Monday, June 1, 2020

MAOMBI YANAYOJIBIWA

 

MAOMBI YANAYOJIBIWA

Ndungu msomaji naamini unashauku ya kufahamu mengi kihusu maombi.Lakini katika kitabu hiki tutajikita katika mada hii isemayo maombi yanayojibiwa.Kwa maana watu wengi huomba lakini hawapati majibu ya yale wanayo ya omba, na hilo huleta maswali mengi katika ucha-Mungu wao na utumishi wao.Na walio wengi usema na kujiuliza je,kweli Mungu anajibu maombi ya watu? Ni kweli Mungu hujibu maombi kupitia jina la Yesu Kristo.Yohana 14:13-14. Na hivi karibuni tutatafakari kuhusu maoombi yasiojibiwa kaa mkao wa kupokea.Lakini fahamu kwamba kuna aina nyingi za maombi.

Maama Ya Maombi

Maombi ni mazungumzo yenyemahitaji muhimu kati ya mtu na Mungu au kati ya Mungu na mtu.Mwanzo 1830-33,45-1-20

5.Namna Ya Mungu Kujibu maombi

Mungu wetu na Bwana wetu Yesu Kristo wametujenga  kwa hadi ya kupokea majibu chanya ya maombi mahitaji yetu kutoka kwao,kama tuliwakilisha mahitaji yetu kulingana na utaratibu wa ki-Mungu majibu ya maombi hujibiwa.Lakini nakuomba ufahamu kwamba mara nyingine  Mungu atakupa kitu au vitu vizuri tofauti na ulivyotarajia.Inawezekana ukaomba Mungu kwa kitu unachofikiria ya kuwa ni kitu kizuri ambacho kitakacho mtukuza Mungu,lakini yeye ni Mungu ajuaye kila jambo,anafahamu kile uombacho kitaumiza kiasi gani kazi zake na hata sisi vilevile.Mungu hupenda sisi watoto wake na anajua muda na kitu fulani cha kutupatia kilicho kizuri kitakacho kuwa baraka kwetu na kumtukuza Mungu.Mara nyingi hujibu maombi yetu si kwa kadri tulivyohitaji lakini kwa njia bora kuliko yale tuliyoyaomba.Tunaweza kuona jambo hili kwa baadhi ya watumishi wake.Paulo alikuwa na udhaifu mwilini mwake ambao ulimtesa sana.Na alifikiri udhaifu huu ulikuwa kikwazo katika huduma yake,na aliomba mara tatu Ili udhaifu huu umtoke.bali Bwana hakuruhusu udhaifu huu kumtoka Paulo haijalishi aliomba.Bali Mungu alimjibu Paulo kwamba neema yake Mungu inamtosha.Na hapo Paulo alibadilisha maombi na akaanza kushukuru Mungu kwa udhaifu huo.2Kor 12:7.Mara nyingi Mungu hatuondoi katika taabu yetu wakati tunapomwomba kufanya hayo.Halafu hutupa nguvu za kumtukuza hata tukiwa katika taabu yenyewe.Na tunamshukuru katika mambo yote.

1.Kwa ahadi.Isaya 58:9.Yer 29:12.Math 7:7

2.Mara kwa ghafla. Dan 9:21,23.10:12

3.Kwa baadae Luk 18:7.1Fal 18:42-44.Dan 10:12

4.Kwa hali usiyoitegemea.2Kor 12:8-9

5.Vyema kuliko tegemeo letu au kuliko tulivyofikiria.Yer 33:3 Efe 3:20.

Ilimaombi yako yajibiwe Fanya Yafuatayo.

Kwakuwa kanisa na mtu binafsi hupenda kupata majibu chanya ya Maombi yao waliyo wakilisha mbele za Mungu, ni vyema maombi yaombwe katika utaratibu huu.

1.Omba Kupitia Jina La Yesu Kristo.

2.Omba Kwa Imani Na Matumaini

3.Omba Kwa Kumaanisha.

4.Omba Kwa Wakati Uliokubalika.

5.Omba Kwa Utaratibu.

Mungu wetu niwautaratibu,kwahiyo mambo yote yatendeka kwa uzuri na kwa utaratibu ukiwemo utaratibu wa kuomba.

1.Omba  Katika Jina Langu

Yatupasa kuomba katika jina la Yesu Kristo.Hilo nitakwa la Yesu Kristo mwenyewe.Yohana 11:13.14:13-16.15:7,16.16:24-26.Tukiomba  katika jina la Yesu Kristo  tutampendeza Mungu na Kristo pia.Unaweza kujiuliza kuomba katika jina la Yesu humaanisha nini?.Kuomba katika jina la Yesu Kristo lina maana ya kuomba kwa kutamka maneno yanayopatana na mapenzi yake.Ukitamka au ukisema neno au maneno kupitia kwa jina lingine maombi hayo hayawezi kumfikia Mungu kwa kuwa Yesu Kristo ndiye njia ya kweli na uzima.Ifahamike kwamba tunayemwomba atutimizie mahitaji yetu ni Mungu lakini yatupasa maombi yetu yapitie katika jina la Yesu Kristo wala si vinginevyo.Kuna baadhi ya Madhehebu ya ki-kristo yamebuni majina mengine na kuyapa heshima ambayo hayastahili kupewa heshima hiyo,kwa maana hata majina hayo hayajatajwa na Biblia kwa heshima hiyo wana jifariji na kudanganya nafsi zao wenyewe. Kwa mfano heshima ya kupindukia kwa Bikira Mariamu,pamoja na watakatifu ambao wana watakasa wao hayo yote ni kujidanganya na kujifariji.Atambuae na kumtakasa mtu ni mtu mwenyewe na Mungu tu.

2.Omba Kwa Imani Na Matumaini.

Walio wenye haki wataishi kwa imani na matumaini.Mark 9:23.Math 17:20.Ebr 11:1,6.1Kor 2:4-7,8-16.2Kor 5:7.Ebr 12:2.Rum 1:17.Habakuki  2:4.Efe 2:8-9.Rum 10:17.Yak 1:22-25.Inatupasa kuomba kwa imani na matumaini makubwa ya kupokea kile tulicho kiomba kwa Baba.Baadhi ya wacha Mungu wanaomba lakini wana imani haba na hupoteza matumaini.

1.Omba Kwa Imani

Tunaweza kusema kwamba imani ni njia ya kupokea kutoka kwake Mungu.katika waefeso  tunaona kwamba tumeokolewa kwa neema,kwa njia ya imani,Efe 2:8-9.Ebr 11:1,6.Tunaweza kueleza maana ya imani kwa njia tofauti lakini inamaanisha kuwa njia rahisi ya kutazama imani na hata kujichunguza  kuona kama tuna imani yenye nia na matumaini ya upokeaji.Tukitathimini mioyo yetu ni shughuli muhimu wakati tunapoanza safari hii ya matumaini pamoja,kwa sababu kumtumainia Mungu na kuwa na matarajio mazuri yanaleta uhusiano wa karibu sana na imani.Tunaweza kusema kwamba kiwango chako cha matarajio ndicho ndicho kiwango chako cha imani.Nionyeshe mtu mwenye matarajio madogo,nami nitakuonyesha mtu anayetumia imani haba.Tena ionyeshe mtu mwenye matarajio makubwa  na nitakuonyesha mtu anayetumia imani kubwa ya kijasiri.Kumbuka tunaongea kuhusu kuwa na matarajio yetu katika Mungu.Hiyo ni zaidi ya kuwa na mtazamo chanya;ni kumtegemea Mungu akutunze  pamoja kila na kitu kinacho kuhusu.Neno la Mungu linatwambia kwamba imani yetu matarajio yetu chanya,yenye matumaini humpendeza Mungu.Ebr 11:6.na mara kadhaa katika Injili tunamwona Yesu akichochewa kutenda jambo kwa sababu ya imani na matarajio ya wale aliokutana nao.Math 9:29,Marko 5:34,Luk 7:50.Mungu yuko upande wako na ana mpango mzuri katika maisha yako.Unapojaribiwa na kuwa mwenye mashaka,na kukaribia kukata tama na kukaribia kufa moyo wewe amini na kuwa na matarajio ya kupokea.Utafaulu kulingana na kiwango chako cha matarajio.Usichukulie kuwa kule ulikotoka na hapo ulipo,kwamba hapawezi kubadilika.Si kwamba mpango wako ni mbaya zaidi la hasha bali ni kwamba mpango wa Mungu ni mzuri zaidi.Kwa hiyo omba kwa imani kubwa sana,utapokea.Mungu hufanya zaidi ya kukushikilia usianguke;na kisha hukupeleka juu zaidi ya pale ulipokuwa mwanzoni.

2.Omba Kwa Matumaini

Mara kwa mara waliowengi huhisi kuwa mtu akitarajia zaidi ya alivyo navyo basi huyo ni mlafi na mkosaji.Ijapokuwa ni kweli kwamba wakati wote tunapaswa kuridhika na kutosheka na vile tulivyonavyo.Hivyo haimaanishi kuwa kuhitaji kuwa na vitu vizuri zaidi ni dhambi au makosa ilimradi tuna sababu mzuri ya kuvitamani na  kuvitumia.Tunaweza kutosheka na huku bado tunahitaji kuwa na vingi zaidi.Mimi Bishop Rhobinson Saleh Baiye sasa hivi ninatosheka sana na kila kitu katika maisha yangu kwa sababu ninaamini wakati wa Mungu maishani mwangu ndiyo mzuri zaidi.Ninaweza kufurahi hata kama sina kitu chochote cha ziada kwa sababu furaha yangu na kutosheka kwangu viko katika Kristo.Hata hivyo,wakati huo huo ninahitaji kuwa na vingi vizuri zaidi kwa sababu ninahitaji kuendelea katika maisha kadri Mungu atakavyoniruhusu na nimfanyie mengi zaidi isipokuwa maisha mazuri zaidi ambayo Mungu anakata kunipa.

Ezekieli 37:11,Isaya 57:10,32:17,20:5,29:16,1Kor 9:10

3.Omba Kwa Kumaanisha.

Walio wengi wanaomba sala na dua ndefu pasipo kumaanisha wanachohitaji.Ni vyema kufahamu tunapoomba kumaanisha kile tunachohitaji.kwahiyo tamka kwa ufasaha kile unachohitaji.1Timoth 2:1-4.Luk 10:2.1The 3:1.Mark 8:22-23.10:46-52(50-52) walio wengi huogopa kuomba baadhi ya mahitaji yao muhimu.lakini fahamu ya kwamba Yesu alisemaje kuhusu kuomba kwetu? Yesu alikuwa akiwauliza baadhi ya watu waliyo mwendea na kusema wataka nikutendee nini? Alikuwa akihitaji musika amaanishe kile anachohitaji kutoka kwake Krsto.Sikiliza jinsi Yesu Kristo alivyo tufundisha kuomba kwa kumaanisha kweli kweli.Ikiwa Yesu Kristo alipokuwa mahali fulani akiomba,alipokwisha,kuomba mmoja katika wanafunzi wake alimwambia,Bwana tufundishe kuomba kama vile Yohana alivyo wafundisha wanafinzi wake.Yesu Kristo akawaambia msalipo semeni hivi,Baba yetu uliye mbinguni jina lako litukuzwe,Ufalme wako uje,[Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni.] utupe siku kwa siku riziki yetu.Utusamehe dhambi zetu,kwa kuwa sisi nasi tuna wasamehe waliyotukosea.Na usitutie majaribuni lakini utuokoe na Yule mwovu kwa kuwa ufalme na nguvu na utukufu ni wako hata milele amina.

Ukifanya uchambuzi  na kutafakari kwa makini,utagundu

a kwamba Yesu Kristo aliwafundisha jinsi ya kuomba kwa kumaanisha , kile unachokiomba na kwa Yule unaye mwomba,na kwa muda unaohitaji.Haijalishi Mungu anajibu na kufanya kwa muda wake,cha muhimu ni wewe kumaanisha kile ukiombacho na kwa Yule umwombaye.Wewe omba kwa maana Yesu Kristo alisema kwamba tutafanyiwa kila tunacho kiomba kwa jina lake ili Baba Mungu atukuzwe na ndani ya Mwana.Yohana 14:13.

Kama  unahitaji chakula wewe omba Mungu kwa kumaanisha Mungu baba nakuomba chakula baba yangu na ni vema kumaanisha chakula unachohitaji si kwamba tu umetamka chakula fahamu kuna aina nyingi za vyakula hapa duniani,waweze kutaja baadhi ya vyakula unavyovifahamu utaona na kujua ni aina nyingi tu.wewe maanisha kila unachohitaji kutoka kwa Mungu kupitia jina la Yesu Kristo wa nazareti.Zaburi 40:8.Math 6:33

Maanisha kuomba msamaha kwa maana tunasamehewa kwa kuwa tuna wasamehe wengine.Yesu Kristo alisema wazi kwa kumaanisha kabisa ya kwamba tutasamehewa tukiwasamehe wengine.Maanisha kuutukuza utukufu wa Mungu katika kuomba kwako.Kama unahitaji kuponywa magojwa maanisha,kama unahitaji utajiri maanisha ,kam,

Unahitaji mifugo,magari,mashamba,kama unahitaji kuwekeza majini maanisha,maanisha chochote unachohitaji mungu atakutimizia.Usiombe kwa kumungunya maneno tamka na kumaanisha.

4.Omba Kwa Wakati Unao kubalika

Omba kwa wakati unaokubalika na Mungu.sio kilamuda ni wakuomba,tafuta muda wakuomba,hasa muda ambao dhamiri zako zinahitaji kuomba.Mara nyingi baadhi ya wakristo hujiuliza kama ni vyema kuomba mara kwa mara? au inampasa kuomba mara ngapi kwa siku au kwa wiki au kwa mwezi au kwa mwaka? Kwa nini umeupa moyo wako kujiuliza swali kama hilo? Je hujiamini unapo mwendea Mungu? Je wewe umechoka kulalama mbele za Mungu ?Biblia inasemaje kuhusu kuomba kwetu. Omba bila kukoma.Ni kweli kwamba kuna watu huwa wanachoka haraka wakati tunapoomba au tunapowasilisha mahitaji yetu mbele za Mungu.Na tena hujihisi kwamba wameomba vitu vingi au wameomba mara nyingi.Si hivyo alivyo Mungu wetu,anapoona na kusikia maombi yetu mara nyingi anafurahi sana kuona tunamtegemea na kuwa wahitaji kwake.Kwa sababu Mungu wetu ni wautaratibu basi yatupasa kuwa na utaratibu katika kuomba kwetu.Danieli,aliomba mara tatu kwa siku Dan 6:10.Daudi,aliomba mara tatu  Zaburi 55:17. Bwana wetu Yesu Kristo alisema ya kwamba yatupasa kuomba siku zote.Luka 18:1Katika 1Th 5:17 Tumeagizwa kuomba bili kukoma hapo tunahimizwa kuomba muda wowote na uombe kwa mahitaji yako mwenyewe na watu wengi vilevile.Maandiko yanasema tudumu katika kuomba Kolosai 4:2

1.Omba Asubui

2.Omba Mchana.

3.Omba Jioni.          Danieli 6:10

4.Omba Usiku         Zaburi 55:17.

5.Omba Kwa Utaratibu.

Fahamu unapoomba unamfanyia Mumgu ibada.Unapokuwa katika ibada ya maombi na maombezi fata utaratibu wa Mungu.Kuna baadhi ya wanaojiita waombaji lakini ukiwasikia wanavyoomba hawana mpangilio wa kuomba kwao.yanayofaa kutangulia kutamkwa yanatamkwa mwishoni mwa mazungumzo.Yale ambayo yangetamkwa mwishoni yanatamkwa mwanzoni mwa mazungumzo yao na Mungu.Mungu wetu aliumba kwa kuweka mambo yake katika mpangiliyo na utaratibu uliyotukuka.Mwanzo 1:1-2:1-

1.Tamka Maneno Ya Kumshukuru Mungu.

2.Tamka Maneno Ya Kumsifu Na Kutukuza Mungu.Tamka Maneno Ya Toba Na Kuomba Msamaha Kwa Mungu.

3.Wakilisha,Mahitaji Omba Unalohitaji Kutendewa.

5.Msikilize Mungu Kwa Kukaa Kimya Kusubiri Majibu.

Tamka Maneno Ya Kumshukuru Mungu

1Th Na mewe na shukrani katika kila hali.Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.Mara baada ya kutuambia katika 1Th 5:17.Tuombe bila kukoma,Mtume Paulo anatuelezea tumshukuru Mungu katika kila jambo.Haijalishi kinachoendelea katika maisha yetu kwa maana hii andiko kusudi la Mungu kwa ajili ya maisha yetu.

Jinsi maombi yanavyopaswa kuwa mtindo wa maisha yetu,ndivyo shukrani zetu zinavyopaswa  kuwa sehemu ya maisha yetu.Kumshukuru Mungu hakupaswi kuwa jambo ambalo tunafanya mara moja kwa siku tunapoketi chini na kujaribu kufikiria mambo yote mema ambayo Mungu ametufanyia hata katika udhaifu wetu.Katika kumwishia Mungu shukrani au kushukuru kwa sababu tunafikiria kuwa Mungu anatuhitaji tufanye.Ni kweli shukrani uendelea kububujika kutoka kwenye moyo ambao umejaa shukrani pamoja na sifa kwa Mungu kwa sababu ya utukufu  wake na matendo yake.tupate kibali cha ushindi na tuhitimu kuweza kupata baraka.Aina ya shukrani ambayo Mungu anahitaji kutoka kwetu ni ile ambayo imechochewa na roho takatifu ndani yetu ambayo inatuvuta kumwelekea Bwana yale tunayohisi katika roho zetu.Zaburi 136:3.

2.Tamka Maneno Ya Kumsifu  Kumtukuza Mungu.

kwa njia yake Basi Yesu yeye,na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima,yaani tunda la midomo iliungamayo jina la lake.Ebr 13:1-.Ufahamu kwamba sifa na ibada.Sifa ni kutamka maneno ambayo yanayorudia mema ambayo Mungu amefanya.Ibada ni namna jinsi na mbinu za uwasilishaji wa mtu mbele za Mungu,Sifa hutambuwa uwepo wa Mungu na utukufu wake,Ni vema kila wakati kutambua na kukiri kwa kulitukuza jina lake katika kuomba kwetu.

3.Tamka Maneno Ya Toba Na Kuomba Msamaha.

Wakati tunapokuwa mbele za Mungu tukiwasilisha mahitaji yetu katika ibada ya maombi,ni vema kutamka maneno ya kuomba msamaha kwa Mungu,kwa maana sisi ni wakosaji muda wowote,lakini Bwana anatufanya upya siku baada ya siku.Lakini hatuwezi kuomba kusamehewa  dhambi na makosa pamoja na madhaifu yetu kama hatujafikiwa na roho ya kupata toba.Toba ni njia ya mtu kutamka maneno ya kusamehewa na Mungu.Md 5:31.Toba ni hatua muhimu ya mwanzo tunayochukua kubapa msamaha wa dhambi na makosa na madhaifu yetu.Md 2:36-38,17:30.Kujihisi na kujisikia kuwa mwenye hatia kuhusiana na dhambi huja kabla ya kutubu.Na mtu atakapotamka maneno ya kutubu na kuomba kusamehewa pasipo kupa tatoba hiyo si toba yenyewe.Hakuna mtu ambaye anayetubu isipokuwa amejisikia kwanza kuwa mwenye dhambi,lakini si wote wanaojisikia wenye hatia hufanya toba ya kweli.Md 24:25.Si hiyo tu kuhuzunishwa na dhambi zako kwa maana watu wengi sana wanasikitika kwa sababu ya matokeo ya dhambi zao au kwa sababu wamekamatwa.Watu wengi husikitika si kwa sababu ya kile walichokikosea bali ni kwa sababu ya adhabu wanayoipokea kutokana. na kushikwa 2Kor7:10.Toba sio tu kujaribu kuwa mtu mzuri,kwa maana watu wengi wanajaribu kwa nguvu zao kuwa watu wazuri kuliko kubadilisha njia zao za maisha.Nguvu yoyote ya kibinafsi ina mizizi ya kujihesabia haki ndani yake,ambayo haikubali hitaji la toba kutoka dhambi.Isaya 64:6.Toba ya kweli haitokani na kuwa wadini sana.Mafarisayo katika Biblia walikuwa watu wa dini sana katika taifa la Israeli katika tabia na desturi na sikukuu za dini lakini bado hawakutubu kwa ajili ya ukosefu wa toba.Mathayo 3:7-10,5:20.Toba ya kweli sit u kuijua kweli.Kuwa na ufahamu wa kiadili kichwani kuhusu kweli si sharti la dhamana kwamba kweli imefanyika kitu hai halisi katika maisha  ya mtu.Kuamini kwa akili na kuamini kwa moyo ni kwa tofauti sana.Rum 10:10.Yakobo 2:19-20.Toba ya kweli ni sikitiko la ndani kwanza ni sikitiko muhimu zaidi ni sikitiko la kweli ya Mungu.Zab 51:1-4,38:8,Kuwa mkweli kuhusu dhambi zako.Zab 32:5,1Yoh 1:9.Ziache dhambi zako.Mat 28:13.Zichukie dhambi,Ebr 1:9,Ezekieli 20:43-44.

Msamaha Takatifu Uliokubalika

Kuomba msamaha ni tabia na hali ya kujikubali kwa mwenye hatia na mwenye dhambi.Lakini la muhimu kujua na kufahamu ni kwamba kuomba msamaha na kusamehewa na kusamehe ni neema kubwa sana katika maisha ya ki-Mungu.Kuna baadhi ya waitwao Wakristo ni wagumu kusamehe na kuomba msamaha kwa Mungu na kwa watu pia.Ndiyo maana nimesema kwamba kusamehe na kusamehewa ni neema ya ajabu sana.Ona jinsi Isaya alivyojihesabia kuwa mwenye dhambi na akasamehewa aloposema ole wangu mimi mwanye midomo michafu na nimekaa katika watu wanye midomo michafu na macho yangu yamemwona Bwana mfalme wa majeshi.Isaya 6:1-7,Yesu mwenyewe alitusamehe bila sisi kuomba kusamehewa.Luka 23:34.ona jinsi neema ilivyo:

Kuomba Msamaha Na Kusamehewa Na Kusamehe.

Kupata nafasi ya kuomba msamaha na kusamehewa na kusamehe ni neema ya ajabu sana.Neema maana ya kawaida inayofahamika ni upendeleo wa Mungu ambao hatukustahili”kwa maneno mengine ingawa tulikuwa wenye dhambi,wenye kustahili hukumu.Mungu alitutazama kwa upendo na akatusamehe.Hata hivyo maana hii ni nusu  tu,pia neema ina maana ya nguvu ya Mungu ya kuwezesha ikiwemo kukuwezesha kupata nguvu na nafasi  na moyo wa kuomba msamaha na kusamehewa na kusamehe.2Th 2:16-17.Neema ya Mungu huwezesha.Efe 1:4-6, 2Kor 5:17,2Petr3:18, Mashujaa wa imani walipewa neema na Mungu.Musa alipewa neema ya kumfikia Farao.ukichunguza maisha ya Musa utaiona neema,Kutoka 3:11-13,4:1-13.Neema katika maisha ya Gideoni.Waamuzi 6:1-24.Neema  katika maisha ya Paulo.Md 15:40.2Kor 11:22-33,12:9

Wakilisha Mahitaji  Omba Unalohitaji Kutendwa.

Wakati unapofanya ibada ya maombi lengo kuu ni kuwa muhitaji mbele za Mungu ili akutimizie yale ambayo umepungukiwa au ambayo hauna kabisa.Watu wengi hawajui jinsi ya kuwakilisha hitaji au mahitaji yao kwa Mungu.Wakati umekaa magotini ili kumwomba Mungu itapendeza kama utaanza na kushukuru,kusifu na kuabudu,kujiwakilisha na kukubali wewe na mwenye dhambi na mkosaji halafu tamka maneno ya kuomba msamaha.Baada ya kujisalimisha omba sasa kile au yale ambayo unahitaji kutendewa na Mungu.Usione aibu wala usiogope kuomba  vitu vingi na vikubwa mno.wewe omba kadri ya uhitaji wako.Fahamu kwamba Mungu mwenyewa ametuita na kusema,Haya njooni,tusemezane asema Bwana.Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana,zitakuwa nyeupe kama theluji,zijapokuwa nyekundu kama bendera,zitakuwa kama sufu.Isaya 1:18.Haya,leteni maneno yenu,asema Bwana;toeni hoja zenye nguvu asema mfalme wa Yakobo.

Msikilize Mungu  Kaa Kimya Kusubiri Majibu.

Ndugu Mkristo na mtumishi wa Mungu wetu.Nakuomba ufahamu kwamba ni vema kumsikia na kumsikiliza Mungu watu muumba mbingu na nchi.Natamani ufahamu kwamba ni vema ukiomba au kuwakilisha mahitaji yako muhimu kwa Mungu wetu si vema kuomba muda wowote bila kumsikiliza Mungu kama amejibu ili usije ukaombe tena kitu au jamba ambalo Mungu amekwisha jibu.Unapoomba chukua muda wa kukaa kimya bila kuomba chochote wala kuimba wala kuomboleza ,wewe nyamaza kimya ili usikie sauti ya Mungu kukuletea majibu ya mahitaji yako.Unapo chukuwa muda wa siku saba ukiomba,unapokamilisha siku saba kama ulivyojipangia kuwa mbele za Mungu kuwakilisha hoja zako zenye nguvu,chukuwa siku tatu au nne za kukaa kimya bila kuomba chochote kwa Mungu kaa kimya kumsikiliza Mungu.Unapoomba kwa muda wa siku 30,chukuwa muda wa siku 7 kukaa kimya ili kusubiri majibu yako kutoka Mungu.Waliyo wengi hupishana na majibu yao kutoka kwa Mungu kwa sababu ya kutokujua umuhimu wa kukaa kimya huku ukimsikiliza Mungu kutokana na yale uliyoyawasilisha kwake kama ameyajibu.Ukigundua kwamba ameyajibu basi hauna  ya kuyaomba tena kwa maana amekwisha tenda kama ulivyo yahitaji.kukaa kimya kunakupa nafasi ya kuona kusikia na kutafakari kile ambacho umekiomba na kukupa muda wa kuyafahamu majibu na njia ambayo Mungu ameitumia kukujibu.Mungu anaweza kukujibu kupitia maandiko,anaweza kukujibu kupitia mtu au watu,anaweza kukujibu kupitia mazingira na matukio fulani fulani,anaweza kukujibu kwa sauti yake waziwazi ikitoka kwenye ukuta wa chumba chako,anaweza kukujibu kupitia ndoto,pia anaweza kukujibu kwa yeye kukaa kimya bila kusema chochote.Kwa maana ukimya wa Mungu nao ni jibu au majibu.Maandiko yanasema kwamba Ukae kimya mbele za Bwana,Nawe umngojee kwa saburi;Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia zake,Wala mtuafanyaye hila.Zaburi 37:7.Nalikuwa sisemi,nalinyamaa,Sina faraja,maumivu yangu yakazidi.Zaburi 39:2.Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya,Wokovu wangu hutoka kwake.Zaburi 62:1,5.76:8,94:17,115:17.Md 8:32,9:7.Ufu 8:1Kwa hiyo ukitaka maombi yako yajibiwe yaishi hayo.

 

Kimeandikwa na

Bishop Rhobinson S.Baiye

rhobinsons.blogspot.com

rhobinsonsaleh1@gmail.com

Whatsapp.0764127531

Mwanza Tanzania

 

 

 


No comments:

Post a Comment

UONGOZI BORA WA KIROHO

Sauti Ya Gombo International Ministries Network KIONGOZI BORA WA KIROHO BISHOP: RHOBINSON S.BAIYE YALIYOMO: 1.Maana...