayari kufanya na kufanya jambo husika.Hapa ndipo mtu anapofanya kile ambacho
unataka afanye au anakupa kile ambacho ulitaka akupe.Kumbuka Yesu alivyosema
kwamba mwana hakuja kutumikiwa bali
kutumika.Hata Mungu aliziumba mbingu na nchi na vyote viijazayo kwa kutumika
kwa kutamka na kusema na kutumia lugha ya kuumba pamoja na kufanya kazi kwa
mikono yake ili kumuumba mtu,Mungu hakutumikiwa bali alitumika.Tunapotumia
kumshawishi mtu mpaka akatumika kwa ajili ya Mungu na watu wake yaani
kanisa,hiyo ndiyo lugha bora wala sio bora lugha.
e: Hatua Ya Tano.
Hatua
ya tano ni kumtoa mtu kwenye kufanya mpaka kwenye kufurahia kufanya na
kuendelea kufanya.Kufanya siyo mwisho wa mzunguko huu,bali mtu anahitaji
kufurahia kwamba amefanya na kuendelea kufanya kadri inavyohitajika.Na huu ndio
mzunguko wa ushawishi ambao unatakiwa kujua na jinsi ya kutumia kwa watu
mbalimbali.Yafaa sana na kutia moyo mtu anapo fanya kazi au anapo hudumu kwa
lugha ya kanisa huku anafanya kwa moyo wa kufurahi,inaleta afya katika kanisa.Na
tufikie ngazi hiyo ili kuimarisha na kustawisha kanisa na makanisa yetu ya
mahali,na huko ndiko kunena kwa lughampya ambayo inasemwa na maandiko.
3: Fahamu Ubongo Wa Mwanadamu.
Ili
uweze kuwa na ushawishi kwa wengine unahitaji kujua vizuri ubongo wa
binadamu.Ubongo wa binadamu umegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo
zinatofautiana kwa miaka ambayo zimekuwepo.Ubongo ndio kiini cha mfumo wa neva
katika wanyama wote wenye ungwemgongo na wanyama wasio na
ungwemgongo.Ubongo unapatikana katika kichwa ukilindwa na mifupa ya fuvu.Kazi
kubwa ya ubongo ni kuhakikisha viungo muhimu vya mwili kama vile moyo na mapafu
vinafanya kazi ipasavyo.Acha tuone baadhi ya mambo muhimu ya kufahamu kuhusiana
na ubongo,kabla ya kuona mgawanyo wa sehemu tatu kuu za ubongo.
1.Ubongo wa binadamu huwa hauna vipokezi vinavyohusika na maumivu hivyo ubongo hauhisi maumivu kabisa,hivyo mtu anaweza kufanyiwa upasuaji wa ubongo huku ukiwa na ufahamu wake na hauhisi maumivu yoyote.
2:Ubongo ndiyo kiungo pekee cha mwili ambacho hutumia nguvu nyingi sana zaidi ya asilimia 20% ya nguvu zote za mwili hutumiwa na ubongo japokuwa ubongo una asilimia (2) tu uzito.
3:Zaidi
ya asilimia 60% ya ubongo wa binadamu huwa umeundwa kwa mafuta huku asilia 75%
uzito ubongo inabebwa na maji.
4:
Sehemu ya ubongo iitwayo Neocortex.Ambayo ina husika na lugha
pamoja na ufahamu ndiyo sehemu kubwa zaidi kuliko sehemu zote zinazounda na
ubongo, huchukua zaidi ya asilimia 76% ya ubongo wa binadamu kumfanya binadamu
awe tofauti na wanyama wengine katika kuwaza kunena na kutenda.
5:Kila
sehemu ya ubongo hufanya kazi,Jambo hili hufanya binadamu asiweze kutumia
ubongo wake kikamilifu,inasadikika kuwa binadamu hutumia chini ya asilimia 10%
tu ya ubongo wake.
6: Homoni inayoitwa Oxytocin ambayo hujulikana kama homoni ya mapenzi huzalishwa kwa wingi kwenye ubongo,na hupatikana kwa wingi katika matukio ya mapenzi ambayo homoni hii ndiyo huamua umpende nani, umpende vipi mapenzi yenu,na hii homoni ndio huamua umpende nani kwa wingi,lakini pia homoni hii huzalishwa wakati wa kukutana kimwili mwanamme na mwanamke,lakini pia wakati wa uchungu wa kuzaa,na lamwisho homoni huongoza na Kulinda mfumo mzima wa unyonyeshaji wa maziwa ya mama
7:Tukiwa kwenye ufahamu wetu,ubongo huzalisha kati ya watts 10 hadi 23 za umeme ambao unatosha kabisa kuwasha taa moja ya umeme.
8:Kupiga
miayo hutokea mara nyingi baada ya kumuona mtu mwingine kafanya hivyo hii ni
kwa sababu ubongo huwa na seli zinazoitwa seli koo mirror celle.Sehemu
hii ya ubongo huingiza kitendo hiki
kutoka kwa mwingine na kikitokea basi hufanya mtu awe na matatizo makubwa.
9:Ubongo
huwa na mishipa ya fahamu zaidi ya
bilioni 100 hii ni mara 15 zaidi ya idadi ya watu wote tuliopo duniani.
10:Mziki husisimua sehemu ileile ya ubongo ambao hutoa kemikali za raha Dopamine wakati wa kujamiana na kula?
Mgawanyo Wa Ubongo Katika Sehemu Tatu Kuu.
1.Sehemu Ya Kwanza:Ubongo
Wa Nyuma)
Sehemu
ya kwanza ya ubongo ni sehemu ya ubongo wa chini,ambao ni ubongo wa nyuma una
tabia za mjusi.Hii ni ile sehemu ya ubongo ambao kazi yake kubwa ni kuhakikisha
unaishi kwa Ubongo huu kazi yake ni kuakikisha umepata chakula na unaweza
kujikinga na hatari.Ubongo huu huwa unachukua hatua haraka bila hata ya kufikiri
kwa kina.Kwa mfano kama umewahi kuwa kwenye hatari mara kukimbizwa na mnyama
kama mbwa hapo utapata nguvu nyingi za haraka hata kuruka utakuta ambao kwa
kawaida usingeweza kuukuta,hii ndiyo kazi ya ubongo huu.Kama kanisa na kama
viongozi na watumishi kuchukua hatua za haraka unapokuwa uhitaji wa kufanya
hivyo.Mungu aliweka ubongo huo wa chini ili kuchukua hatua za haraka kwa
Kuimarisha na kustawisha kanisa lako.
2.Sehemu Ya Pili: Ubongo Wa Kati.
Sehemu
ya pili ni ubongo wa kati,ambao una tabia za mnyama.Hii ni sehemu ya ubongo
ambayo imebeba hisia zote za mtu.Hisia za upendo,wivu,hata rahaa zipo kwenye
sehemu hii ya ubongo.Sehemu hii ya ubongo ndiyo inatusukuma kufanya vitu
vinavyotupa hisia nzuri na kutuepusha na vitu vinavyoleta hisia mbaya.Fahamu
kwamba unapotumia lugha ambayo hajaeleweka vizuri sehemu hii hufanya kazi kwa
kuhisi kama kuna kitu ambacho kimefichwa watu hawakifahamu mahali hapa.Na hapo
ndipo mwanzo wa mtu kuwa na maswali yasio kuwa na majibu na kukatisha tamaa,na
kulichukulia kanisa,na mwanzo wa kanisa kutokuimarika na kustawi.Lugha nzuri
huusika katika sehemu hii.
3.Sehemu Ya Tatu: Ubongo
Wa Mbele)
Sehemu
ya tatu ni ubongo wa juu ambao una tabia za utu.Huu ndio ubongo ambao
unatutofautisha sisi binadamu na viumbe wengine wote.Huu ndio ubongo ambao
unafikiri kwa kina kwenye kila jambo tunalofanya au linalotokea.Huu ndio ubongo
ambao unatunza kumbukumbu.Ubongo huu unakusanya taarifa kutoka kwenye sehemu
nyingine za ubongo na kufanya maamuzi sahihi.
Tumia
lugha na kufanya maamuzi kwa kutumia ubongo wa sehemu ya juu.Kwa bahati sana
watu wengi wamekuwa wakifanya maamuzi
kwa kuongozwa na ubongo wa chini na ubongo wa kati.Ni mara chache sana
watu wanaweza kuutumia ubongo wa juu vizuri na kufanya maamuzi bora.Maamuzi
mengi yanayofanywa na ubongo wa chini na ubongo wa kati ni maamuzi ambayo yana
faida ya muda mfupi lakini kwa muda mrefu yana hasara kwao.Mfano Ni mtu ambaye
anabaka,hapa anauridhisha ubongo wa kati ambao utapata raha,lakini angetumia
ubongo wa juu angeona siyo kitu sahihi kwake kufanya.
5:Shawishi Mtu Akiwa Kwenye Ubongo Wa Mbele
Ili
uweze kumshawishi mtu yeyote,hakikisha unaongea naye akiwa kwenye ubongo wa
juu.Hakuna kitu unachoweza kumwambia akakusikia na kukuelewa.Haijalishi
utatumia mbinu bora kiasi gani,kama mtu hayupo kwenye ubongo wa juu utapoteza
muda wako.Hii ndiyo maana ni vigumu sana kumshauri mtu ambaye ana hasira,au
hana raha na yupo katikati ya hisia kali za mapenzi.Kuweza kumshawishi mtu mtoe
kwanza kwenye Ubongo wa kati na wa chini na mpeleke kwenye Ubongo wa juu ambapo
anaweza kufikiri sawasawa.
6:Adui Wa Kwanza Wa kushawishi Ni Wewe
Adui
wa kwanza kuwashawishi wengine ni wewe mwenyewe.Ili uweze kuwashawishi wengine
ni lazima wewe kwanza kushawishika.Ni lazima wewe ukubaliane na kile anachotaka
wengine wafanye au kukupatia.Ni lazima
uweze kujithibiti mwenyewe ili kuweza kuwashawishi wangine kuchukua
hatua ambayo unajua ni muhimu.
7:Ondoa Chujio Tayari Unalo.
Ondoa
chujio ambalo tayari unalo.Fahamu kwamba kila mmoja wetu ana chujio ambalo
anatumia kuwachuja wengine kwa kadiri wanavyoonekana au alivyowazoea.Hivyo
tunawapanga watu kwenye makundi kwa kufikiri tunawajua sana.Ili kuweza kuwa na
ushawishi kwa wengine kwanza ondoa chujio hili na mwendee kila mtu bila ya
kumhukumu,kuwa tayari kujifunza zaidi kutoka kwake.Usimweke mtu kwenye upande
wowote,badala yake msikilize yeye na
utapata njia bora za kuweza kumshawishi.
8:Fahamu Kitu Kinacho Kusukuma.
Naomba
fahamu kwamba kila kitu anachofanya,sababu inayomsukuma kufanya.Hakuna mtu
anayefanya kitu kwa ajali au kwa bahati mbaya pekee.Hivyo unapokutana na tatizo
au changamoto kutoka kwa wengine jua Kuna kitu kimewasukuma kufanya
walichofanya.Ili uweze kuwashawishi watu,jua ni kitu gani kinawasukuma wafanye
kile ambacho wanafanya sasa na ni jinsi gani unaweza kuwafanya kuacha
wanachofanya sasa na wafanye kile ambacho unawashawishi wafanye.
9:Mfanye Mtu
Ajisikie Ameeleweka.
Mfanye
mtu ajisikie ameeleweka,ni lazima umwelewe mtu kabla hujakaribia kumshawishi
afanye chochote unachotaka afanye.Jaribu kuvaa viatu vyake na mwelewe wazi ya
kwamba unaelewa kwa nini yupo pale alipo sasa.Na hata kama anafanya kitu
ambacho anakosea, mwelewe kwamba kuna kitu ambacho kinasababisha yeye afanye
hivyo.Usione kwamba yeye hayupo sahihi na kumweleza hivyo,ukienda kwa njia hiyo
atakachofanya ni kujitetea na hutaweza kumshawishi kwa njia yoyote ile.Mwelewe
mtu na atafunguka kwako.
10:Wafanye Watu Wakujali
Kama
unataka wengine wajali kuhusu wewe,anza kujali kuhusu wao kwanza.Moja ya njia
muhimu za kuweza kushawishi watu ni kuwafanya wavutiwe na wewe,na wajali kuhusu
wewe,na wawe tayari kufanya kile ambacho unawaambia wafanye.Lakini hii
haitakuja kuwavunja moyo wewe kukazana,watu wavutiwe na wewe na wajali kuhusu
wewe.Badala yake inakuja pale unapoanza kujali kuhusu wengine,na unapovutiwa na
wengine.Hivyo unapokutana na watu usitumie nafasi hiyo kujisifia zaidi
wewe,badala yake tumia nafasi hiyo kutaka kuwajua zaidi.Ni vema kujua ni jambo
gani wanafanya changamoto gani wanapitia yapi ambayo wameweza kukamilisha.Kadri
unavyojali kuhusu wao wataanza kufunguka kwako na watakuwa tayari kufanya kile
unachotaka wafanye.
11:Ona Thamani Ya
Wengine.
Wafanye
wengine wajione ni wa thamani kwako.Hii ni mbinu muhimu sana kila mshirika wa
kanisa la mahali anatakiwa kuwanayo kama anataka kuwashawishi watu ili
kuimarisha na kustawisha kanisa la mahali watu huchukua hatua fulani.Hakuna
kitu ambacho mtu anapenda kama kuona amethaminiwa.Hii ndio maana watu wanapenda
kuitwa mheshimiwa,bosi,mtaalamu bingwa na majina mengine mengi yenye sifa za
kuheshimika.Mfanye mtu aone ana mchango mkubwa kwenye kile anachofanya na kile
anachotaka afanye ataweka mchango mkubwa pia.Kufanya watu kuwa wa thamani kwako
au kwenu Ni zawadi kubwa sana unayoweza kupata.Hata Mungu alituthamini sisi
wanadamu, maana alituumba kwa mfano na sura yake.Mwa 1:26.
12:Epuka Kueleweka Tofauti.
Epuka
kueleweka tofauti na unavyotaka ueleweke.Katika harakati za kushawishi wengine
unaweza kutoa picha iliyo kinyume kabisa na kile ulichokuwa unataka kutoa
wewe.Mfano unataka watu wakuone wewe ni mwenye busara lakini kwao unaonekana ni
mpumbavu.Au unataka wakuone mwaminifu ila wao wanakuona ni tapeli.Matokeo hayo
hutokana na mtu kutokujiandaa vizuri na kutosikiliza wale ambao anataka
kuwashawishi.Unahitaji kuwafundisha kwa makini na kuona wanapokeaje kile
ambacho unawapa.
13:Tambua Vitu Vitatu Muhimu.
Kuna
vitu vitatu ambavyo vinawasukuma watu kuchukua hatua ,ukiweza kuvitumia vizuri
vitu hivi utaweza kuwashawishi watu iwe ni kwenye kazi,biashara na hata kwenye
familia.Jambo la kwanza ni mapenzi,hamu au shauku.Watu wapo tayari
kufanya kile ambacho wanapenda kufanya na wana shauku kubwa kukifanya.Hivyo
angalia ni kitu gani watu wanapenda na kitumie katika ushawishi wako.Hata Yesu
alikuwa akitazama na kugundua kile wasikilizaji wake wanachohitaji hata kama ni
kinyume na mapenzi yake,aliwafundisha na alikuwa anaeleweka vizuri sana hata
kama wengine hawakuwa wafuasi wake.Jambo la pili ni hamasa watu wanakuwa
tayari kuchukua hatua kwenye jambo lolote ambalo wanapenda.Wafanye watu
wahamasike kwenye kile ambacho unataka wafanye.Jambo la tatu ni fahari.Watu
wanaona fahari pale wanapoona wamekuwa na mchango kwenye Jambo fulani.Watu
wanapoona kile walichofanya kina mchango kwa wengine wanafarijika
sana.Tafadhali tumia vitu hivi vitatu kwa pamoja na utaweza kushawishi watu
kuchukua hatua.
14:Tafuta Na jitahidi Kuwa Mwaminifu.
Uaminifu
ni muhimu sana katika kuwashawishi wengine.Huwezi kuwashawishi watu kama
hawakuamini na watu hawawezi kukuamini kama husemi kweli na kutekeleza kile
unachoahidi.Usiwe na haraka katika kushawishi kwako,badala yake jenga mahusiano
yenye uaminifu,kadiri watu wanavyo kuamini,kutokana na matendo yako na siyo
maneno tu, ndiyo wanavyokuwa tayari kukubaliana nawe.
Lugha yenye mvuto wa kushawishi
Kushindwa
kushawishi kumewafanya watu wayaone
maisha ni adhabu.kushindwa kushawishi kumewaangusha wengi katika ulimwengu huu,
ulimwengu unao kwenda kwa kasi ya ajabu.Si rahisi kushawishi mtu akubali ombi
na kutoa huduma au msaada kwa mtu mwingine.Kazi hii ngumu inaweza kufanikishwa
kwa kutumia mbinu tano (5) rahisi.Mbinu hizo tano ni zifuatazo.
1:Kwenda Sambamba Na Mshawishiwa.
Mshawishi
anapaswa kutazama kwa makini jinsi anayeshawishiwa anavyowasiliana na mshawishi
hili ni pamoja na matumizi ya lugha ya ishara ya mazungumzo na ya maandishi,ili
naye afanye vivyo hivyo.Ingawaje, mshawishi anapaswa kuwa makini ili asionekane
anamkebehi mshawishiwa.Ikiwa mshawishiwa atagundua kuna usanii hatotia maanani
yale anayoambiwa na hatimaye kutokubali kutimiza ombi la mshawishi.
2:Kutimiza Mahitaji Ya Wakati Husika.
Watu
hujipendelea na watu hupenda mahitaji yao yatimizwe kwanza ndipo ya wengine
yafuate.Mshawishi atambue vipaumbele vya mshawishiwa atakavyotekeleza ili
maombi yake yatimizwe kwa urahisi.Mshawishi atazame mahitaji,matakwa,vionjo
nk.ili aweze kuvuta hisia za mshawishiwa.Mshawishi ajitahidi kutimiza kero au
matakwa ya mshawishiwa kwa kadiri ya maadili,hali na uwezo wake kabla ya kutoa
ombi.
3:Mbinu Ya Tatu: Uthibitisho.
Mshawishi
atoe uthibitisho unaoonyesha ya kwamba ombi au lengo lake litatekelezeka bila
ya vikwazo vingi.Mshawishi atoe uthibitisho pasipo na shaka ya kwamba bidhaa
bora baada ya muda husika, baada ya ombi lake kukubaliwa na
kutekelezeka.Mshawishi ashindanishe Uthibitisho wake dhidi ya washindani
wengine.Mshawishi ahakikishe anayosema au kutoa ni ya kweli na
yanawezekana.Mshawishi aonyeshe uhusika au nafasi yake huku akitabasamu ili
kukuza imani na urafiki.Pia mshawishi aonyeshe ya kwamba yupo tayari kutoa
msaada wa ziada kama ikibidi kufanya hivyo.
4:Mbinu Ya Nne:Kuwasiliana Kwa Ufasaha.
Takribani
watu wote wanapenda wakubalike na kueleweka kadiri wanavyohisi ni rahisi,kwa
kadiri ya hisia zao bila kujali jinsi wanavyowasiliana.Mshawishi anapaswa
kujiuliza,je niwasilisheje ombi langu bila ya kumkwaza mshawishiwa?.Ili kufanya
hivyo, mshawishi anapaswa kutumia mbinu za mawasiliano bora.Mshawishi atambue na
kukwepa maneno ambayo huathiri utu wa mtu au jamii husika kama yasipotumika kwa
kuzingatia mazingira na aina ya mazungumzo.
5:Mbinu Ya Tano:Kukubaliana Na Mshawishiwa.
Takribani
watu wote hupenda uridhika kwa kuambiwa “nimekuelewa”.Katika hili mshawishi
ahakikishe anasikiliza kwa makini mawazo yanayofanikisha ombi lake
likubalike.Mshawishi akubaliane pia na mawazo kinzani kabla ya kukosoa au kutoa
ufafanuzi.Kwa mfano,unaweza kuwa sahihi lakini ni bora kama ingekuwa hivi,kwa
maana natambua hali halisi lakini naomba tufanye hivi.Mshawishi ahakikishe ya
kwamba pindi ombi lake litakapokubaliwa na kutekelezeka pande zote mbili
zitafanikiwa ili mshawishiwa akubali kutoa msaada.Mshawishiwa atatoa msaada na
ushirikiano pale atakapohisi anafanya uamuzi sahihi.
Neno La Mungu Mbinu Ya Ushawishi:
Moyo
wa mwenye hekima husababisha kinywa chake kuonyesha ufahamu wenye kina,na kwa
midomo yake huongeza ushawishi. Mith 16:23. Mradi wetu
tukiwa waalimu wa neno la Mungu ni kuelimisha,si akili tu za Kuwafundisha watu
au wanafunzi wetu,bali pia mioyo yao.Efe 1:18. Kwa hiyo, kufundisha kunahusisha
mengi kuliko tu kuwasilisha habari.Mith 16:23.Moyo wa mwenye hekima
husababisha kinywa chake kuonyesha ufahamu wenye kina,na kwa midomo yake
huongeza ushawishi.kwa hakika,mtume Paulo alitumia kanuni hiyo katika kazi yake
ya kufundisha.Alipokuwa korinto,yeye alikuwa akitoa hotuba katika sinagogi kila
sabato na alikuwa akiwashawishi Wayaudi na Wagriki. Mdo 18:4.Kulingana
na chanzo kimoja chenye mamlaka,neno la kigriki linalotafsiriwa hapa kushawishi
lamaanisha kusababisha badiliko la moyoni kupitia uvutano wa ufikirio wa
maadili.Kwa njia ya majadiliano yenye kusadikisha, Paulo aliweza kufanya watu
wabadilishe hasa njia yao ya kufikiri.Uwezo wake wa kushawishi ulikuwa wa ajabu
sana,maadui wake walimwogopa. Mdo 19:24-27. Hata hivyo ufundishaji wa
Paulo haukuwawonyesho wa uwezo wa mwanadamu.Aliwaambia Wakorinto maneno yangu
na kuhubiri kwangu haikuwa kwa maneno ya yenye ushawishi wa hekima bali kwa
wonyesho wa roho na nguvu ili Imani yenu ipate kuwa si katika hekima ya
wanadamu,bali katika nguvu ya Mungu. 1Kor 2:4-5. Kwa kuwa Wakristo wote
wana msaada wa roho ya Mungu wote wanaweza kuwa walimu wenye kushawishi.Mifano
hiyo na mafunsho ambayo Yesu alitoa na kuunganisha yaliwashawishi watu kwa kuwa
alifahamu na kutambua mahitaji na mambo au vitu alivyohitaji.Alitumia lugha
yenye mvuto na kutia
moyo,kufariji,kujenga,kushauri,kukaripia,kukemea,ku'oa,kuteketeza,kupanda.Tujifunze
njia za kushawishi kwa kumwiga Yesu Kristo.Ametuambia kwamba twende kwake na
tujifunze kwake kwa kuwa yeye ni mpole na mnyenyekevu wa moyo.Yesu alionyesha
kuwathamini wote.
Watu Katika Makundi Manne.
Katika
harakati za kuwashawishi wengine nivema ufahamu makundi manne ambayo Wataalamu
wameyahainisha ili kuweza kumshawishi mtu au watu kufuatana na kundi
lake.Unapoelewa na kujuwa kundi ambalo mtu unaye mshawishi alilomo
hatakupashida.
Hawa
watu hujali sana wengine.Wanapenda kuwafurahisha wengine hata kwa mambo yasiyo
muhimu,wanapenda sana hali ya maendeleo.Kwa hiyo kwanye migogoro hawafanyi kazi
vema,hata maamizi yao yanazingatia mapenzi ya watu.Wanataka kusifiwa sana mara
kwa mara.Hawawezi kuwaambia watu mambo magumu na yasiyofurahisha,wana huruma na
wanahusiana mazuri na watu wengi.Kwa hiyo unapomshawishi mtu mwenye kupenda
sifa inakubidi ujipange sawasawa.
2:Kundi La Pili: Senling.
Hawa
ni watu ambao wasiyopenda masula mapya kama hakuna utaratibu wa
kuyashughulikia.Wanataka utaratibu wa kudumu.Wanafanya kazi kwa mpango wakijua
hatua za kufuata na lini kazi itamalizika.Watu au kundi hili hawana uvumilifu
katika mambo yanapo changanyika.Siyo rahisi kuwatia moyo kwa sababu hawaamini
wanayoambiwa juu yao.Wanalinda ukweli na hawakoseikosei mambo.Watu au kundi
hili halishawishiki hata kama ungefanya nini,kwa hiyo watu hawa wasikupotezee
muda wa kufanya mambo mengine.
3:Kundi La Tatu: Thinking.
Watu
hawa au kundi hili halitawaliwi na hisia za wengine.Wanaumiza watu bila
kujua,wanataka maelezo na mafafanuzi yanayooeleweka wazi.Wanaweza kufanya kazi
vizuri hata kama kuna migogoro.Wanapofanya maamuzi hawajali sana mapenzi ya
watu.Wanataka kutendewa haki,hawaogopi wala kusita kuonya au kufukuza watu
wanakosea.Wanaelewana zaidi na watu wanaopenda hoja nao hupoteza marafiki mara
kwa mara.
4:Kundi La Nne. Intuitive.
Watu
hawa au kundi hili linataka kupambana na changamoto n matatizo mapya.Hawataki
kurudia-rudia Mambo,wanataka kuelewa mbinu mpya hata kama hawataitumia.Hufanya
kazi kwa nguvu sana jazba halafu wanapotea.Hurukia mambo ya kuamua kabla
hawajajua ukweli mzima.Wanavumilia Mambo magumu,lakini hawataki Mambo yanayo
rudiwa-rudiwa kila mara.Hawapendi kuchelewa kutekeleza Mambo kwa hiyo wanafanya
makosa mengi.
Uwe Msikilizaji Mzuri.
Mbinu
ya kufundisha kama kushawishi ina husisha kusikiliza bali si tu kusema kama
tuoivyoonyeshwa kwenyeMith 16:23. Ili tuwe wenye kushawishi ni lazima
tuwe na ufahamu wenye kina.Kwa hakika Yesu alikuwa na ufahamu kwa kina kuhusu
watu aliofundisha.Yoh 2:25.
hutumika
kama chombo cha mawasiliano kwa kupashana habari.
b.Lugha,hutumika,kujenga
Umoja,Mshikamano,Ushirikiano.
c.Lugha
hutumika Kukuza,Kutunza,na Kuendeleza tamaduni za jamii.
d.Lugha
hutumika katika kutetea maarifa mbalimbali.Lugha ni nyenzo ya
kufundishia.e.Lugha hutumika kama alama ya utambulisho wa Taifa,Kabila ya jamii
fulani.e.Lugha hutumika kutoaburudani.
Kimeandikwa
na
Bishop.Rhobinson
S,Baiye
rhobinson.blogspot.com
Whatsapp.0764127531
Mwanza
Tanzania
No comments:
Post a Comment