Monday, June 1, 2020

JE WAWEZA KUWA RAFIKI ANAYEFAA?

Mbinu za kuwa rafiki mzuri.

Mnamo Desemba 25,2010, kabla ya mwanamke fulani mwenye umri wa miaka 42)Kujiua aliandika ujumbe kwenye tuvuti ya kijamii.Ujumbe wake ulikuwa kilio chakuomba msaada Ingawa alikuwa na marafiki zaidi ya elfu moja kwenye mtandao,Hakuna hata mmoja aliyemsaidia.Siku moja baadaye,polisi walimpata akiwa amekufa.Alijiua kwa kumeza dawa nyingi kupita kiasi.Leo kupitia teknolojia tumeweza kupata mamia au maelfu ya marafiki kwenye mitandao ya kijamii kwa kuongeza tu majina yao kwenye orodha yetu ya anwani  katika kompyuta.Pia tukitaka kukatisha urafiki na yeyote  kati yao tunafuta tu,jina lake kutoka kwenye orodha yetu.Hata hivyo msiba uliotajwa mwanzoni kuhusu yule mwanamke huko Uingereza unakazia ukweli muhimu,watu wengi hawana marafiki wa kweli.Utafiti mmoja wa hivi karibuni unaonyesha kwamba ingawa watu wanawasiliana sana,idadi ya marafiki wa kweli imepungua.Bila shaka,kama watu wengi wanakubali kwamba ni muhimu kuwa na marafiki wa kweli.Huenda pia umetambua kwamba urafiki unahusisha mengi kuliko kuongeza majina kwenye orodha ya kompyuta au simu yako.Rafiki wa kweli anapaswa kuwa na sifa zipi?.Je unaweza kuwa rafiki mzuri? Ni mambo gani yanayohitajika ili kupata marafiki wa kudumu?

a.Wajali  wengine kweli kweli.

Urafiki wa kweli unahusisha vitendo.Kwa maneno mengine,rafiki mzuri anajua majukumu yake,na ni mwenye kujali.Kwa kweli urafiki unahusisha pande mbili,na kila mmoja anapaswa kutimiza sehemu yake.Lakini kuna faida ya kufanya hivyo.Lakufanya ni kujiuliza kwamba uko tayari kujitolea kutumia muda na mali zako kwa ajili ya rafiki yako?Kumbuka kwamba ili upate rafiki mzuri wewe mwenyewe unapaswa kuwa na

Urafiki wa kweli hauwezi kustawi bila mawasiliano ya kawaida.Kwa hiyo,zungumzeni mambo yanayowapendeza.Msikilize rafiki yako na uheshimu maoni yake.Ikiwezekana, mpongeze na umtie moyo.Nyakati nyingine,rafiki atahitaji ushauri au hata kurekebishwa,na huenda isiwe rahisi kufanya hivyo.Hata hivyo rafiki mshikamanifu anajua jinsi ya kumkosoa mwenzake na kutoa ushauri kwa busara.Rafiki wa kweli anapaswa kujieleza kwa uhuru na asikasirike,na asipokubaliana na maoni yangu.Mimi namthamini sana marafiki zangu ambao wako tayari kutumia muda pamoja nami na kunisikiliza,hasa ninapokuwa na matatizo.Na marafiki zangu hao ni  kama wafuatao.Saleh wa Saleh,Yusuph Sabato,Didas Malango,Sebastiano Kabeza.Mmalabwe Byondo.Ogi Byondo.Marafiki wa kweli watakuambia ukweli hata kama wanajua kwamba utaumia kwa sababu wanakujali.Marafiki wa kweli hupenda kusikilizwa.Hata hivyo hutawala mazungumzo kuonyesha kwamba tunafikiri maoni yetu ni bora kuliko ya wengine.Kwa hiyo,sikiliza kwa makini rafiki anapokueleza maoni yake ya moyoni na mahangaiko yake.Pia,usikasirike akikuambia ukweli.Yak 1:19,Mith 27:6.

 c.Usitazamie mengi mno.

Kadri tunavyozidi kuwa karibu na rafiki zetu ndivyo inavyokuwa rahisi kutambua makosa yake.Kama sisi,rafiki zetu sio waaminifu,hatupaswi utakatifu kutoka  kwa rafiki zetu.Badala yake ni vizuri kupendezwa na sifa nzuri na kutokazia fikira makosa yao.Mara nyingi tunadai mengi kutoka kwa wengine kuliko yale tunayowaza kutimiza.Tukitambua makosa yetu na kwamba tunahitaji kusamehewa,itakuwa rahisi kuwasamehe wengine.Kubali kwamba rafiki yako atafanya makosa.Matatizo yanapotokea ni vizuri kuyatatua haraka sana na kujitahidi kuyasahau. Yak 3:2,Ebr 3:13-14. Kilosai 3:13-14.

 d.Uwe na marafiki wa aina mbalimbali.

Ni kweli kwamba tunahitaji kuchagua marafiki wetu kwa uangalifu.Lakini haimaanishi kwamba tunapashwa tu kuwa na marafiki wa umri fulani au malezi kama yetu.Kupendezwa na watu wa umri,na malezi,na mataifa mbalimbali inaweza kuboresha maisha yetu.Kuwa na marafiki wa umri na yatupendezayo ni sawa na kuvaa nguo za ringi moja unayoipenda kila siku.Hata kama iwe unaipenda rangi hiyo kiasi gani mwishowe itakuchosha.Kuwa na marafiki wa aina mbalimbali kutatusaidia kuwa watu wakomavu.Nimejifunza kuishi na watu wa umri na malezi mbalimbali,na hilo limenifanya niweze kushugulika na watu na hali tofauti-tofauti.Rafiki zangu wanapendeza na hilo.2Kor 6:13.

Kwa Nini Sina Marafiki?.

Kama ukiwa mtandaoni na unaona picha za tafrija iliyofanywa hivi karibuni.Na marafiki zako wote wakaonekana kwenye picha hizo na wana furaha sana.Lakini kuna kitu ambacho kimekosekana au tuseme mtu fulani amekosekana,na mtu huyo ni wewe.Udadisi wako utakufanya uanze kuhisi uchungu.Unahisi umesahaulika.Ni kana kwamba mahusiano yako yote yameyeyuka mara moja kama ukungu.Umeelemewa na upweke,na kujiuliza,kwa nini sina marafiki?.kuwa na marafiki wengi hakumaanishi kuwa hutahisi upweke.Unaweza kuwa na hali hii na kusema ninawajali marafiki zangu,lakini wakati mwingine sidhani kama wananijali kama Ninavyowajali.Unaweza kuwa mpweke  sana unapozungukwa na marafiki ambao hawaonyeshi kuwa wanakupenda au wanakujali.Kujiunga na mitandao ya kijamii hakumaanishi kwamba umetengana na upweke.Watu wengi wana jikusanyia marafiki kama vile vinyango na kuvihifadhi.Lakini kujirundikia vinyango vingi hakumfanyi mtu ajihisi kwamba anapendwa.Ikiwa huna marafiki wanaokuona ukiwa muhimu maishani mwao,marafiki unaokutana  nao mitandao watakuwa tu kama vinyago visivyo na uhai.Kuwatumia watu ujumbe mfupi kwa wingi kadri uwezavyo hakumaanishi kuwa hutawahi kuwa mpweke.Nyakati nyingine unapokuwa mpweke unaangalia simu yako kila mara ili uone ikiwa Kuna rafiki yeyote amekutumia ujumbe.Na unapotambua hakuna aliyejaribu kuwasiliana nawe hilo linakufanya ujihisi mpweke hata zaidi.Kuwasaidia wengine hakumaanishi kuwa hutawahi kuhisi upweke.Siku zote nimejitahidi kuwaonyesha marafiki zangu ukarimu,lakini inanishangaza kwamba hajawahi kunitendea kwa fadhila kama ninavyowatendea.

Unaweza kufanya nini ikiwa unajihisi mpweke na huna marafiki?.

a.Jitahidi  Kustawisha Sifa Ya Kujiamini Unapokuwa Huna Marafiki.

Hali ya kutojiamini inaweza kukufanya uwe mpweke.Ni vigumu kuanzisha na wengine hasa unapojihisi  kwamba hustahili kupendwa na wengine.Gal 5:14,6:3-4

b.Epuka Kujisikitikia Unapokuwa Huna Marafiki.

Mtu mpweke ni kama aliye katika dibwi lenye matope mengi.Mtu huyo anapokanyaga matope hayo ndiyo anavyozidi kudidimia.Ukiruhusu upweke utawale mawazo yako,punde si punde watu watakuepuka na utazidi kuwa mpweke zaidi na zaidi. 1Kor 13:4-5,2Kor 12:15,

 c.Usishushe Viwango Vyako Ili Kupata Marafiki.

Watu wapweke hupenda sana kuonyesha urafiki,na wanaweza kufikia hatua ambayo hawajali Ni nani anayewaonyesha urafiki.Wanataka Kuridhisha hisia zao kwamba mtu fulani anawajali.Lakini watu wangine watakutendea kana kwamba wanakujali kisha wakutumie vibaya.halafu utajihisi mpweke zaidi na zaidi. Mith 13:20). Kila mtu huwa mpweke wakati fulani;na watu fulani huhisi upweke zaidi kuliko wengine.Ijapokuwa hisia za upweke zinaweza kumletea mtu matokeo mabaya,ukweli wa mambo ni kwamba sikuzote zitabaki kuwa hisia tu.Chanzo cha hisia zetu ni mawazo yetu,na tunaweza kudhibiti mawazo yetu.Pia usitarajie mengi kutoka kwa wengine.Si kila mtu atakuwa rafiki wa karibu milele.

 9.Marafiki Wangu Wa Kweli Ni Nani?.

Cori,amenifunza Mambo mengi sana ambayo sikujua.Tunapokuwa pamoja,mimi huanzisha urafiki na watu wengine wapya,ninajifunza kufanya mambo mabaya,nami hufurahia chochote tunachofanya pamoja.Kwa kweli urafiki wangu na Cori,umebadirisha kabisa maisha yangu.Je, unahisi kwamba haiwezekani kwa na marafiki wa aina hiyo?.Ikiwa ndivyo usivujike moyo.Umezugukwa na watu ambo wanaoweza kuwa rafiki zako.Mbinu hizi zitakusaidia kuwatambua.

 a.Rafiki Wa Kweli Anategemeka

Rafiki wa kweli humwambia rafiki yake Siri zake,na hiyo nitafikiria kwamba ninaweza kumtumainia kwamba atatunza siri zangu pia. Kwa hiyo siku moja nikamwambia kwamba ninafutiwa na kijana fulani.Kumbe nilikuwa nimefanya kosa kubwa sana!mara moja alieneza habari hiyo mtaani kwetu.Rafiki wa kweli anaweza kuambiwa kilajambo la siri na hawezi kumwambia mtu au watu wengine.Mith 17:17.

 b.Rafiki Wa Kweli Hujidhabihu

Pindi fulani katika urafiki wowote,mtu mmoja huwa mwenye nguvu zaidi kuliko yule mwingine.Rafiki wa kweli hutambua anapokuwa dhaifu na mara moja anakusaidia.Kwa kweli rafiki huyo anatumainiwa kwamba atafanya vivyo hivyo pia anapohitaji msaada.Mama yangu alipokufa,nilikuwa na rafiki mpya.Bado hatukuwa na uhusiano wa karibu sana lakini tulikuwa tumepanga kuhudhuria harusi fulani pamoja.Lakini ikawa kwamba siku ambayo hotuba ya mazishi ya mama yangu ilikuwa itolewe na siku hiyo ndio Ilikuwa siku ya harusi hiyo.Nilishangaa sana kumwona rafiki yangu kwenye hotuba ya mazishi badala ya kwenda kwenye harusi.Hapo ndipo nilipojua kwamba alikuwa rafiki yangu wa kweli.Ni Nani  kati ya rafiki zako ambaye huonyesha roho ya kujidhabihu?.Rafiki wa kweli ataendelea kutafuta,si faida yake mwenyewe,bali ya yule mtu mwingine.1Kor 10:24.

 c.Rafiki Wa Kweli Uboresha Utu.

Watu fulani hutazamia niwe mshikamanifu kwao na nikubali maoni yao hata kama kufanya hivyo kutamaanisha kutenda kinyume na viwango vyangu na hata kupuuza  dhamiri yangu.Hao sio marafiki wa kweli.Dada yangu ndie rafiki yangu wa karibu zaidi.Yeye hunisukuma nifanye Mambo ambayo ninaona kuwa magumu,naye hunisaidia niwe mwenye urafiki zaidi.Yeye uniambia ukweli wa Mambo hata kama hayanifurahishi.Rafiki yako hukusaidia kufikia miradi yako. Mith 13:30. Naamini umefahamu mengi kuhusu urafiki au marafiki.Kwa zaidi utafahamu kupitia sifa kuu nne za upendo wa kirafiki.Na Mungu akubariki sana.


Kimeandaliwa na kuandikwa na

Bishop:Rhobinson S.Baiye

rhobinsons.blogspot.com

rhobinsonsaleh1@mail.com

Whatsapp: 0764127531

Mwanza Tanzania.

 

 


No comments:

Post a Comment

UONGOZI BORA WA KIROHO

Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...