Mbinu za kuwa rafiki mzuri.
Mnamo
Desemba 25,2010, kabla ya mwanamke fulani mwenye umri wa miaka 42)Kujiua
aliandika ujumbe kwenye tuvuti ya kijamii.Ujumbe wake ulikuwa kilio chakuomba
msaada Ingawa alikuwa na marafiki zaidi ya elfu moja kwenye mtandao,Hakuna hata
mmoja aliyemsaidia.Siku moja baadaye,polisi walimpata akiwa amekufa.Alijiua kwa
kumeza dawa nyingi kupita kiasi.Leo kupitia teknolojia tumeweza kupata mamia au
maelfu ya marafiki kwenye mitandao ya kijamii kwa kuongeza tu majina yao kwenye
orodha yetu ya anwani katika
kompyuta.Pia tukitaka kukatisha urafiki na yeyote kati yao tunafuta tu,jina lake kutoka kwenye
orodha yetu.Hata hivyo msiba uliotajwa mwanzoni kuhusu yule mwanamke huko
Uingereza unakazia ukweli muhimu,watu wengi hawana marafiki wa kweli.Utafiti
mmoja wa hivi karibuni unaonyesha kwamba ingawa watu wanawasiliana sana,idadi
ya marafiki wa kweli imepungua.Bila shaka,kama watu wengi wanakubali kwamba ni
muhimu kuwa na marafiki wa kweli.Huenda pia umetambua kwamba urafiki unahusisha
mengi kuliko kuongeza majina kwenye orodha ya kompyuta au simu yako.Rafiki wa
kweli anapaswa kuwa na sifa zipi?.Je unaweza kuwa rafiki mzuri? Ni mambo gani
yanayohitajika ili kupata marafiki wa kudumu?
a.Wajali wengine kweli
kweli.
Urafiki wa kweli unahusisha vitendo.Kwa maneno mengine,rafiki mzuri anajua majukumu yake,na ni mwenye kujali.Kwa kweli urafiki unahusisha pande mbili,na kila mmoja anapaswa kutimiza sehemu yake.Lakini kuna faida ya kufanya hivyo.Lakufanya ni kujiuliza kwamba uko tayari kujitolea kutumia muda na mali zako kwa ajili ya rafiki yako?Kumbuka kwamba ili upate rafiki mzuri wewe mwenyewe unapaswa kuwa na
Urafiki wa kweli hauwezi kustawi bila mawasiliano ya kawaida.Kwa hiyo,zungumzeni mambo yanayowapendeza.Msikilize rafiki yako na uheshimu maoni yake.Ikiwezekana, mpongeze na umtie moyo.Nyakati nyingine,rafiki atahitaji ushauri au hata kurekebishwa,na huenda isiwe rahisi kufanya hivyo.Hata hivyo rafiki mshikamanifu anajua jinsi ya kumkosoa mwenzake na kutoa ushauri kwa busara.Rafiki wa kweli anapaswa kujieleza kwa uhuru na asikasirike,na asipokubaliana na maoni yangu.Mimi namthamini sana marafiki zangu ambao wako tayari kutumia muda pamoja nami na kunisikiliza,hasa ninapokuwa na matatizo.Na marafiki zangu hao ni kama wafuatao.Saleh wa Saleh,Yusuph Sabato,Didas Malango,Sebastiano Kabeza.Mmalabwe Byondo.Ogi Byondo.Marafiki wa kweli watakuambia ukweli hata kama wanajua kwamba utaumia kwa sababu wanakujali.Marafiki wa kweli hupenda kusikilizwa.Hata hivyo hutawala mazungumzo kuonyesha kwamba tunafikiri maoni yetu ni bora kuliko ya wengine.Kwa hiyo,sikiliza kwa makini rafiki anapokueleza maoni yake ya moyoni na mahangaiko yake.Pia,usikasirike akikuambia ukweli.Yak 1:19,Mith 27:6.
Kadri
tunavyozidi kuwa karibu na rafiki zetu ndivyo inavyokuwa rahisi kutambua makosa
yake.Kama sisi,rafiki zetu sio waaminifu,hatupaswi utakatifu kutoka kwa rafiki zetu.Badala yake ni vizuri
kupendezwa na sifa nzuri na kutokazia fikira makosa yao.Mara nyingi tunadai
mengi kutoka kwa wengine kuliko yale tunayowaza kutimiza.Tukitambua makosa yetu
na kwamba tunahitaji kusamehewa,itakuwa rahisi kuwasamehe wengine.Kubali kwamba
rafiki yako atafanya makosa.Matatizo yanapotokea ni vizuri kuyatatua haraka
sana na kujitahidi kuyasahau. Yak 3:2,Ebr 3:13-14. Kilosai 3:13-14.
Ni kweli kwamba tunahitaji kuchagua marafiki wetu kwa uangalifu.Lakini haimaanishi kwamba tunapashwa tu kuwa na marafiki wa umri fulani au malezi kama yetu.Kupendezwa na watu wa umri,na malezi,na mataifa mbalimbali inaweza kuboresha maisha yetu.Kuwa na marafiki wa umri na yatupendezayo ni sawa na kuvaa nguo za ringi moja unayoipenda kila siku.Hata kama iwe unaipenda rangi hiyo kiasi gani mwishowe itakuchosha.Kuwa na marafiki wa aina mbalimbali kutatusaidia kuwa watu wakomavu.Nimejifunza kuishi na watu wa umri na malezi mbalimbali,na hilo limenifanya niweze kushugulika na watu na hali tofauti-tofauti.Rafiki zangu wanapendeza na hilo.2Kor 6:13.
Kwa Nini Sina Marafiki?.
Kama
ukiwa mtandaoni na unaona picha za tafrija iliyofanywa hivi karibuni.Na
marafiki zako wote wakaonekana kwenye picha hizo na wana furaha sana.Lakini
kuna kitu ambacho kimekosekana au tuseme mtu fulani amekosekana,na mtu huyo ni
wewe.Udadisi wako utakufanya uanze kuhisi uchungu.Unahisi umesahaulika.Ni kana
kwamba mahusiano yako yote yameyeyuka mara moja kama ukungu.Umeelemewa na
upweke,na kujiuliza,kwa nini sina marafiki?.kuwa na marafiki wengi hakumaanishi
kuwa hutahisi upweke.Unaweza kuwa na hali hii na kusema ninawajali marafiki
zangu,lakini wakati mwingine sidhani kama wananijali kama Ninavyowajali.Unaweza
kuwa mpweke sana unapozungukwa na
marafiki ambao hawaonyeshi kuwa wanakupenda au wanakujali.Kujiunga na mitandao
ya kijamii hakumaanishi kwamba umetengana na upweke.Watu wengi wana jikusanyia
marafiki kama vile vinyango na kuvihifadhi.Lakini kujirundikia vinyango vingi
hakumfanyi mtu ajihisi kwamba anapendwa.Ikiwa huna marafiki wanaokuona ukiwa
muhimu maishani mwao,marafiki unaokutana
nao mitandao watakuwa tu kama vinyago visivyo na uhai.Kuwatumia watu
ujumbe mfupi kwa wingi kadri uwezavyo hakumaanishi kuwa hutawahi kuwa
mpweke.Nyakati nyingine unapokuwa mpweke unaangalia simu yako kila mara ili
uone ikiwa Kuna rafiki yeyote amekutumia ujumbe.Na unapotambua hakuna
aliyejaribu kuwasiliana nawe hilo linakufanya ujihisi mpweke hata
zaidi.Kuwasaidia wengine hakumaanishi kuwa hutawahi kuhisi upweke.Siku zote
nimejitahidi kuwaonyesha marafiki zangu ukarimu,lakini inanishangaza kwamba
hajawahi kunitendea kwa fadhila kama ninavyowatendea.
Unaweza kufanya nini ikiwa unajihisi mpweke na huna marafiki?.
a.Jitahidi Kustawisha Sifa Ya Kujiamini Unapokuwa Huna Marafiki.
Hali
ya kutojiamini inaweza kukufanya uwe mpweke.Ni vigumu kuanzisha na wengine hasa
unapojihisi kwamba hustahili kupendwa na
wengine.Gal 5:14,6:3-4
b.Epuka Kujisikitikia Unapokuwa Huna Marafiki.
Mtu
mpweke ni kama aliye katika dibwi lenye matope mengi.Mtu huyo anapokanyaga
matope hayo ndiyo anavyozidi kudidimia.Ukiruhusu upweke utawale mawazo
yako,punde si punde watu watakuepuka na utazidi kuwa mpweke zaidi na zaidi.
1Kor 13:4-5,2Kor 12:15,
Watu wapweke hupenda sana kuonyesha urafiki,na wanaweza kufikia hatua ambayo hawajali Ni nani anayewaonyesha urafiki.Wanataka Kuridhisha hisia zao kwamba mtu fulani anawajali.Lakini watu wangine watakutendea kana kwamba wanakujali kisha wakutumie vibaya.halafu utajihisi mpweke zaidi na zaidi. Mith 13:20). Kila mtu huwa mpweke wakati fulani;na watu fulani huhisi upweke zaidi kuliko wengine.Ijapokuwa hisia za upweke zinaweza kumletea mtu matokeo mabaya,ukweli wa mambo ni kwamba sikuzote zitabaki kuwa hisia tu.Chanzo cha hisia zetu ni mawazo yetu,na tunaweza kudhibiti mawazo yetu.Pia usitarajie mengi kutoka kwa wengine.Si kila mtu atakuwa rafiki wa karibu milele.
Cori,amenifunza
Mambo mengi sana ambayo sikujua.Tunapokuwa pamoja,mimi huanzisha urafiki na
watu wengine wapya,ninajifunza kufanya mambo mabaya,nami hufurahia chochote
tunachofanya pamoja.Kwa kweli urafiki wangu na Cori,umebadirisha kabisa maisha
yangu.Je, unahisi kwamba haiwezekani kwa na marafiki wa aina hiyo?.Ikiwa ndivyo
usivujike moyo.Umezugukwa na watu ambo wanaoweza kuwa rafiki zako.Mbinu hizi
zitakusaidia kuwatambua.
Rafiki
wa kweli humwambia rafiki yake Siri zake,na hiyo nitafikiria kwamba ninaweza
kumtumainia kwamba atatunza siri zangu pia. Kwa hiyo siku moja nikamwambia
kwamba ninafutiwa na kijana fulani.Kumbe nilikuwa nimefanya kosa kubwa
sana!mara moja alieneza habari hiyo mtaani kwetu.Rafiki wa kweli anaweza kuambiwa
kilajambo la siri na hawezi kumwambia mtu au watu wengine.Mith 17:17.
Pindi
fulani katika urafiki wowote,mtu mmoja huwa mwenye nguvu zaidi kuliko yule
mwingine.Rafiki wa kweli hutambua anapokuwa dhaifu na mara moja anakusaidia.Kwa
kweli rafiki huyo anatumainiwa kwamba atafanya vivyo hivyo pia anapohitaji
msaada.Mama yangu alipokufa,nilikuwa na rafiki mpya.Bado hatukuwa na uhusiano
wa karibu sana lakini tulikuwa tumepanga kuhudhuria harusi fulani pamoja.Lakini
ikawa kwamba siku ambayo hotuba ya mazishi ya mama yangu ilikuwa itolewe na
siku hiyo ndio Ilikuwa siku ya harusi hiyo.Nilishangaa sana kumwona rafiki
yangu kwenye hotuba ya mazishi badala ya kwenda kwenye harusi.Hapo ndipo
nilipojua kwamba alikuwa rafiki yangu wa kweli.Ni Nani kati ya rafiki zako ambaye huonyesha roho ya
kujidhabihu?.Rafiki wa kweli ataendelea kutafuta,si faida yake mwenyewe,bali ya
yule mtu mwingine.1Kor 10:24.
Watu
fulani hutazamia niwe mshikamanifu kwao na nikubali maoni yao hata kama kufanya
hivyo kutamaanisha kutenda kinyume na viwango vyangu na hata kupuuza dhamiri yangu.Hao sio marafiki wa kweli.Dada
yangu ndie rafiki yangu wa karibu zaidi.Yeye hunisukuma nifanye Mambo ambayo
ninaona kuwa magumu,naye hunisaidia niwe mwenye urafiki zaidi.Yeye uniambia
ukweli wa Mambo hata kama hayanifurahishi.Rafiki yako hukusaidia kufikia miradi
yako. Mith 13:30. Naamini umefahamu mengi kuhusu urafiki au
marafiki.Kwa zaidi utafahamu kupitia sifa kuu nne za upendo wa kirafiki.Na Mungu akubariki sana.
Kimeandaliwa na kuandikwa na
Bishop:Rhobinson S.Baiye
rhobinsons.blogspot.com
rhobinsonsaleh1@mail.com
Whatsapp: 0764127531
Mwanza Tanzania.
No comments:
Post a Comment